-
Baada ya vitisho, Marekani yatangaza tarehe ya kujiondoa WHO
Sep 04, 2020 02:40Miezi michache baada ya Marekani kuamua kulikatia misaada yote ya kifedha Shirika la Afya Duniani kwa madai kwamba linadhibitiwa na China, sasa utawala wa Donald Trump umeenda mbali zaidi ya kuainisha tarehe ya kujiondoa WHO.
-
WHO yatahadharisha kuhusu ufisadi katika ugavi wa vifaa vya tiba na kujikinga na corona
Aug 22, 2020 04:18Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ametahadharisha kuwa, ufisadi unaoonekana katika ugavi wa vifaa na zana za madaktari na wauguzi kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa COVID-19 ni kielelezo cha uhalifu na jinai.
-
WHO: Covid-19 ni janga baya zaidi la afya linaloikabili dunia
Jul 28, 2020 00:13Maambukizi mapya ya virusi vya corona yaliyopelekea watu zaidi ya milioni 16 kuathiriwa na virusi hivyo ni janga baya zaidi la kiafya duniani kuwahi kulikumba Shirika la Afya Duniani (WHO).
-
Burundi yawatimua nchini humo maafisa wa WHO wakati huu wa corona
May 14, 2020 19:58Serikali ya Burundi imemfukuza nchini humo Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini humo na maafisa watatu wa timu yake waliokuwa wakifuatilia mwenendo wa mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19 (corona) katika nchi hiyo.
-
WHO: Kulegezwa vizuizi vya watu kubaki majumbani kutaibua changamoto
May 13, 2020 09:02Wakati idadi ya watu waliougua ugonjwa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya corona ikifikia zaidi ya milioni 4 duniani kote, Shirika la Afya Duniani, WHO limesema, hatua ya baadhi ya nchi kulegeza vizuizi vya watu kubakia majumbani imeonesha baadhi ya changamoto zitakazoyakabili mataifa siku za usoni.
-
China yaipa WHO dola milioni 50 baada ya US kulikatia misaada shirika hilo la UN
Apr 23, 2020 22:02China imeliongeza Shirika la Afya Duniani (WHO) msaada wa dola milioni 30 za Marekani za kudhibiti mlipuko wa maambukizi ya virusi vya Corona duniani, siku chache baada ya Marekani kuikatia misaada taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa.
-
Hatua ya Marekani ya kusitisha mchango wake wa kifedha kwa Shirika la Afya Duniani
Apr 15, 2020 08:22Rais Donald Trump wa Marekani ametelekeza kivitendo tishio lake la kusitisha mchango wa kifedha ya nchi hiyo kwa shirika la Afya Duniani (WHO). Trump amedai kuwa, WHO imefeli katika kutekeleza majukumu yake.
-
UN yakerwa na hatua ya Trump kuikatia ufadhili WHO wakati huu wa Corona
Apr 15, 2020 03:44Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitizia udharura wa kuungwa mkono Shirika la Afya Duniani (WHO), muda mfupi baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kutangaza kuwa nchi hiyo imelikatia misaada yake ya kifedha shirika hilo.
-
WHO yatangaza mlipuko wa homa ya njano Sudan Kusini
Apr 14, 2020 08:40Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza habari ya mlipuko wa homa ya njano katika maeneo ya kusini mwa Sudan Kusini.
-
Tishio la Marekani la kuikatia misaada WHO wakati huu wa corona
Apr 08, 2020 22:10Baada ya kuenea sana maambukizi ya kirusi cha corona nchini Marekani na kupamba moto lawama dhidi ya utendaji mbovu wa rais wa nchi hiyo katika kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19, Donald Trump amekuwa akitapatapa huku na huko kwa kutoa tuhuma zisizo na msingi. Huko nyuma aliilaumu China kuwa imechelewa kuijulisha Marekani kuhusu ugonjwa huo na sasa amelivurumishia Shirika la Afya Duniani WHO tuhuma hizo hizo na kutishia kulikatia misaada.