-
Papa Leo XIV : Uvamizi wa kijeshi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran 'sio vita vya haki'
Jun 07, 2026 03:44Kiongozi wa kanisa katoliki Dunia, Papa Leo XIV amesema uchokozi wa kijeshi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa "vita vya haki", akisisitiza kwamba itikadi hiyo ya karne nyingi haiendani na uhalisia wa vita vya kisasa.
-
WFP: Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinasukuma mamilioni kukumbwa na njaa Afrika
Jun 06, 2026 03:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya kuwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinawasukuma mamilioni ya watu duniani kuingia katika hali ya njaa huku bara Afrika likionekana kuathirika zaidi.
-
Iran yapinga 'matakwa ya kupita kiasi' katika mazungumzo au kusitisha mapigano
Jun 04, 2026 03:08Mshauri wa Masuala ya Kijeshi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema kuwa Tehran haitairuhusu Marekani kuwasilisha matakwa ya kupita kiasi, iwe ni katika mazungumzo au wakati wa mchakato wa kusitisha mapigano.
-
Jeshi la Iran lashambulia vituo vya kijeshi vya Marekani baada ya ukiukaji karibu na Mlango wa Hormuz
Jun 03, 2026 03:01Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kwamba vikosi vyake vimetekeleza mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya meli ya adui, makao makuu ya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain, pamoja na kambi ya jeshi la anga ya Marekani katika eneo hilo, kufuatia vitendo viwili vya uchokozi wa Marekani vilivyolenga mali za Iran.
-
Bei ya mafuta duniani yapanda huku majeshi ya Israel yakisonga ndani zaidi kusini mwa Lebanon
Jun 02, 2026 02:56Bei ya mafuta duniani yapanda huku majeshi ya Israel yakisonga ndani zaidi kusini mwa Lebanon
-
Simulizi la Wall Street Journal kuhusu vita vya Marekani dhidi ya Iran: Ni ushindi wa kimaonyesho wa Trump au kushindwa halisi?
May 31, 2026 12:50Mhariri mkuu wa Wall Street Journal amesema: "Trump analazimika kudhihirisha kushindwa kwake mbele ya Iran kama ushindi ili kulinda sura na hadhi yake."
-
CNN: Trump amezitishia au kuzishambulia nchi 15 akiwa madarakani
May 29, 2026 03:05Ripoti ya televisheni ya CNN imeeleza kuwa Rais Donald Trump wa Marekani amezitishia, ameeleza wazi uwezekano wa kufanya mashambulizi au amezishambulia nchi 15 katika mihula yake miwili ya uongozi; yaani kwa mahesabu ya haraka amefanya hivyo kwa nchi moja kati ya kila nchi 13 duniani.
-
Mkuu wa ujasusi wa Trump ajiuzulu kwa mashinikizo ya White House kuhusu vita haramu dhidi ya Iran
May 23, 2026 03:01Mkurugenzi wa Ujasusi wa Kitaifa (DNI) wa Rais wa Marekani, Donald Trump, Tulsi Gabbard, amejiuzulu kutokana na shinikizo kubwa la Ikulu ya White House baada ya kupinga vikali vita haramu na vya uchokozi vya Marekani dhidi ya Iran.
-
MEE: Misri iliishinikiza Al-Azhar 'kuunga mkono UAE' katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
May 23, 2026 02:43Ripoti zinasema kwamba Ofisi ya Rais wa Misri iliishinikiza taasisi ya Al-Azhar, ambayo ni mamlaka ya juu zaidi ya Waislamu wa madhehebu ya Suni, kuunga mkono hadharani Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na mataifa mengine ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Iran yatahadharisha kuhusu Marekani kulitumia vibaya Baraza la Usalama la UN
May 20, 2026 11:06Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa: "Marekani inalitumia vibaya Baraza la Usalama kwa kueneza uwongo na tuhuma zisizo na msingi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mpango wake wa nyuklia."