-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kuhusu kukaribia kuangamia utawala wa Kizayuni katika eneo
May 23, 2020 02:38"Bila shaka kirusi cha Uzayuni hakitadumu kwa muda mrefu na kwa kutegemea hima, imani, ghera ya vijana, mizizi ya kirusi hicho itang'olewa na kuondolewa katika eneo".
-
Chama cha Republican cha Tunisia: Umoja na muqawama, njia pekee ya kuikomboa Palestina
May 22, 2020 08:07Katibu Mkuu wa chama cha Republican cha Tunisia amesema utawala ghasibu wa Israel hauelewi lugha nyingine isipokuwa ya mapambano na kusisitiza kuwa, "umoja na muqawama ndiyo njia pekee ya kuikomboa Palestina."
-
"Siku ya Kimataifa ya Quds ni nembo ya uvumilivu, umoja na mshikamano wa Waislamu"
May 22, 2020 03:17Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameielezea Siku ya Kimataifa ya Quds inayoadhimishwa hii leo kote duniani kama utamaduni mzuri na nembo ya uvumilivu, umoja na mshikamano wa Waislamu katika kuhami na kutetea thamani za Kiislamu.
-
Siku ya Kimataifa ya Quds: Viongozi wa Hamas, Ansarullah na Hizbullah wazungumza
May 21, 2020 03:01Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema "Muamala wa Karne" unakusudia kusambaratisha kadhia ya Palestina.
-
Maadhimisho ya Siku ya Quds kufanyika kwenye mitandao ya kijamii Afrika Kusini
May 12, 2020 14:51Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds ya mwaka huu yanatazamiwa kufanyika katika ukumbi wa Instagram na mitandao mingine ya kijamii nchini Afrika Kusini, kutokana na janga la corona.
-
Israel yamkamata mkurugenzi katika Shirika la Wakfu Quds
Mar 17, 2020 01:41Utawala wa Kizayuni wa Israel umemkamata Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Wakfu wa Kiislamu katika mji wa Quds (Jerusalem) huku kukiwa na tetesi kuwa Wazayuni wanalenga kumuambukiza kirusi cha corona.
-
Marekani yatekeleza njama mpya dhidi ya Wapalestina kwa kubadilisha utambulisho wa wakazi wa Quds
Mar 12, 2020 15:33Harakati ya Kidemokrasia kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina imesema, hatua ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani ya kubadilisha utambulisho wa Wapalestina wa eneo la Baitul Muqaddas Mashariki ni hujuma ya dhahiri na uchokozi wa wazi dhidi ya utambulisho wa Wapalestina.
-
Sanders: Nikichaguliwa kuwa rais nitaurejesha ubalozi wa US Tel Aviv
Feb 27, 2020 02:25Seneta wa jimbo la Vermont nchini Marekani anayeongoza katika mbio za kuwakilisha chama cha Democratic katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo amemtaja Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Benjamin Netanyahu kama mbaguzi asiyependa ustawi wa kisiasa na kijamii.
-
Rais wa Tunisia: Quds ni mji mkuu wa Palestina, si bidhaa ya kuuzwa
Feb 25, 2020 07:48Rais Kais Saied wa Tunisia amesema Palestina ni milki ya Wapalestina na Quds tukufu inapaswa kuwa mji mkuu wa taifa hilo la Kiarabu.
-
Sayyid Ammar al Hakim: Quds ni utambulisho wa Waislamu wote
Feb 02, 2020 02:42Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq amelaani njama mpya za rais wa Marekani Donald Trump za "Muamala wa Karne" ambazo zinalenga kuwapora Waislamu maeneo yao matakatifu hasa Kibla chao cha Kwanza yaani Msikiti wa al Aqsa na kusisitiza kuwa, rais wa Marekani anapaswa kutambua kuwa Quds ni utambulisho wa Waislamu wote na watasimama kidete kulilinda eneo lao hilo takatifu kwa nguvu zao zote.