-
Msafara wa wanajeshi vamizi wa Marekani washambuliwa kusini mwa Iraq
Apr 13, 2021 22:06Duru za habari za Iraq zimetangaza kuwa, msafara wa magari yaliyokuwa yamepakia vifaa mbalimbali na zana za kijeshi kwa ajili ya wanajeshi vamizi wa Marekani umeshambuliwa kusini mwa nchi hiyo.
-
Marekani yasimamisha chanjo ya corona ya Johnson & Johnson kwa hofu ya kuganda damu
Apr 13, 2021 22:05Marekani imesitisha matumizi ya chanjo ya virusi vya corona iliyotengenezwa na kampuni ya dawa ya nchi hiyo, Johnson and Johnson, ambayo kuna madai kuwa inasababisha kuziba kwa mishipa kama matokeo ya tatizo la kuganda kwa damu kwa watu waliopewa chanjo hiyo.
-
Kukiri Biden juu ya kuudhiwa na kubughudhiwa Waislamu nchini Marekani
Apr 13, 2021 21:52Rais Joe Biden wa Marekani amekiri katika ujumbe wake kwa mnasaba wa kuwadia mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani juu ya kuudhiwa na kubughudhiwa Waislamu katika jamii ya Marekani.
-
Marekani yasisitiza Israel ni mshirika wake wa kistratejia katika eneo
Apr 11, 2021 08:13Waziri wa Ulinzi wa Marekani amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel ni mshirika wa kistratejia wa nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi.
-
Mgogoro wa mauaji ya kiholela Marekani na kilio cha Joe Biden, rais wa nchi hiyo
Apr 09, 2021 22:01Rais Joe Biden wa Marekani amelalamikia vikali mashambulizi ya silaha moto na mauaji ya kiholela nchini humo na ametaka uhalifu huo ukomeshwe mara moja. Amesema, mashambulizi ya silaha moto Marekani ni sawa na ugonjwa wa kuambukiza na ni aibu kwa nchi hiyo kimataifa.
-
Walensky : Ubaguzi wa rangi ni tishio kwa mfumo wa afya wa Marekani
Apr 09, 2021 09:36Mkurugenzi wa Kituo cha Kudhibiti Magonjwa nchini Marekani amesema kuwa, ubaguzi wa rangi ni tishio kubwa kwa mfumo wa afya ya umma nchini humo.
-
Ushahidi mpya unaothibitisha uhusiano wa karibu wa Marekani na magaidi wa ISIS
Apr 09, 2021 06:36Marekani ina nafasi kubwa ya kuzuka na kupata nguvu magenge ya kigaidi hususan genge la kigaidi la Daesh (ISIS) hasa katika nchi za Kiislamu za Iraq na Syria. Sasa hivi ushahidi mpya umetolewa unaozidi kufichua uhusiano wa karibu sana baina ya Marekani na magaidi hao makatili.
-
Kikao cha pamoja cha JCPOA; matarajio ya kundi la 4+1 na matumaini ya Iran
Apr 08, 2021 03:37Kikao cha 18 cha Kamisheni ya Pamoja ya JCPOA kilifanyika juzi Jumanne huko Vienna mji mkuu wa Austria kwa kuhudhuriwa na wawakilishi wa kundi la 4+1 na pia Iran. Nchi wanachama wa mapatano ya JCPOA baada ya majadiliano na kuchunguza mapatano hayo zimekubaliana kuendeleza mashauriano katika ngazi ya kitaalamu ili kuiondolea Iran vikwazo.
-
Tathmini ya kikao cha tatu cha Baghdad na washington
Apr 07, 2021 22:07Duru mpya ya mazungumzo ya kistratijia baina ya Baghdad na Washington ilianza jana Jumatano kwa njia ya video. Taarifa iliyotolewa huko nyuma na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilisema kuwa mazungumzo hayo yatahusu usalama, namna ya kupambana na ugaidi, nishati na masuala ya kisiasa.
-
Araqchi: Mkutano wa Kamisheni ya Pamoja ya JCPOA Vienna ni chanya
Apr 07, 2021 03:17Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa ameashiria kuhusu mkutano wa jana Jumanne mjini Vienna wa Kamisheni ya Pamoja ya makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kusisitiza kuwa, muelekeo wa kikao hicho ni chanya na wenye kutia matumaini.