-
Mwenyekiti wa Chadema alipoachiliwa huru kwa dhamana Tanzania + Sauti
Mar 07, 2019 15:28Nchini Tanzania Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Kikuu cha Upinzani nchini humo cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe, pamoja na Mbunge Esta Matiko wameachiwa kwa dhamana baada ya kushinda rufaa ya dhamana katika Mahakama Kuu ya Tanzania Dar es salaam, na kutakiwa kuripoti mahakamani kwa mwezi mara moja. Kwa taarifa zaidi na tumtegee sikio mwandishi wetu wa Dar es Salaam Amar Dachi
-
Rais Magufuli aliambia Jeshi la Polisi kuwa, kuna maswali mengi kuhusu sakata la kutekwa Mohammed Dewji
Mar 04, 2019 11:22Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania, amesema kuwa, suala la kutekwa nyara kwa mfanyabiashara mashuhuri wa nchi hiyo na Afrika, Mohammed Dewji mashuhuri kwa jina ‘Mo’ limeacha maswali mengi kwa wananchi ambayo yanahitaji majibu hivyo jeshi la polisi liwaeleze Watanzania kwani si wajinga sana.
-
Lowassa atangaza kurejea CCM, Tanzania, Sumaye asema hakushangaa
Mar 01, 2019 12:50Waziri Mkuu wa zamani nchini Tanzania ambaye alikuwa mgombea urais kupitia tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Edward Ngoyai Lowassa leo ametangaza uamuzi wa kuhama chama hicho na kurejea chama tawala (CCM).
-
SAUTI, Sheikh Hemed Jalala: Uislamu ndio umemuinua na kumtukuza mwanamke na kamwe haujamuacha nyuma hata kidogo
Feb 27, 2019 12:52Kiongozi wa Chuo cha Imam Swadiq (as) cha jijini Dar es Salaam, Tanzania Sheikh Hemed Jalala amesema kuwa dini ya Kiislamu haijamtenga wala kumuacha nyuma kwa namna yoyote mwanamke na kwamba ni dini hiyo ndio imempa hadhi kiumbe huyo baada ya kuwa alikuwa duni katika jamii.
-
Taasisi ya al Mustafa Khairiya yaozesha vijana 100 Tanga, Tanzania + Sauti
Feb 26, 2019 03:09Taasisi ya al Mustafa Khairiya ya jijini Tanga Tanzania imefanya hafla ya kuwaozesha vijana 100 wa Kiislamu katika jitihada za kupunguza maovu kwenye jamii. Ammar Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam...
-
Jenerali Ulimwengu: Rais Magufuli ana uthubutu, lakini asikilize anayoambiwa na watu
Feb 21, 2019 04:33Jenerali Ulimwengu, mwandishi mkongwe wa habari na mkosoaji mashuhuri wa serikali nchini Tanzania sambamba na kumuunga mkono Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania, amemtaka rais huyo kusikiliza yale anayoambiwa na wananchi.
-
Chadema: Inamaana Tanzania haitachunguza matukio ya Azori na Ben Saanane hadi warudi?
Feb 15, 2019 11:15Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini Tanzania (CHADEMA) kimeendelea kukosoa takwa la Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo , Kangi Lugola la kutaka Tundu Lissu, mbunge wa Singida Mashariki kupitia tiketi ya chama hicho pamoja na dereva wake walioko nje ya nchi kimatibabu, kurejea nyumbani ili waweze kuhojiwa kuhusiana na shambulizi lililomlenga Lissu hapo tarehe 7 Septemba 2017.
-
Wasomi Tanzania: Iundwe tume huru ili kuepusha utata wa tuhuma kati ya Tundu Lissu na serikali
Feb 14, 2019 12:12Wasomi na wanasheria nchini Tanzania wametoa mwito wa kuundwa tume huru isiyo na mahusiano na serikali ya nchi hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa shambulio lililompata Tundu Lissu, Mbunge wa upinzani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hapo Septemba 7 mwaka 2017 na kumaliza utata uliopo kuhusiana na sakata hilo.
-
Sheikh Ponda: Inasikitisha mno Chuo Kikuu cha Dodoma, Tanzania kusitisha ujenzi wa msikiti
Feb 10, 2019 13:41Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda amesema kuwa, jumuiya hiyo imesikitishwa mno na hatua ya uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kusitisha ujenzi wa msikiti uliokuwa ujengwe chuoni hapo.
-
Balozi Farhang: Miradi ya nyuklia ya Iran ni ya amani kikamilifu + Sauti
Feb 07, 2019 14:26Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania, Bw. Mousah Farhang amesema kuwa miradi ya nyuklia ya Iran ni ya amani kikamilifu, kinyume kabisa na propaganda zinazoenezwa na madola ya kibeberu. Ammari Dachi na taarifa kamili kutoka Dar es Salaam...