Jan 29, 2019 13:16
Rais Nicolas Maduro wa Venezuela jana alisisitiza katika gwaride la jeshi la nchi hiyo lililofanyika kwa ajili ya kumuunga mkono kwamba, hakuna mtu yoyote ambaye anamheshimu mtu dhaifu, mwoga na msaliti na akaongeza kuwa, serikali ya Caracas inaungwa mkono kikamilifu na jeshi na kwamba, vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo vimejiandaa kikamilifu kuilinda nchi.