-
Maseneta wa Marekani watishia 'kuichukulia hatua' Saudia
Apr 11, 2020 09:19Maseneta wa Marekani wametishia kuangalia upya uhusiano wao na Saudi Arabia kutokana na hatua ya Riyadh ya kuendelea kuvutana na Russia juu ya bei ya mafuta ghafi ambayo imeiathiri pia Marekani.
-
Virusi vya Corona vyasababisha hasara ya dola bilioni moja katika utajiri wa Trump
Apr 08, 2020 22:11Gazeti la The Guardian limeeleza kuwa utajiri wa Rais Donald Trump wa Marekani, umepata hasara ya dola bilioni moja kutokana na kuenea virusi vya Corona.
-
Tishio la Marekani la kuikatia misaada WHO wakati huu wa corona
Apr 08, 2020 22:10Baada ya kuenea sana maambukizi ya kirusi cha corona nchini Marekani na kupamba moto lawama dhidi ya utendaji mbovu wa rais wa nchi hiyo katika kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19, Donald Trump amekuwa akitapatapa huku na huko kwa kutoa tuhuma zisizo na msingi. Huko nyuma aliilaumu China kuwa imechelewa kuijulisha Marekani kuhusu ugonjwa huo na sasa amelivurumishia Shirika la Afya Duniani WHO tuhuma hizo hizo na kutishia kulikatia misaada.
-
Kamisheni ya Usalama ya Bunge la Iraq yaonya kuhusu kupuuzwa uwepo wa Marekani nchini humo
Apr 08, 2020 08:36Mkuu wa Kamisheni ya Usalama na Ulinzi ya Bunge la Iraq ametahadharisha kuhusiana na kuendelea kuwepo majeshi ya Marekani katika kituo cha Ain al-Assad katika mkoa wa al-Anbar na al-Harir katika eneo lenye Mamlaka ya Ndani la Kurdestan.
-
Idadi ya wahanga wa corona huko New York ni zaidi ya wale wa mashambulio ya Septemba 11
Apr 08, 2020 03:25Idadi ya watu walioaga dunia kwa maambukizi ya virusi vya corona katika mji wa New York nchini Marekani ni zaidi ya wale waliofariki dunia katika mashambulizi ya Septemba 11 katika kituo cha kimataifa cha biashara mjini humo.
-
Raia weusi wanaathiriwa kwa wingi na corona Marekani huku UN ikionya kuhusu ubaguzi katika utoaji huduma
Apr 07, 2020 10:27Takwimu za majimbo mbali mbali nchini Marekani zinaonyesha kuwa jamii za raia weusi wenye asili ya Afrika ndizo zinazoathiriwa kwa wingi na maambukizo ya virusi vya corona.
-
Mgogoro wa corona umedhihirisha kuwa US haiwezi hata kujiongoza yenyewe
Apr 07, 2020 03:04Msaidizi Maalumu wa Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) katika masuala ya kimataifa amesema mgogoro wa ugonjwa wa Covid-19 (corona) umeudhihirishia ulimwengu kuwa, utawala wa kibeberu wa Marekani ambao unajiona kuwa kiongozi na mtawala wa dunia umeshindwa hata kujiongoza wenyewe.
-
Hitilafu za Russia na Saudia kuhusiana na bidhaa ya mafuta zaahirisha mkutano wa OPEC+
Apr 06, 2020 01:31Vita vya bei ya mafuta baina ya Russia na Saudi Arabia vilivyoanza baada ya kufeli mkutano wa mwanzoni mwa mwezi Machi uliopita wa OPEC+ mjini Vienna vimesababisha kuporomoka kwa bei ya bidhaa hiyo kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika kipini cha miaka 18 iliyopita.
-
Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq yatahadharisha juu ya malengo ya Marekani ya kubakia kwa muda mrefu nchini Iraq
Apr 05, 2020 22:03Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa wa Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq ya nchini Iraq ametahadharisha juu ya mipango ya Marekani ya kutaka kubakia kwa muda mrefu nchini humo.
-
Kissinger: Virusi vya corona vitabadili mfumo wa dunia, serikali ya Trump haina mwelekeo wala sifa
Apr 05, 2020 07:19Waziri wa zamani wa Marekani, Henry Kissinger, amesema katika makala yake iliyochapishwa kwenye gazeti la The Wall Street Journal kwamba, mlipuko wa maambukizi ya virusi vya corona utabadilisha mfumo wa dunia milele.