-
UN: Raia 114 wameuawa Lebanon katika ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa na Israel
Nov 13, 2025 23:07Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa Israel uliotokana na makubaliano yaliyofikiwa kati ya utawala huo wa kizayuni na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon ya Hizbullah mnamo Novemba 2024 umesababisha vifo vya raia 114 wa nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa watahadharisha kuhusu hatari ya njaa katika nchi 16
Nov 13, 2025 22:55Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) zimeonya kuhusu mgogoro mkubwa wa ukosefu wa usalama wa chakula unaozidi kuwa mbaya katika nchi 16, na kuweka hatarini maisha ya mamilioni ya watu, hasa katika maeneo yenye migogoro na majanga ya hali ya hewa.
-
UN: Mashambulizi ya walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukingo wa Magharibi yamefikia kiwango cha juu zaidi
Nov 08, 2025 04:27Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba walowezi wa Israel wamefanya mashambulizi yasiyopungua 264 dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu mwezi uliopita wa Oktoba, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya kila mwezi tangu maafisa wa Umoja wa Mataifa walipoanza kufuatilia mashambulizi kama hayo mwaka 2006.
-
UN: Israel imekataa maombi zaidi ya 100 ya kuingiza misaada Ghaza tangu vita viliposimamishwa
Nov 07, 2025 06:47Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, tangu yalipoanza kutekelezwa makubaliano ya kusitisha vita tarehe 10 Oktoba, utawala wa kizayuni wa Israel umekataa maombi 107 ya kuingizwa vifaa vya misaada katika Ukanda wa Ghaza, na hivyo kuzuia vifaa muhimu vya kibinadamu kuwafikia Wapalestina wa eneo hilo wanaoishi katika mazingira magumu na ya mateso.
-
UNSC yapitisha azimio la US la kuunga mkono mpango wa Morocco kuhusu Sahara Magharibi
Nov 02, 2025 02:53Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepiga kura ya kurefusha kwa mwaka mmoja muda wa kazi za ujumbe wake ulioko Sahara Magharibi (MINURSO), sambamba na kuidhinisha rasmi mpango wa serikali ya Morocco wa kutoa mamlaka ya ndani kwa eneo hilo kama msingi pekee wa kutatua mgogoro huo wa miongo kadhaa, hatua ambayo imesababisha mpasuko mkubwa katika jamii ya kimataifa.
-
Araghchi na Guterres wajadili migogoro ya Gaza, Yemen
Oct 21, 2025 08:12Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres wamefanya mazungumzo ya simu na kuzungumzia matukio ya kikanda ikiwemo hali ya Gaza na Yemen.
-
UN: Makubaliano ya amani ya Kongo na Rwanda 'hayaheshimiwi'
Oct 14, 2025 09:17Umoja wa Mataifa umesema kuwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda "hayaheshimiwi."
-
Umoja wa Mataifa wakaribisha taarifa ya Hamas kuhusu usitishaji vita Gaza
Oct 04, 2025 04:01Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha kwa mikono miwili taarifa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas inayoonyesha utayarifu wake wa kuwaachilia mateka na kukubali kwa masharti mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Je, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limenasa katika mtego wa kura ya turufu?
Sep 30, 2025 23:02Haki ya kura ya turufu ni mojawapo ya masuala yenye utata kuhusu mamlaka ya wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Iran yalaani urejeshaji vikwazo vya UN vilivyokwisha muda wake uliofanywa na Marekani na Ulaya
Sep 30, 2025 04:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi ameikosoa Marekani na mataifa matatu ya Ulaya kwa kujaribu kutumia utaratibu wa 'snapback' wa makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 ili kurejesha tena vikwazo vilivyokwisha muda wake vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.