-
Hatimaye bunge la Tanzania lapitisha azimio la kutofanya kazi na CAG, wapinzani wakataa
Apr 02, 2019 09:42Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha azimio la kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.
-
Maalim Seif: Inaniuma kukihama Chama cha Wananchi Tanzania CUF
Apr 01, 2019 10:43Kinara wa siasa za upinzani visiwani Zanzibar na pia mwanachama namba moja wa chama cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania, Maalim Seif Sharif Hamad amesema hatua yake ya kuondoka katika Chama cha Wananchi (CUF) imeacha majonzi moyoni mwake.
-
SAUTI, Rais Mstaafu wa Tanzania Dr Jakaya Kikwete, aipongeza Shia Ithna Asharia JAMAT kwa kupambana na maradhi ya Usonji
Mar 31, 2019 11:28Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne nchini Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete, ameongoza mamia ya Watanzania katika matembezi ya kuadhimisha siku ya utokomezaji wa maradhi ya usonji duniani jijini Dar es Salaam.
-
Mahakama EACJ yaitaka Tanzania kuondoa vifungu kandamizi katika Sheria Ya Vyombo Vya Habari
Mar 28, 2019 10:43Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ) imekipa ushindi Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Baraza la Habari Tanzania (MCT) pamoja na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kesi Namba 2 ya mwaka 2017 ya kupinga vifungu kandamizi katika Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari, 2016.
-
Maalim Seif: Ndugu yangu Magufuli jiulize je, unatenda haki? Kumbuka utaenda kujibu kwa Mungu
Mar 27, 2019 11:52Mwanachama namba moja wa chama kidogo cha upinzani nchini Tanzania, ACT-Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad amemtupia lawama Rais John Pombe Magufuli wa nchi hiyo kwamba hatendi haki kwa vyama vya siasa vya upinzani. Maalim Seif ameyasema hayo leo akielezea hatua ya jeshi la polisi kuzuia mkutano wa chama hicho eneo la Temeke ambapo kilikuwa kimepanga kuwapatia kadi wanachama wapya 12, 600 na kulazimika kusitisha zoezi hilo.
-
Zitto Kabwe ajibu barua ya tishio la kufutwa chama chake cha ACT-Wazalendo Tanzania
Mar 26, 2019 10:34Kiongozi wa chama cha upinzani ACT-Wazalendo, nchini Tanzania Zitto Kabwe ametoa majibu matatu kufuatia chama hicho kuandikiwa barua na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini humo kwamba huwenda kitafutiwa usajili wake.
-
Chama tawala nchini Tanzania: Wanachama wa CCM waheshimuni wapinzani
Mar 23, 2019 09:52Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), nchini Tanzania Dk Bashiru Ally amewataka wanachama wa chama hicho tawala nchini humo, kutowabeza wapinzani na badala yake kuheshimu alama za vyama vyote vya siasa kwa sababu vimesajiliwa kisheria.
-
SAUTI, Ripoti ya matukio ya Kiislamu, Benki za Kiislamu TZ, dua ya kuomba mvua na mitandao ya kijamii
Mar 22, 2019 12:26Utekelezwaji wa sheria na kanuni kwa benki za Kiislamu wahimizwa kwa ajili ya kuzifanya benki hizo ziweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Hii ni kwa kuwa benki za Kiislamu zinaonekana kuwa kivutio kwa wateja wengi kutokana na uwajibikaji wake unaoenda sawa na mafundisho ya Kiislamu.
-
Chadema Tanzania: Tulitamani kumchukua Maalim Seif, lakini hatukufikia mwafaka
Mar 20, 2019 13:17Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini Tanzania Chadema ambacho ni chama kikuu cha upinzani nchini humo, kimesema kuwa, kilitamani kumchukua aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, lakini hakikufikia makubaliano na mwanasiasa huyo.
-
Siasa za upinzani TZ zazidi kunoga; Maalim Seif akabidhiwa kadi namba moja ya uwanachama ACT-Wazalendo
Mar 19, 2019 13:03Siasa za upinzani TZ zazidi kunoga, baada ya Maalim Seif kukabidhiwa kadi namba moja ya uwanachama ACT Wazalendo