-
Rais Rouhani: Endapo Marekani itatekeleza ahadi zake, sisi pia tutafanya hivyo
Mar 31, 2021 07:20Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, endapo kutakuwa na azma imara na Marekani ikarejea katika mazingira ya kabla ya vikwazo, sisi pia siku hiyo hiyo tutaanza kutekeleza ahadi zetu.
-
Wakazi wa Kanda ya Ziwa Tanzania wamuaga Magufuli, Majaliwa asema ameacha alama kote nchini
Mar 24, 2021 09:54Wananchi wa Mwanza na mikoa jirani ya Kanda ya Ziwa nchini Tanzania wamejitokeza kwa wingi kwenye barabara na mitaa ya Mwanza kumuaga aliyekua Rais wa Tanzania, Dk John Magufuli.
-
Madharau ya Biden dhidi ya Putin, na mzozo wa aina yake katika uhusiano wa Marekani na Russia
Mar 19, 2021 06:00Uhusiano wa Marekani na Russia tangu Rais Joe Biden aliposhika madaraka ya nchi katika White House mwezi Januari mwaka huu umekuwa ukidorora siku baada ya nyingine huku Washington ikiendelea kuzidisha misimamo ya kihasama na kiuadui dhidi ya Russia. Sasa makabiliano baina ya nchi hizo mbili yamefikia kiwango cha vita vya maneno baina ya marais wa nchi hizo.
-
Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania afariki dunia
Mar 17, 2021 23:43Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefariki dunia katika Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
-
Kushindwa mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran
Mar 17, 2021 23:16Baada ya serikali ya Donald Trump, Rais wa zamani wa Marekani kutangaza kujitoa rasmi katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA mnao Mei 2018, serikali hiyo ilianza kutekeleza vikwazo vikali zaidi katika historia ya nchi hiyo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika fremu ya mchakato wa kile kilichotajwa kuwa mashinikizo ya juu zaidi dhidi ya nchi hii.
-
Somalia yazindua kampeni ya kitaifa ya utoaji chanjo ya Corona
Mar 17, 2021 01:10Rais Mohamed Abdullahi Farmaajo wa Somalia hapo jana alipokea chanjo ya Corona ya shirika la AstraZeneca la Uingereza, kuashiria kuanza kwa kampeni ya kitaifa ya utoaji wa chanjo ya Corona katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Rouhani: Kufidia makosa yaliyofanywa na serikali iliyopita ya Marekani ni kwa manufaa ya wote
Mar 16, 2021 09:01Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kufidia makosa yaliyofanywa na serikali iliyopita ya Marekani si kwa manufaa ya Iran tu bali ni kwa maslahi ya Marekani yenyewe , eneo na taasisi za kimataifa.
-
Kuvunjwa Bunge na mwanzo wa kipindi kipya cha kisiasa nchini Algeria
Feb 20, 2021 06:47Katika miaka ya karibuni Algeria imekumbwa na misukosuko na matukio mengi ya kisiasa. Tukio la karibuni kabisa nihatua ya Rais Abdelmadjid Tebboune wa nchi hiyo ya kulivunja Bunge na kuitisha uchaguzi wa mapema. Tebboune alitangaza hatua hiyo Alkhamisi iliyopita katika hotuba yake kwa taifa iliyotolewa kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Shahidi.
-
Biden akiri, ubaguzi wa rangi unaendelea kuitafuna jamii ya Marekani
Feb 19, 2021 04:38Ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kimbari na ukatili dhidi ya watu weusi daima vimekuwa miongoni mwa sifa kuu za jamii ya Marekani tangu nchi hiyo ilipoasisiwa, na hadi sasa Wamarekani weusi wangali wanasumbuliwa na aina mbalimbali za ubaguzi na ukatili.
-
Hatua mpya ya chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa
Feb 18, 2021 22:53Mwenendo wa chuki dhidi ya Uislamu na kushadidi mashinikizo dhidi ya Waislamu nchini Ufaransa unaonekana kushtadi na kuchukua mkondo mpana zaidi katika miaka ya hivi karibuni katika nchi hiyo ya bara Ulaya.