-
Kuanza Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi huko Glasgow; shaka na mazingatio katika mkutano huo
Nov 03, 2021 07:48Mkutano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa (COP26) ulianza shughuli zake juzi Jumatatu katika mji wa Glasgow nchini Scotland kwa kuhudhuriwa na wakuu wa nchi zaidi ya 100 na viongozi wengine wa ngazi za juu wa nchi mbalimbali duniani.
-
Jihad Islami yalaani kitendo cha mwakilishi wa Israel cha kuchana ripoti ya Baraza la Haki za Binadamu la UN
Oct 31, 2021 04:02Harakati ya Jihad Islami ya Palestina imewangaza kuwa hatua ya mwakilishi wa utawala wa Kizayuni wa Israel ya kurarua ripoti ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ni kielelezo cha kilele cha kiburi cha kisiasa cha utawala huo na jinsi unavyozidharau taasisi za kimataifa.
-
Ravanchi:Baraza la Usalama liilazimishe Israel ihitimishe kuikalia kwa mabavu Golan
Oct 28, 2021 11:15Balozi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa Baraza la Usalama la umoja huo linalazimiika kutekeleze wajibu wake na kuulazimisha utawala wa Kizayuni wa Israel uache kuikalia kwa mabavu miinuko ya Golan na uvamizi dhidi ya Syria.
-
UN: Ulimwengu uko hatarini kuwa na ongezeko la joto lisilopungua nyuzijoto 2.7 katika karne hii
Oct 27, 2021 00:36Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira UNEP limesema, ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwengu kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto 2.7 katika karne hii.
-
Iran ina azma ya kuwawezesha wanawake na wasichana
Oct 22, 2021 03:45Balozi na Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina azma ya kufanya kilicho dharura ili kuwawezesha wanawake na wasichana."
-
UN yaunga mkono usitishaji vita kati ya Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na waasi
Oct 17, 2021 04:25Antonio Guterres Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa jana alitangaza kuwa anakaribisha usitishaji vita uliofikiwa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati na Rais wa nchi hiyo Faustin-Archange Touadera na makundi ya waasi.
-
Taliban wataalikwa katika mazungumzo ya kimataifa ya Moscow kuhusu Afghanistan
Oct 08, 2021 04:31Russia imesema, italialika kundi la Taliban katika mazungumzo ya kimataifa kuhusu Afghanistan yaliyopangwa kufanyika tarehe 20 ya mwezi huu wa Oktoba mjini Moscow.
-
UN yazindua mkakati wa kufikisha chanjo ya Covid-19 kwa 70% ya watu wote duniani ifikapo 2022
Oct 08, 2021 04:00Shirika la Afya Duniani WHO limezindua mkakati wa kufikisha chanjo ya COVID-19 kwa asilimia 70 ya watu wote duniani ifikapo katikati ya mwaka ujao wa 2022, lengo likiwa ni kumaliza kile kilichoitwa mwenendo usio sahihi wa utoaji chanjo hizo katika mataifa maskini na yale tajiri na hivyo kuhakikisha kila mtu amekingwa dhidi ya ugonjwa huo.
-
UN: Mazungumzo baina ya Iran na Saudi Arabia ni "muhimu sana"
Oct 08, 2021 03:59Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema, mazungumzo kati ya Iran na Saudi Arabia ni "muhimu sana".
-
Serikali ya Ethiopia yatoa amri ya kutimuliwa maafisa 7 wa UN kwa "kuingilia" masuala ya ndani ya nchi hiyo
Sep 30, 2021 22:57Serikali ya Ethiopia imeamuru maafisa saba waandamizi wa Umoja wa Mataifa waondolewe nchini humo kwa kile ilichokiita kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.