-
Mahakama EACJ yaitaka Tanzania kuondoa vifungu kandamizi katika Sheria Ya Vyombo Vya Habari
Mar 28, 2019 10:43Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ) imekipa ushindi Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Baraza la Habari Tanzania (MCT) pamoja na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kesi Namba 2 ya mwaka 2017 ya kupinga vifungu kandamizi katika Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari, 2016.
-
Maalim Seif: Ndugu yangu Magufuli jiulize je, unatenda haki? Kumbuka utaenda kujibu kwa Mungu
Mar 27, 2019 11:52Mwanachama namba moja wa chama kidogo cha upinzani nchini Tanzania, ACT-Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad amemtupia lawama Rais John Pombe Magufuli wa nchi hiyo kwamba hatendi haki kwa vyama vya siasa vya upinzani. Maalim Seif ameyasema hayo leo akielezea hatua ya jeshi la polisi kuzuia mkutano wa chama hicho eneo la Temeke ambapo kilikuwa kimepanga kuwapatia kadi wanachama wapya 12, 600 na kulazimika kusitisha zoezi hilo.
-
Zitto Kabwe ajibu barua ya tishio la kufutwa chama chake cha ACT-Wazalendo Tanzania
Mar 26, 2019 10:34Kiongozi wa chama cha upinzani ACT-Wazalendo, nchini Tanzania Zitto Kabwe ametoa majibu matatu kufuatia chama hicho kuandikiwa barua na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini humo kwamba huwenda kitafutiwa usajili wake.
-
Chama tawala nchini Tanzania: Wanachama wa CCM waheshimuni wapinzani
Mar 23, 2019 09:52Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), nchini Tanzania Dk Bashiru Ally amewataka wanachama wa chama hicho tawala nchini humo, kutowabeza wapinzani na badala yake kuheshimu alama za vyama vyote vya siasa kwa sababu vimesajiliwa kisheria.
-
SAUTI, Ripoti ya matukio ya Kiislamu, Benki za Kiislamu TZ, dua ya kuomba mvua na mitandao ya kijamii
Mar 22, 2019 12:26Utekelezwaji wa sheria na kanuni kwa benki za Kiislamu wahimizwa kwa ajili ya kuzifanya benki hizo ziweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Hii ni kwa kuwa benki za Kiislamu zinaonekana kuwa kivutio kwa wateja wengi kutokana na uwajibikaji wake unaoenda sawa na mafundisho ya Kiislamu.
-
Chadema Tanzania: Tulitamani kumchukua Maalim Seif, lakini hatukufikia mwafaka
Mar 20, 2019 13:17Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini Tanzania Chadema ambacho ni chama kikuu cha upinzani nchini humo, kimesema kuwa, kilitamani kumchukua aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, lakini hakikufikia makubaliano na mwanasiasa huyo.
-
Siasa za upinzani TZ zazidi kunoga; Maalim Seif akabidhiwa kadi namba moja ya uwanachama ACT-Wazalendo
Mar 19, 2019 13:03Siasa za upinzani TZ zazidi kunoga, baada ya Maalim Seif kukabidhiwa kadi namba moja ya uwanachama ACT Wazalendo
-
Tanzania yasema imeimarisha usimamizi wa matumizi salama ya nyuklia
Mar 12, 2019 04:31Serikali ya Tanzania kupitia Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) imefanikiwa kuimarisha usimamizi na udhibiti wa matumizi ya teknolojia ya nyuklia nchini humo.
-
Tanzania ingali inashuhudia mfumko wa bei za bidhaa+SAUTI
Mar 10, 2019 13:06Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii Tanzania, Ephraim Kwesigabo amesema kuwa mfumuko wa bei nchini humo kwa mwaka ulioishia mwezi Februari 2019 umebaki kuwa asilimia 3 kama ilivyokuwa mwaka ulioisha.
-
Tanzania yatakiwa kuangalia upya sheria zinazokandamiza wanawake
Mar 08, 2019 04:28Huku Tanzania ikijiunga na nchi nyingine duniani katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake inayoadhimishwa hii leo, serikali ya Dar es Salaam imetakiwa kuangalia upya sera na sheria zinazohusu wanawake ili kuimarisha ustawi wao.