-
Sudan yakanusha taarifa za UN kuhusu Al-Burhan kukubali kukutana na Hemedti nchini Uswisi
Feb 09, 2024 04:40Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Sudan jana Alhamisi ilikanusha taarifa iliyotolewa na Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, Martin Griffiths, ambaye alidokeza kuwa Rais wa Baraza Kuu la Utawala nchini Sudan, Jenerali Abdel Fattah Al-Burhan, amekubali kukutana na Kamanda wa Kikosi cha Msaada wa Haraka, Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), nchini Uswisi, kwa madhumuni ya kuwezesha kuwasili kwa misaada kwa watu walioathirika na vita huko Sudan.
-
MSF: Watoto 13 wanaaga dunia kila siku kambini Darfur, Sudan
Feb 06, 2024 07:29Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) imesema kwa akali watoto 13 wanafariki dunia kila siku kutokana na utapiamlo wa kiwango cha juu katika kambi moja ya wakimbizi nchini Sudan.
-
Rais Raisi: Sera ya msingi ya Iran ni kuunga mkono nchi zinazojitenga na Israel
Feb 05, 2024 23:30Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema sera ya msingi ya Jamhuri ya Kiislamu ni kuunga mkono nchi zinazojitenga na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Amir Abdollahian: Ni muhimu kufunguliwa tena balozi za Iran na Sudan ili kupanua ushirikiano
Feb 05, 2024 12:04Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa suala la kufunguliwa tena balozi za Iran na Sudan na kurejea shughuli za mabalozi wa nchi hizo mbili kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano wa pande zote lina umuhimu mkubwa, na kueleza kwamba kuna matumaini ya kustawishwa zaidi ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
-
ICC: Tunaamini pande zote mbili za vita nchini Sudan zimefanya uhalifu wa kivita Darfur
Jan 30, 2024 08:00Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, Karim Khan, ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba kuna "sababu za kuamini" kwamba jeshi la Sudan, Vikosi vya Msaada wa Haraka, na vikundi washirika wao wamefanya uhalifu wa kivita huko Darfur.
-
EU yayawekea vikwazo makampuni sita yanayodaiwa kuhusika katika kufadhili vita Sudan
Jan 22, 2024 23:51Baraza la Ulaya limeidhinisha vikwazo kwa makampuni sita yanayodaiwa kuhusika katika kufadhili vita nchini Sudan, ambapo vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo (SAF) na Wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) wamekuwa wakipigana tangu Aprili mwaka jana.
-
UN: Zaidi ya watu 13,000 wameuawa katika vita vya Sudan
Jan 22, 2024 03:59Zaidi ya watu 13,000 wameuawa na wengine 26,000 kujeruhiwa katika vita vinavyoendelea nchini Sudan tangu mwaka jana, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya kibinadamu imetangaza Jumapili.
-
Mapigano ya kikabila yameua zaidi ya 15,000 katika mji mmoja Sudan
Jan 20, 2024 03:51Ripoti ya Umoja wa Mataifa imesema watu kati ya 10,000 na 15,000 waliuawa katika ghasia na mapigano ya kikabila mwaka jana katika mji mmoja ulioko katika jimbo la Darfur Magharibi nchini Sudan.
-
Ethiopia na Sudan zasusia mkutano wa Jumuiya ya IGAD
Jan 18, 2024 07:22Ethiopia imesema mkutano wa Wakuu Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali (IGAD) umefanyika leo Alhamisi huku ikiwa na mipango mengine. Wakati huo huo Sudan pia imedai kuwa haikushirikishwa katika ajenda ya mkutano huo.
-
Vita vya Sudan vyapanuka hadi katika mabaki ya ufalme wa kale wa Kush
Jan 17, 2024 23:24Vita vikali vya miezi tisa huko Sudan kati ya majenerali wawili hasimu vimepanuka zaidi hadi kwenye eneo la Urithi wa Dunia wa Shirika la UNESCO. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika lisilo la kiserikali la The Regional Network for Cultural Rghts.