-
Serikali ya Tanzania yawataka raia wachukue tahadhari ya magonjwa ya kuambukiza
Dec 18, 2021 04:44Wizara ya Afya ya Tanzania imewataka raia kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya kuambukiza, wakati huu hospitali nyingi nchini humo, zikiripoti ongezeko la wagonjwa wanaougua mafua, kifua na maumivu ya viungo.
-
Mkuu wa Kanisa la Kilutheri Tanzania aomba Wimbo wa Taifa ubadilishwe
Dec 07, 2021 12:27Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Fredrick Shoo, ameomba neno HAKI liongezwe katika wimbo wa taifa hilo, akisisitiza kuwa ni tunda la amani ya nchi.
-
Sisitizo la Rais wa Tanzania kwa mkutano wa COP26: Tunapimwa kwa vitendo vyetu, si kwa ahadi kubwa kubwa tunazotoa
Nov 02, 2021 04:09Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaeleza viongozi wa mataifa ya dunia wanaohudhuria mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP26 huko Glasgow, Scotland, kwamba mshikamano na juhudi zao kama viongozi katika kukabili mabadiliko ya tabianchi vitapimwa si kwa ahadi kubwa wanazotoa kwenye mkutano huo bali kwa jinsi watakavyotekeleza vipengele vyote vya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi.
-
Rais wa Tanzania: Tutaendelea Kushirikiana na Burundi
Oct 22, 2021 11:13Tanzania imesema itaendelea kushirikiana na Burundi katika kuimarisha ulinzi katika mipaka ya nchi hizo mbili. Hayo yamesemwa na Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mazungumzo yake huko Chamwino Dodoma na Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye ambaye yupo nchini humo kwa ziara ya siku tatu.
-
Mamilioni ya Watanzania wanasumbuliwa na matatizo ya akili
Oct 10, 2021 04:26Tanzania inakadiriwa kuwa na watu milioni saba wenye matatizo yanayohusiana na afya ya akili. Hayo yamebainika wakati huu ambapo nchi hiyo ya Afrika Mashariki imejiunga na nchi zingine duniani hii leo kuadhimisha Siku ya Afya ya Akili.
-
Rais Samia awaomba Watanzania ushirikiano katika kutekeleza ahadi zake UN
Sep 25, 2021 11:48Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameomba ushirikiano wa Watanzania ili kuyatekeleza kwa vitendo yale aliyoahidi katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York huko Marekani.
-
Mahakama ya Tanzania yamfutia mashtaka ya uchochezi Tundu Lissu na wenzake watatu
Sep 22, 2021 10:07Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es salaam, Tanzania imefuta mashtaka dhidi ya makamu mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu na wenzake watatu, baada ya upande wa mashtaka wa serikali ya nchi hiyo kutangaza leo kuwa hauna nia tena ya kuendelea na mashtaka yote matano uliyokuwa umefungua dhidi ya washtakiwa hao.
-
Rais wa Tanzania azindua kampeni ya uelimishaji kuhusu sensa ya mwaka 2022
Sep 14, 2021 07:56Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amezitaka mamlaka zinazoshughulikia zoezi la sensa lililopangwa kufanyika mwakani kutumia gharama ndogo na kufanya zoezi hilo kwa ufanisi kwani serikali haina pesa ya kubeba gharama kubwa.
-
Mkuu wa Jeshi la Polisi ya Tanzania: Polisi itakagua yanayofundishwa nyumba za ibada
Sep 11, 2021 09:00Jeshi la Polisi Tanzania limesema kuwa litakuwa likipita katika nyumba za ibada kukagua mafunzo wanayofundishwa watoto katika madrasa na shule za Jumapili (Sunday Schools) kufahamu aina ya mafundisho yanayotolewa.
-
Baada ya miaka kadhaa, mara hii Rais wa Tanzania atashiriki mkutano wa Baraza Kuu la UN
Sep 04, 2021 03:30Kwa mara ya kwanza, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kushiriki katika mkutano wa kila mwaka wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambao katika ngazi ya viongozi wakuu, unatarajiwa kuanza tarehe 21 mpaka 27 za mwezi huu wa Septemba 2021.