-
Mufti wa Oman akosoa vikali kimya kinachoonyeshwa mbele ya jinai za Israel dhidi ya Ghaza
Apr 05, 2025 07:20Mufti Mkuu wa Oman, Sheikh Ahmed al-Khalili, amekosoa vikali kimya kinachoonyeshwa mbele ya jinai za kinyama zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.
-
UN: Israel imegeuza theluthi mbili za ardhi ya Ghaza kuwa eneo lisiloruhusiwa kufika
Apr 05, 2025 02:36Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imetangaza kuwa, hivi sasa utawala wa Kizayuni wa Israel umewawekea vizuizi Wapalestina vya kutoruhusiwa kufika kwenye takriban theluthi mbili ya eneo la Ukanda wa Ghaza, ama kwa kuyatangaza maeneo makubwa kadhaa ya ukanda huo kuwa ni marufuku kufika au kutoa amri ya kuwalazimisha wananchi hao kuyahama makazi yao.
-
Iran: Tutatumia njia zote kuuwajibisha utawala wa Kizayuni kwa kuushambulia ubalozi wetu
Apr 02, 2025 11:59Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kwa mnasaba wa kumbukumbu ya jinai iliyofanywa na utawala wa Kizayuni ya kuushambulia ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu mjini Damascus na kutangaza kuwa: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeazimia kutumia fursa na njia zote kutekeleza uadilifu na kuuwajibisha utawala wa kigaidi wa Israel.
-
Iran yaalani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon
Apr 02, 2025 07:14Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo la Dhahiya katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.
-
Wapalestina 11 wauawa shahidi katika mashambulizi ya leo ya jeshi la Israel
Apr 02, 2025 06:58Duru za kitiba zimetangaza kuwa Wapalestina 11 wameuawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza mapema leo.
-
Utawala wa Kizayuni waendelea kupinga utoaji wa misaada kwa Wapalestina
Mar 31, 2025 10:13Vitendo vya kikatili vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wanaoishi Gaza vinaendelea, na bado utawala huo unazuia kufikishwa kwa misaada ya chakula na dawa kwa wakazi wa Gaza.
-
Jinai za kinyama za Israel za kuwaua Wapalestina hata katika Siku ya Idi zalaaniwa vikali
Mar 31, 2025 07:41Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeendelea kuwaua watu wa Ghaza hata katika wakati huu wa Sikukuu ya Idul-Fitri na kutoonyesha heshima yoyote kwa Sikukuu hiyo.
-
Rais wa Iran: Mwelekeo wa mazungumzo unategemea mwenendo wa Wamarekani
Mar 31, 2025 02:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Tehran haijawahi kukwepa mazungumzo, lakini ni aina ya mwenendo wa Wamarekani ndio unaoamua ikiwa mazungumzo yataendelea au la.
-
Kuongezeka hatua za Trump dhidi ya vyuo vikuu na wanafunzi wanaowatetea Wapalestina
Mar 30, 2025 07:05Katika muhula wake wa pili wa urais, Donald Trump, rais mpya wa Marekani kwa mara nyingine tena ameamua kutumia mtindo alioutumia katika muhula wake wa kwanza wa kuuunga mkono bila mpaka utawala wa Kizayuni wa Israel na kuchukua hatua mpya za kuisaidia na kuihami Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Radiamali ya Hamas kufuatia kuuliwa shahidi "Abdel-Latif al-Qanoua" katika hujuma ya Israel
Mar 28, 2025 02:29Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imeashiria katika taarifa yake kuhusu kuuawa shahidi Abdel-Latif al-Qanoua Msemaji wa harakati hiyo katika shambulio la utawala wa Kizayuni na kutangaza kuwa: "Kuwalenga kwa masambulizi viongozi wa harakati ya Hamas na wasemaji wake kamwe hakuwezi kuvunja irada yetu.