-
Tsunami ya kujiua katika jeshi la Marekani, nembo ya mgogoro wa kinafsi na kimaadili
Jun 26, 2021 10:31Ripoti ya karibuni ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) inaonesha ongezeko la visa vya kujiua kati ya wanajeshi wa nchi hiyo hususan maveterani wa jeshi.
-
Ansarullah: Hatujawahi na kamwe hatutafuti utambulisho wetu kutoka kwa Marekani
Jun 26, 2021 02:46Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya harakati ya Ansarullah ya Yemen ametuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter na kusisitiza kuwa, harakati hiyo ya wananchi wa Yemen kamwe haijawahi kufikiria kutafuta utambulisho wake kutoka kwa Marekani na haina haja ya kutambuliwa rasmi na dola hilo la kiistikbari.
-
Afisa wa polisi aliyemuua George Floyd afungwa miaka 22.5 nchini Marekani
Jun 26, 2021 02:46Mahakama ya Minnesota nchini Marekani imemuhukumu kifungo cha miaka 22 na nusu afisa wa polisi aliyemuua kikatili George Floyd, Mmarekani mwenye asili ya Afrika, aliyeuliwa kikatili mchana kweupe na afisa huyo mzungu mwenye chuki za kibaguzi.
-
Russia: Uingereza na Marekani zinataka kuzusha mzozo na vita katika Bahari Nyeusi
Jun 25, 2021 22:10Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia amesema kuwa, Uingereza na Marekani zinafanya njama za kuanzisha mzozo na vita katika Bahari Nyeusi.
-
Utafiti: Askari wa US wanaojiua ni wengi zaidi ya wanaokufa vitani
Jun 22, 2021 21:59Utafiti mpya umefichua kuwa, idadi ya askari wa Marekani na maveterani wa kijeshi wa nchi hiyo wanaoaga dunia kwa kujitoa uhai ni mara nne zaidi ya wanajeshi wa dola hilo la kibeberu wanaouawa vitani katika vita vinavyoanzishwa na Washington kila uchao tokea Septemba 11 mwaka 2001.
-
Uporaji wa mali ya Syria na Iraq, sababu ya mashinikizo ya wananchi ya kutaka wavamizi wa Kimarekani waondoke
Jun 21, 2021 22:01Kuwepo kwa majeshi vamizi ya Marekani katika eneo lolote la Magharibi mwa Asia na hata maeneo mengine ya dunia daima kumekuwa sababu ya ukosefu wa amani na mashaka na machungu kwa wakazi wa maeneo hayo, tofauti kabisa na madai yanayotolewa na serikali ya Washington.
-
Ansarullah yakosoa kauli ghalati ya jenerali wa kijeshi wa US dhidi ya Yemen
Jun 20, 2021 22:19Mwanachama wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen amemkosoa vikali Kamanda Mkuu wa Kamandi Kuu ya Kijeshi ya Marekani (CENTCOM) kwa kutoa matamshi yasiyo na msingi kuwa Sanaa imekataa kuketi kwenye meza ya mazungumzo na kusisitiza kuwa, afisa huyo wa Washington hana ufahamu wowote kuhusu siasa.
-
Kim ataka Korea Kaskazini ijiandae kwa makabiliano na Marekani
Jun 19, 2021 00:34Kiongozi wa Korea Kaskazini amesema nchi hiyo inakaribisha mpango wowote wa kufanyika mazungumzo mapya baina yake na Marekani, lakini kamwe haiweza kuondoa mezani chaguo la vita.
-
Biden atafakari kuvirejesha vikosi vya Marekani nchini Somalia
Jun 17, 2021 03:04Rais wa Marekani, Joe Biden anatafakari kuwarejesha wanajeshi wa nchi hiyo huko Somalia, eti kwenda kusaidia juhudi za kupambana na magaidi wa kundi la ukufurishaji la al-Shabaab.
-
Uzinduzi wa Stratijia ya Kitaifa ya Kupambana na Ugaidi wa Ndani nchini Marekani
Jun 16, 2021 23:07Ikulu ya Rais wa Marekani, White House, Jumanne wiki hii ilizindua Stratijia ya Kitaifa ya Kupambana na Ugaidi wa Ndani (National Strategy for Countering Domestic Terrorism) ambayo imetayarishwa na Baraza la Usalama wa Taifa. Kwa mujibu wa hati hiyo, taasisi zote za utekelezaji ndani ya Marekani zinalazimika kupambana na aina mbalimbali za ugaidi wa ndani ya nchi hiyo.