-
Hizbullah yautahadharisha utawala wa Kizayuni wa Israel, yasema makombora yake yako ange
Jun 21, 2020 23:30Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imeutahadharisha utawala wa kizayuni kwamba iwapo utashambulia ardhi ya Lebanon itashambulia maeneo mbalimbali ya utawala huo kwa kutumia makombora yanayolenga shabaha kwa umakini mkubwa.
-
Wanaharakati wa masuala ya kiraia watoa wito wa kususiwa Israel kimataifa
Jun 20, 2020 22:44Jumuiya ya Kimataifa ya Mshikamano wa Kusini nchini Afrika Kusini imetoa wito wa kususiwa utawala haramu wa Israel katika nyanja za kimataifa.
-
Hamas yalaani hatua ya Wazayuni ya kubomoa vituo vya Wapalestina
Jun 17, 2020 22:22Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa kitendo cha utawala wa Kizayuni wa Israel cha kubomoa vituo vya Wapalestina huko Quds inayokaliwa kwa mabavu ni jitihada za utawala huo zinazolenga kubadili utambulisho wa Quds; njama ambazo hazitafikia popote.
-
Algeria: Kutwaliwa eneo la Ukingo wa Magharibi ni mpango batili na wa kiadui
Jun 14, 2020 01:58Serikali ya Algeria imetangaza kuwa, mpango wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kulitwaa eneo la Palestina la Ukingo wa Magharibini batili na wa kiuhasama si kwa taifa la Palestina pekee bali kwa nchi zote za Waislamu.
-
Shamkhani: Kuvunjwa 'masanamu ya kibaguzi' kumewatia kiwewe Wazayuni
Jun 13, 2020 08:06Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kitendo cha kuvunjwa nembo na masanamu yanayoashiria ubaguzi wa rangi katika nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani kimeutia kiwewe na wahka mkubwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
OIC yatahadharisha matokeo mabaya ya mpango wa kughusubu eneo la Ukingo wa Magharibi
Jun 11, 2020 07:35Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imetahadharisha juu ya matokeo mabaya ya uamuzi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kutaka kuzipora na kuzikalia kwa mabavu ardhi zaidi za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kulaani vikali hatua hiyo.
-
Barua ya Ismail Hania kwa viongozi 40 wa nchi za Kiarabu kwa ajili ya kusambaratisha mpango wa Israel
Jun 10, 2020 03:26Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) amewatumia barua tofauti wakuu na viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu zaidi ya 40 akiwataka kuchukua hatua za harakati kusitisha mpango wa Israel wa kutaka kuyaunganisha baadhi ya maeneo ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na ardhi zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Wazayuni wauhujumu Msikiti wa Al Aqsa
Jun 10, 2020 00:24Makumi ya walowezi wa Kizayuni, wakiwa wanapata himaya ya wanajeshi wa utawala wa Israel wameuhujumu Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem).
-
Kubaidishwa khatibu wa Msikiti wa al Aqsa; jinai mpya ya Wazayuni
Jun 06, 2020 07:01Polisi ya utawala wa Kizayuni imetoa amri ya kubaidishwa kwa miezi minne Sheikh Ikrima Sabri Khatibu wa Msikiti wa al Aqsa.
-
Serikali ya Palestina: Mpango wa kutwaa Ukingo wa Magharibi utazusha machafuko yasiyo na kifani
Jun 04, 2020 08:15Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina imetangaza kuwa, mpango wa utawala haramu wa Israel wa kuyatwaa maeneo zaidi ya Ukingo wa Magharbi wa Mto Jordan utazusha machafuko ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika eneo la Mashariki ya Kati.