Jan 28, 2019 02:43
Kwa sasa Venezuela ingali inakabiliwa na mzozo na mgogoro wa kisiasa. Katika hali ambayo Marekani na waitifaki wake wanaendelea kufanya kila mbinu na njama ili kuiondoa madarakani serikali ya mrengo wa kushoto ya Rais Nicolás Maduro na ambaye ndiye rais halali wa nchi hiyo, kiongozi huyo sambamba na kupinga kuainishiwa makataa na muhula maalumu pamoja na vitisho vya kigeni dhidi yake, amesisitiza juu ya kulinda katiba na kuitetea Venezuela.