-
Magaidi 21 waangamizwa Rasi ya Sinai nchini Misri
May 10, 2018 09:17Jeshi la Misri limetangaza habari ya kuangamizwa magaidi 21 katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na jeshi na polisi wa nchi hiyo katika Rasi ya Sinai.
-
Serikali ya Misri yalaumiwa kwa kuwatesa wafungwa
May 07, 2018 10:36Shirika la Kimataifa la Msahama Duniani la Amnesty International limelaani mateso wanayofanyiwa wafungwa na serikali ya Misri ikiwa ni pamoja na kuwekwa wafungwa wa kisiasa kwenye seli za mtu mmoja mmoja kwa muda mrefu na kusema kuwa, huo ni ushahidi wa wazi wa namna serikali ya Rais Abdul Fattah el Sisi inavyowatesa wafungwa nchini humo.
-
Misri: Inawezekana kutuma nchini Syria vikosi vya Kiarabu
May 04, 2018 09:04Misri imesema kuwa mazungumzo yanaendelea kufanyika baina ya maafisa wa nchi kadhaa kujadili pendekezo la Marekani la kuunda jeshi la Kiarabu litakalochukua nafasi ya wanajeshi wa Marekani waliopo Syria.
-
Al Sisi aahidi kuhitimisha oparesheni za jeshi huko Sinai
Apr 29, 2018 03:10Rais wa Misri ametangaza kuwa oparesheni za jeshi la nchi hiyo katika mkoa wa Sinai ya Kaskazini zitahitimishwa hivi karibuni.
-
Darul Iftaa ya Misri yakosoa ombi la shakhsia 300 wa Ufaransa
Apr 25, 2018 10:03Katibu wa Idara Kuu ya Misri inayohusika na Fatwa za Kiislamu (Darul Iftaa) amekosoa ombi lililowasilishwa na shakhsia 300 wa Ufaransa waliotaka kuondolewa baadhi ya aya katika kitabu kitakatifu cha Qur'ani.
-
Misri na Imarati zatuhumiwa kuvuruga mchakato wa mapatano ya kitaifa Libya
Apr 24, 2018 11:54Jumuiya ya International Action Group for Libya imezituhumu nchi za Imarati na Misri kuwa zinavuruga jitihada zinazofanywa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mapatano ya kitaifa nchini Libya.
-
Viongozi wengi wa Ikhwanul Muslimin ya Misri wawekwa katika orodha ya magaidi
Apr 23, 2018 12:10Mahakama ya Misri imeweka idadi kubwa ya maafisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Ikhwanul Muslimin katika orodha ya magaidi.
-
Sheikh wa al-Azhar: Beitul-Muqaddas ni ardhi ya Waislamu
Apr 21, 2018 23:17Sheikh Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha al-Azhar nchini Misri amesema kuwa, Beitul-Muqaddas ni ardhi ya Kiislamu na daima itaendelea kuubakia kuwa ni ya Kiislamu.
-
Sudan yaishtaki Misri kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
Apr 18, 2018 12:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan amewasilisha mashtaka ya nchi yake dhidi ya Misri kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya Misri kuendesha uchaguzi wa rais katika maeneo ya mpakani yanayogombaniwa ya Halaib na Shalateen.
-
Rais wa Misri arefusha hali ya hatari kwa miezi mingine mitatu
Apr 14, 2018 02:31Rais Abdul Fattah al-Sisi wa Misri ametangaza kurefusha muda wa hali ya hatari nchini humo kwa miezi mitatu mingine ambao ulianza kutekelezwa mwezi Aprili mwaka jana baada ya kujiri mashambulizi makubwa dhidi ya makanisa.