-
Sisitizo la Rais Maduro la uwezekano wa kufikiwa makubaliano na wapinzani kwa sharti Marekani iache kuingilia mambo ya Venezuela
Jul 10, 2019 03:20Kuendelea mgogoro wa kisiasa wa Venezuela na kushindwa wapinzani kuiangusha serikali ya Rais Nicolas Maduro kumemfanya Juan Guaido, kiongozi wa upinzani nchini humo akubali pendekezo la upatanishi wa Norway na kufanyika mazungumzo baina ya wapinzani na wawakilishi wa serikali ya Caracas.
-
UN yasikitishwa na hali mbaya inayowakabili wahajiri nchini Marekani
Jul 09, 2019 03:49Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa sanjari na kukosoa vikali sera za wahajiri za utawala wa Rais Donald Trump, ameeleza kusikitishwa kwake na hali mbaya inayowakabili wahajiri na wakimbizi nchini Marekani.
-
Ujerumani yakataa ombi la Marekani la kutuma askari Syria
Jul 09, 2019 03:48Rais Donald Trump wa Marekani Disemba mwaka 2018 aliwaahidi Wamarekani kwamba ataliondoa jeshi la nchi hiyo huko Syria. Trump alitoa ahadi hiyo katika kile kinachoaminika kuwa ni sehemu ya kutekeleza kampeni yakee ya kubakia ikulu ya White House.
-
Trump na balozi wa Uingereza washambuliana kwa maneno
Jul 08, 2019 03:16Rais Donald Trump amemshambulia vikali balozi wa Uingereza mjini Washington aliyemtaja kiongozi huyo wa Marekani kama mtu mtepetevu, asiye na tajriba na anayeendesha Ikulu ya White House kishaghalabaghala.
-
Iran: Ni haki yetu kuchukua hatua za kukabiliana na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani
Jul 07, 2019 22:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ni haki ya Tehran kuchukua hatua za kisheria ndani ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA katika kukabiliana na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani dhidi yake.
-
"Siasa za Marekani dhidi ya Iran zimefeli"
Jul 07, 2019 22:12Naibu wa Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, siasa za serikali ya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimefeli.
-
Hamas yaapa kudumaza mpango wa Trump wa "Muamala wa Karne"
Jul 06, 2019 21:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa itaendeleza harakati za kupinga mpango eti wa amani uliozusha makelele mengi wa Rais Donald Trump wa Marekani baina ya utawala haramu wa Israel na Wapalestina uliopewa jina la "Muamala wa Karne"
-
Afrika Kusini: Hatutaruhusu uchumi wetu udumazwe na wivu wa Marekani
Jul 06, 2019 08:25Rais wa Afrika Kusini amesema nchi hiyo kamwe haitaruhusu uchumi wake uvurugwe na kurejeshwa nyuma kutokana na vita vya kibiashara vya Marekani, vilivyochechewa na wivu.
-
Ukosoaji wa Russia kuhusu mkinzano uliopo kati ya shaari na hatua za Ulaya katika kulinda makubaliano ya JCPOA
Jul 06, 2019 07:19Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Uingereza ambazo ni nchi wanachama wa Ulaya katika kundi la 4+1 mara kwa mara zimekuwa zikisisitiza juu ya ulazima wa kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA; na hata kudai kuwa zimeanzisha mfumo maalumu kwa lengo hilo. Pamoja na hayo, shaari na nara zinaotolewa na pande hizo za Ulaya zinakinzana na matendo yao.
-
Wasaudia waendelea kulalamikia kualikwa mwanamuziki mcheza uchi nchini mwao
Jul 05, 2019 10:42Wanaharakati wengi wa mitandao ya kijamii na wananchi wa Saudi Arabia wamekasirishwa mno na kualikwa mwanamuziki mmoja wa RAP wa Kimarekani katika tamasha la muziki la mjini Jeddah.