-
Bunge la Juu ya Uingereza lataka kuondolewa vikwazo Iran
Apr 15, 2020 03:39Mwenyekiti wa Kamati ya Uhusiano wa Kimataifa na Ulinzi ya Bunge la Juu la Uingereza (House of Lords) amesema anaunga mkono miito inayotolewa na maafisa wa nchi za Ulaya na Marekani za kutaka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iondolewa vikwazo, katika kipindi hiki ambapo Iran inaendelea kukabiliana na maambukizi makubwa ya virusi vya Corona.
-
Baraza la Makanisa Duniani laitaka Marekani iiondolee Iran vikwazo
Apr 12, 2020 23:06Baraza la Makanisa Duniani na Jumuiya ya Kitaifa ya Makanisa ya Kristo zimeeleza wasiwasi wao juu ya athari mbaya za vikwazo vya Marekani dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais Rouhani: Kuzinduliwa INSTEX ni hatua chanya, lakini haitoshi
Apr 06, 2020 23:01Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepongeza kuzinduliwa mfumo maalumu wa mabadilishano ya fedha kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Umoja wa Ulaya (INSTEX) na kusisitiza kuwa hatua hiyo ni chanya, lakini haitoshi kukidhi maslahi yote ya Iran.
-
Madai ya uongo ya Trump kuwa eti Iran haijaomba kupunguziwa vikwazo
Apr 03, 2020 23:43Baada ya kujitoa bila ya sababu katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei 2018 serikali ya Donald Trump huko Marekani iliirejeshea Iran vikwazo vyote vilivyokuwa vimeondolewa baada ya kufikiwa makubaliano hayo, bali iiiwekea Tehran vikwazo vya kiwango cha juu kabisa kama anavyojitapa mara kwa mara Donald Trump.
-
Rouhani: Marekani imepoteza fursa ya kihistroria ya kusahihisha makosa yake
Apr 01, 2020 21:55Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani imepoteza fursa ya kipekee na ya kihistoria ya kusahihisha makosa yake kwa kukataa kulindolea taifa hili vikwazo haramu wakati huu ambapo Iran inakabiliana na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwana virusi vya corona.
-
Ripota Maalumu wa UN ataka kuondolewa vikwazo vya upande mmoja vya Marekani
Apr 01, 2020 03:37Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya "Haki ya Chakula" ametaka kuondolewa vikwazo vya upande mmoja vya Marekani.
-
Zarif: Marekani inafanya ugaidi wa kitiba na kiuchumi dhidi ya taifa la Iran
Mar 29, 2020 22:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezungumzia vita vya pande zote na visivyo na kifani vya Marekani dhidi ya taifa la Iran na kusisitiza udharura wa kukomeshwa vikwazo haramu vya serikali ya Washington.
-
Vikwazo vipya vya Marekani; sisitizo la Washington la kuendeleza sera ya mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran
Mar 28, 2020 01:47Licha ya matakwa na mashinikizo ya kimtaifa ya kuondolewa vikwazo vya upande mmoja vya Marekani dhidi ya Iran hasa kwa kuzingatia mlipuko wa virusi vya corona na kuweko ulazima wa kukabiliana navyo, lakini serikali ya Washington inasisitiza kuendeleza utendaji wake usio wa kiutu na kibinadamu.
-
Ombi la nchi 8 kwa Umoja wa Mataifa kuhusu kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran
Mar 27, 2020 05:25Kuendelea vikwazo vya kidhalimu na vilivyo dhidi ya ubinadamu vya Marekani dhidi ya Iran katika fremu ya mashinikizo ya juu kabisa ya utawala wa Trump katika kipindi hiki cha kuenea ugonjwa wa COVID-19 au corona nchini Iran sambamba na udharura wa kukabiliana na ugonjwa huo angamizi kumepelekea jamii ya kimataifa iwasilishe maombi ya kutaka vikwazo hivyo viondolewa mara moja.
-
Kuendelea vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran katika kivuli cha Corona
Mar 27, 2020 03:28Katika radiamali yake dhidi ya msimamo wa hivi karibuni wa Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani juu ya kuendelea mashinikizo ya juu zaidi ya Washington dhidi ya Tehran, Muhammad Jawad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtaja waziri huyo wa Marekani kuwa 'waziri wa chuki'.