-
Mbunge wa chama cha Leba ataka sheria ya kuwaadhibu wanaomvunjia heshima Mtume (saw)
Jul 11, 2021 00:12Mbunge wa Uingereza ametetea heshima ya Mtume Muhammad (saw) katika hotuba ya kupendeza kwenye Bunge la nchi hiyo, akiangazia mashinikizo ya kiroho na madhara yaliyosababishwa kwa Waislamu ulimwenguni kote kutokana na katuni na picha zinazochapishwa mara kwa mara barani Ulaya zikimvunjia heshima Nabii huyo wa Mwenyezi Mungu.
-
Waziri wa zamani wa mambo ya ndani wa Uingereza aitaka Conservative itupilie mbali Islamophobia
May 26, 2021 21:50Waziri wa zamani wa mambo ya ndani wa Uingereza amekishauri chama tawala cha Conservative kujipanga upya kwa kutupilia mbali sera za kupiga vita Uislamu (Islamophobia).
-
Marekani yasimamisha chanjo ya corona ya Johnson & Johnson kwa hofu ya kuganda damu
Apr 13, 2021 22:05Marekani imesitisha matumizi ya chanjo ya virusi vya corona iliyotengenezwa na kampuni ya dawa ya nchi hiyo, Johnson and Johnson, ambayo kuna madai kuwa inasababisha kuziba kwa mishipa kama matokeo ya tatizo la kuganda kwa damu kwa watu waliopewa chanjo hiyo.
-
7 waaga dunia UK kwa kuganda damu baada ya kupigwa chanjo ya AstraZeneca
Apr 03, 2021 07:27Wakala wa Kudhibiti Madawa Uingereza (MHRA) umesema miongoni mwa watu 30 waliopaata matatizo ya kuganda damu baada ya kupigwa chanjo ya AstraZeneca, saba wameaga dunia.
-
Bri. Jen. Hatami: Uingereza ichukue hatua za kivitendo kulipa deni la Iran
Mar 23, 2021 22:39Waziri wa Ulinzi wa Iran ameashiria jinsi Uingereza ilivyokiri kuwa ina deni la miaka 42 la Iran na kuitaka London ichukue hatua za kivitendo za kuilipa Tehran fedha zake hizo ambazo ni mamia ya mamilioni ya dola.
-
Iran yakosoa undumakuwili wa Uingereza, yataka silaha zote za nyuklia ziharibiwe
Mar 17, 2021 03:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali undumakuwili wa Uingereza; ambayo kwa upande mmoja inatoa madai yasiyo na msingi dhidi ya miradi ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani na kwa upande mwingine, inasema kuwa inataka kuongeza akiba ya silaha zake za nyuklia.
-
Oxfam yaitaka UK iache kuiuzia Saudia silaha baada ya ripoti ya mauaji ya Khashoggi
Feb 28, 2021 22:50Shirika la misaada ya kibinadamu la Oxfam limeitaka Uingereza isimamishe mauzo ya silaha zake kwa Saudi Arabia, baada ya ripoti ya kiintelijensia ya Marekani kusema Mohammad Bin Salman, mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia ndiye aliyetoa amri ya kuuawa Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari aliyekuwa akiukosoa utawala wa Aal-Saud.
-
UK: Aina mpya ya virusi vya corona imetokea Afrika Kusini
Dec 24, 2020 04:43Waziri wa Afya wa Uingereza amesema spishi mpya ya kirusi cha corona iliyogunduliwa nchini humo na inayoambukiza na kuenea kwa kasi kubwa zaidi iliibukia nchini Afrika Kusini.
-
Iran na nchi kadhaa duniani zasimamisha safari za ndege za Uingereza
Dec 21, 2020 04:49Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na nchi nyingine kadhaa duniani zimesimamisha kwa muda safari za ndege za kwenda na kutoka Uingereza baada ya kuripotiwa aina mpya ya msambao wa virusi vya corona mjini London na kusini mashariki mwa UK.
-
COVID-19 Ulaya: Sheria za udhibiti zaibua ghasia Uhispania, Uingereza yafungwa
Nov 01, 2020 08:04Bara Ulaya sasa linakabiliana na wimbi la pili la maambukizi ya COVID-19 au corona huku hali ikitabiriwa kuendelea kuwa mbaya katika wiki kadhaa zijazo.