-
Yemen yatoa taarifa kuhusu mashambulizi iliyofanya dhidi ya ngome za utawala wa Kizayuni
Nov 18, 2024 07:15Jeshi la Yemen limetoa taarifa kuhusu mashambulizi liliyofanya dhidi ya baadhi ya maeneo nyeti na muhimu sana ya kijeshi ya adui Mzayuni katika maeneo ya Jaffa na Ashkelon huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu iliyopachikwa jina bandia la Israel.
-
Mamilioni ya Wasenegal wameelekea vituo vya kupigia kura kuchagua Bunge jipya
Nov 17, 2024 12:13Wasenegal leo wamepiga kura katika uchaguzi wa Bunge ambao utaamua kama rais mpya wa nchi hiyo Bassirou Diomaye Faye ataweza kufanya mageuzi makubwa aliyokusudia au la.
-
Hizbullah yashambulia maeneo ya kistratijia ya utawala wa Kizayuni wa Israel
Nov 17, 2024 02:27Kituo cha Taarifa za Vita cha Hizbullah ya Lebanon kimetangaza kuwa wapiganaji wa harakati hiyo wamefanya mashambulizi ya makombora katika maeneo kadhaa ya kistratijia ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Qatar yaonya kuhusu kupigwa marufuku UNRWA
Nov 16, 2024 13:25Serikali ya Qatar imeonya kuhusiana na hatua ya kupigwa marukufu shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) na kusisitiza udharura wa kuheshimiwa haki za Wapalestina.
-
HAMAS yaendelea kuangamiza wanajeshi wa Israel kaskazini mwa Ghaza
Nov 16, 2024 07:28Brigedi za Izzuddin Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS zimetangaza kuwa zimeangamiza maafisa wengine watatu wa jeshi la utawala wa Kizayuni na zana zao za kijeshi kaskazini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Hizbulla yaendelea kutoa vipigo dhidi ya Wazayuni
Nov 16, 2024 07:25Kitengo cha habari za kivita cha Hizbullah ya Lebanon kimetangaza kuwa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu imeendelea kutoa vipigo na kuyatwanga kwa makombora na droni maeneo mbalimbali ya kijeshi ya Israel.
-
Kiongozi mmoja wa HAMAS auawa katika jela za Israel
Nov 16, 2024 02:55Mmmoja wa viongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS, Samih Aliwi, aliuawa shahidi jana Ijumaa, Novemba 15, 2024 ikiwa ni siku sita baada ya kuhamishwa kutoka gereza la Ramla na kupelekwa katika hospitali ya Assaf Harofeh. Taarifa nyingine zinasema aliuawa shahidi tangu siku sita nyuma lakini utawala wa Kizayuni ulikuwa unaficha kifo chake.
-
Juhudi za Marekani za kuhalalisha jinai za Israel na kuendelea kuitumia silaha za mauaji ya umati
Nov 16, 2024 02:50Vedant Patel, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ametoa matamshi ambayo yanaonyesha kuwa Marekani haiko tayari kwa vyo vyote vile kumuwajibisha mshirika wake wa jinai za kivita, yaani utawala haramu wa Israel, na kuwa inatosheka tu kwa kutoa madai matupu yasiyo na maana kuhusiana na suala zima la haki za binadamu.
-
HAMAS: Andamaneni na zidini kuzizingira balozi za utawala wa Kizayuni na wanaouunga mkono
Nov 14, 2024 07:14Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa wito wa kuzidishwa harakati za umma katika ngazi ya kimataifa katika kulaani mwendelezo wa jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza na kuliunga mkono taifa la Muqawama la Palestina.
-
Maporomoko ya udongo yaua watu 16 magharibi ya Madagascar
Nov 14, 2024 07:05Watu wapatao 16 wamefariki dunia wakati mashua waliyokuwa wakisafiria kupitia mtoni magharibi mwa Madagascar kukumbwa na maporomoko ya udongo. Hayo yameelezwa na mamlaka husika za nchi hiyo jana Jumatano.