-
Iran na Uturiki zahimizwa kukabiliana na ugaidi na propaganda chafu dhidi ya Uislamu
Dec 05, 2018 04:39Mkuu wa Jumuiya ya Masuala ya Dini nchini Uturuki amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki ambazo ni nchi kubwa zaidi katika eneo la Mashariki ya Kati zinapaswa kuzidisha ushirikiano kwa ajili ya kupambana na ugaidi na njama zinazoeneza propaganda za kuchafua sura safi ya Uislamu.
-
Iran na Uturuki zahimiza kufanikishwa biashara ya dola bilioni 30 baina yao
Nov 30, 2018 01:03Maspika wa mabunge ya Iran na Uturuki wamesisitizia haja ya kufanikishwa biashara ya dola bilioni 30 baina ya nchi zao.
-
Sisitizo la Umoja wa Ulaya na Uturuki la kuendelea kushirikiana na Iran
Nov 24, 2018 08:18Hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump ya kuiondoa nchi hiyo katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kuiwekea tena Iran vikwazo imepingwa vikali na nchi nyingine wanachama wa makubaliano hayo ya JCPOA yaani kundi la 4+1.
-
Uturuki: Maelezo ya Mwanasheria Mkuu wa Saudia kuhusu mauaji ya Khashoggi, hayatoshi
Nov 16, 2018 01:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mevlüt Çavuşoğlu amekosoa maelezo ya Mwanasheria Mkuu wa Saudi Arabia kuhusiana na mauaji ya Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud mjini Istanbul na kuongeza kwamba maelezo hayo hayatoshi kabisa.
-
"Saudia ilitumia programu ya udukuzi ya Israel kumfuatilia Kashoggi"
Nov 08, 2018 11:49Edward Snowden, afisa wa zamani wa Shirika la Usalama wa Taifa la Marekani (NSA) amefichua nafasi ya utawala haramu wa Israel katika mauaji ya kikatili ya mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi yaliyofanywa na Riyadh nchini Uturuki mwezi uliopita.
-
Uturuki: Timu ya mauaji ya Khashoggi imefanya mauaji kama hayo huko nyuma
Nov 02, 2018 12:54Vyombo vya Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki vimefuichua kuwa, Ankara ina ushahidi unaothibitisha kuwa, timu ya mauaji ya Saudi Arabia iliyoshiriki katika mauaji ya kigaidi dhidi ya mwandishi na mkosoaji wa serikali ya kifalme ya nchi hiyo, Jamal Khashoggi mjini Istanbul yapata mwezi mmoja uliopita, iliwahi kufanya mauaji kadhaa kama hayo hapo kabla.
-
Erdogan aitaka Saudia imfichue aliyetoa agizo la kuua Jamal Khashoggi
Oct 26, 2018 11:37Kwa mara nyingine tena Rais Recep Tayyib Erdogan wa Uturuki ameitaka Saudi Arabia imfichue mtu ambaye alitoa amri ya kuuawa Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari na mkosoaji mkubwa wa utawala wa Aal-Saud.
-
Jamii ya kimataifa yazidisha mashinikizo dhidi ya Saudia kuhusu mauaji ya Khashoggi
Oct 26, 2018 01:19Jamii ya kimataifa imezidisha mashinikizo dhidi ya utawala wa kifalme wa Saudi Arabia ambao umekiri kwamba maafisa wake walimuua mwandishi na mkosoaji wa utawala huo, Jamal Khashoggi zaidi ya wiki mbili zilizopita mjini Istanbul, Uturuki.
-
Rouhani: Saudia haiwezi kufanya jinai kubwa kama ya kumuua Khashoggi bila ya uungaji mkono wa Marekani
Oct 24, 2018 13:32Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani mauaji ya mwandishi na mkosoaji wa utawala wa kifalme wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi na kusema kuwa, misimamo ya nchi mbalimbali duniani dhidi ya mauaji hayo ni mtihani mkubwa kwa nchi zinazodai kutetea haki za binadamu hususan Marekani na nchi za Ulaya.
-
Uturuki: Mikono ya Bin Salman imeroa damu ya Jamal Khashoggi
Oct 24, 2018 13:31Mshauri wa Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema kuwa mikono ya Mohammed bin Salman mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia ina damu ya mwandishi habari mkosoaji Jamal Khashoggi.