-
Jumuiya ya Wayahudi wa Iran yataka kulipiza kisasi baada ya Israel kumuua Haniyeh
Aug 04, 2024 02:23Jumuiya ya Wayahudi wa Iran imelaani vikali mauaji yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya kiongozi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) Ismail Haniyeh akiwa ugenini mjini Tehran, ikitoa wito wa kulipiza kisasi dhidi ya mauaji hayo.
-
Baada ya UN, Iran yaitaarifu EU: Tutalitia adabu genge la wahalifu la utawala wa Kizayuni wa Israel
Aug 03, 2024 06:57Iran itatumia haki yake ya asili na halali ya kuliadhibu "genge la wahalifu la Kizayuni" kwa shambulio lake la kigaidi la siku ya Jumatano iliyopita, ambalo lilipelekea kuuawa mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) Ismail Haniyeh mjini Tehran.
-
UN: Wapalestina Gaza wanahitaji chanjo haraka ili kuzuia polio
Jul 31, 2024 02:40Katika jitihada za kuzuia janga la ugonjwa wa polio huko Gaza, mashirika ya misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa jana Jumanne yalikariri wito wa kufanyika jitihada za kimataifa za kuutaka utawala wa Israel usitishe vita ili kuruhusu kampeni kubwa ya utoaji chanjo kuanza.
-
Rais mpya wa Iran: Sera za Iran katika kuitetea Palestina haziwezi kubadilika
Jul 30, 2024 07:37Rais mpya wa Iran amesema alipoonana na kuzunguzma na Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina kuwa misimamo na sera za mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kuwaunga mkono waliodhulumiwa wakiwemo wananchi wa Palestina haziwezi kubadilika.
-
Tovuti ya Uingereza: Utawala wa Marekani ni kipofu kiasi kwamba unamhami mtu kama Netanyahu
Jul 30, 2024 02:29"Kuporomoka kwa dola kunakuwa jambo lisiloepukika mara tu watawala wake wanapopoteza kabisa hisia za jinsi walivyokuwa wapuuzi na wa kutisha", hivi ndivyo ilivyoandika tovuti ya Uingereza ya Middle East Eye ikizungumzia fedheha kubwa ya Congress ya Marekani ya kumkaribisha na kumpigia makofi nduli na Adolf Hitler wa zama hizi, Benjamin Netanyahu, anayeendelea kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Ripoti ya mashirika ya UN: Ghaza ina hali mbaya zaidi ya uhaba wa chakula duniani
Jul 27, 2024 11:35Ripoti mpya ya pamoja iliyotolewa na mashirika matano ya Umoja wa Mataifa imeeleza kuwa Ukanda Ghaza uliowekewa mzingiro na kuzuiliwa na jeshi la Kizayuni kuingiziwa misaada ya chakula, ndilo eneo linalokabiliwa na hali mbaya zaidi ya ukosefu wa chakula duniani.
-
HAMAS: Kauli ya Marekani ni uongo mtupu, Wapalestina Ghaza wanauawa kwa silaha zake
Jul 26, 2024 12:59Mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: "Madai ya Washington kwamba inatiwa wasiwasi na hali ya kibinadamu na inasikitishwa na machungu na mateso wanayopata watu wa Ghaza ni uongo wa Kimarekani".
-
Amnesty International: Marekani mshirika wa Israel katika mauaji ya kimbari Palestina
Jul 25, 2024 07:11Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International imeonya Marekani kuhusu kuupa silaha utawala wa Kizayuni katika vita vya Gaza na kutangaza kuwa, Washington ni mshirika wa utawala huo katika mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
-
Kufanyika kura ya maoni Palestina; mkakati na suluhisho la Iran
Jul 23, 2024 13:59Nasser Kanani, msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, "suluhisho bora zaidi la kuhitimisha hali haramu ya sasa katika Palestina inayokaliwa kwa mabavu ni kufanyika kura ya maoni jumuishi kwa kushirikisha wakaazi wote na raia asili wa ardhi hiyo."
-
Ripota wa Umoja wa Mataifa akosoa vitendo vya kibaguzi vya utawala wa Israel
Jul 23, 2024 02:25Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu huko Palestina amekosoa mienendo ya kikatili ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina.