-
Badr: Marekani inakula njama ya kuwarejesha magaidi Iraq
Mar 21, 2021 04:35Mkuu wa Ofisi ya Shirika la Badr katika mkoa wa al-Anbar nchini Iraq amesema Marekani inapanga njama ya kuwarejesha magaidi katika mikoa ya magharibi mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Mwana wa Trump amfanyia istihzai rais wa Marekani, Joe Biden
Mar 20, 2021 23:50Mwana wa kiume wa rais wa zamani wa Marekani, amerusha katika mtandao wa Twitter kipande cha video kilichotengenezwa maalumu kwa ajili ya kumfanyia istihzai Joe Biden baada ya rais huyo wa Marekani kula mweleka mara tatu mfululizo wakati alipokuwa anapanda ngazi ya ndege.
-
Kikao cha Alaska na kukaririwa tuhuma za Marekani dhidi ya China
Mar 20, 2021 23:49Kushadidi mpambano baina ya Marekani na China tangu baada ya Joe Biden kushika hatamu za uongozi kumezifanya pande hizo mbili kuitisha kikao cha ngazi za juu ambacho kilifanyika Alkhamisi iliyopita katika eneo la Anchorage kwenye jimbo la Alaska.
-
Iran: Hatujapokea ujumbe wowote kutoka Marekani
Mar 20, 2021 04:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haijapokea ujumbe wowote kutoka kwa Marekani wala haina azma yoyote ya kuitumia Washington ujumbe.
-
Kuendelea siasa za uhasama za Marekani dhid ya Iran
Mar 20, 2021 04:24Ikiwa ni katika kuendeleza siasa za uhasama za Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Wizara ya Fedha ya Marekani imewatuhumu raia wengine 10 wa Iran kuwa wamekiuka vikwazo vya nchi hiyo dhidi ya Iran.
-
Rais wa Marekani 'ala mweleka' mara tatu na kuzidisha wasiwasi kuhusu uzima wake kimwili
Mar 20, 2021 00:10Rais Joe Biden wa Marekani ameteleza na kuanguka mara tatu wakati akipanda ndege ya rais Air Force One, hali ambayo imezidisha wasiwasi kuhusu uzima wa kimwili wa kiongozi huyo.
-
Madharau ya Biden dhidi ya Putin, na mzozo wa aina yake katika uhusiano wa Marekani na Russia
Mar 19, 2021 06:00Uhusiano wa Marekani na Russia tangu Rais Joe Biden aliposhika madaraka ya nchi katika White House mwezi Januari mwaka huu umekuwa ukidorora siku baada ya nyingine huku Washington ikiendelea kuzidisha misimamo ya kihasama na kiuadui dhidi ya Russia. Sasa makabiliano baina ya nchi hizo mbili yamefikia kiwango cha vita vya maneno baina ya marais wa nchi hizo.
-
Vitendo vya uhalifu vyaongezeka kwa asilimia 25 nchini Marekani
Mar 19, 2021 04:32Polisi ya Federali ya Marekani FBI imetangaza habari ya kuongezeka kwa asilimia 25 vitendo vya uhalifu na jinai nchini humo katika mwaka uliopita wa 2020.
-
Uingiliaji wa aina tofauti wa Marekani katika masuala ya ndani ya Yemen
Mar 18, 2021 10:43Jumanne ya tarehe 16 Machi, Idara ya Kiitikadi ya Vikosi vya Ulinzi vya Yemen ilitoa nyaraka mpya zinazobainisha juu ya uwepo wa kijeshi wa Marekani na vituo vya kijeshi vya Washington huko nchini Yemen na pamoja na uhusiano wa serikali ya wakati huo ya Ali Abdullah Saleh na mashirika ya kijsasu ya Marekani.
-
Kushindwa mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran
Mar 17, 2021 23:16Baada ya serikali ya Donald Trump, Rais wa zamani wa Marekani kutangaza kujitoa rasmi katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA mnao Mei 2018, serikali hiyo ilianza kutekeleza vikwazo vikali zaidi katika historia ya nchi hiyo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika fremu ya mchakato wa kile kilichotajwa kuwa mashinikizo ya juu zaidi dhidi ya nchi hii.