-
Kesi ya kupinga uteuzi wa Mwanasheria Mkuu Tanzania yaanza kusikilizwa
Feb 07, 2019 11:17Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam nchini Tanzania imeanza kusikiliza kesi ya kupinga uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Dk Adelardus Kilangi uliofanywa na Rais John Magufuli tarehe Mosi Februari mwaka jana 2018.
-
Mgogoro wa Burundi umeshindikana? Mkapa alia na EAC kumtelekeza
Feb 07, 2019 11:13Wachunguzi wa mambo wanasema kuwa kuna kila dalili za kuonesha kuwa mgogoro wa Burundi umeshindikana kutatuliwa.
-
Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania azindua mahakama inayotembea
Feb 06, 2019 09:12Rais John Magufuli wa Tanzania amezindua gari maalumu la mahakama inayotembea litakalosaidia kusikiliza kesi katika mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam.
-
Taharuki yaibuka mkoani Njombe, Tanzania kutokana na vitendo vya utekaji nyara na mauaji dhidi ya watoto wadogo
Feb 04, 2019 10:46Hali ya taharuki imeendelea kushuhudiwa mkoani Njombe, Tanzania kutokana na vitendo vya utekaji nyara na mauaji dhidi ya watoto wadogo. Vitendo hivyo vimeendelea kushuhudiwa huku serikali ya Tanzania sambamba na kufanya juhudi kubwa zenye lengo la kuzuia jinai hizo, ikitakiwa pia kutoa kauli rasmi itakayoleta utulivu katika eneo hilo.
-
Wazazi Njombe Tanzania walazimika kuacha kazi na kusindikiza watoto shuleni wasiuawe + Sauti
Feb 03, 2019 14:33Wazazi mkoani Njombe nchini Tanzania wameongeza uangalifu kwa watoto wao na wengine wanaacha shughuli zao ili kusindikiza watoto wao shuleni. Hii ni kutokana na wimbi la mauaji ya watoto hao mkoani humo. Amari Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam...
-
Mkutano wa wakuu wa EAC hatimaye wafanyika Arusha, Tanzania
Feb 01, 2019 10:24Marais wanne kati ya sita wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, wamewasili Arusha Tanzania, kushiriki mkutano wa wakuu wa jumuiya hiyo ya kikanda ambao mwaka jana ulifutwa mara mbili ndani ya muda wa wiki tatu.
-
Tanzania kuchunguza uchinjaji wa watoto 10 Njombe
Jan 29, 2019 10:25Serikali ya Tanzania imesema itachunguza tukio la kusikitisha la watoto 10 kupoteza maisha baada ya kuchinjwa katika eneo la Njombe.
-
Viongozi wa dini Tanzania: Kubeti ni kamari, ni haramu! + Sauti
Jan 27, 2019 14:50Viongozi wa kidini na wa kiserikali nchini Tanzania wamekemea vitendo vya kubeti na kucheza kamari ambavyo vimekithiri nchini humo hali ambayo inapelekea kuzalika vijana wasiofanya kazi wakiweka matumaini zaidi ya kupata kipato chao kupitia njia hizo. Ammar Dachi na maelezo zaidi kutoka Dar es Salaam Tanzania.
-
Burundi: Kuna njama za kuvuruga uhusiano wetu na Tanzania + Sauti
Jan 21, 2019 14:51Mashirika ya Capes na Pisc ya nchini Burundi yamesema kuwa, kugunduliwa sare za jeshi la Tanzania katika kambi ya wakimbizi huko Burundi kunadhihirisha kuwepo njama za kutaka kuvuruga uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizo mbili. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura.
-
CAG Tanzania ahojiwa na kamati ya bunge, huku Mahakama Kuu ikipokea kesi ya kupinga kuhojiwa kwake
Jan 21, 2019 13:03Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imemuhoji Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kuhusu kauli yake ya “udhaifu wa Bunge la nchi hiyo.”