-
Iran yaangamiza rada za jeshi la Marekani Magharibi mwa Asia, askari kadhaa wauawa
Jul 21, 2026 11:33Majeshi ya Iran yametekeleza operesheni za uharibifu mkubwa wa miundombinu kadhaa ya rada na mifumo ya mawasiliano ya kijeshi ya Marekani katika eneo hili sambamba na hujuma iliyofanya dhidi ya kambi tatu za Marekani nchini Kuwait, ikiwa ni hatua endelevu ya kulipiza kisasi dhidi ya ukiukaji unaofanywa na Marekani.
-
Iran yataka Baraza la Usalama la UN kulaani shambulizi la Marekani dhidi ya kituo cha nyuklia cha Darkhovin
Jul 21, 2026 11:31Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa wito kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani bila kusita shambulizi la kombora lililofanywa na Marekani dhidi ya Kituo cha Nishati ya Nyuklia cha Darkhovin, na kuthibitisha tena kuwa shambulizi lolote au tishio dhidi ya vituo vya nyuklia vya amani ni kinyume na sheria za kimataifa.
-
Askari mwingine wa Marekani auawa nchini Iraq huku idadi ya majeruhi ikipanda katika vita na Iran
Jul 20, 2026 04:10Jeshi la Marekani limekiri Jumapili kwamba askari wake mwingine ameuawa kufuatia shambulio la ndege isiyo na rubani ya Iran, huku operesheni za kulipiza kisasi za Jamhuri ya Kiislamu zikiendelea kuwasababishia hasara kubwa askari wa jeshi katili Marekani katika kanda nzima.
-
Iran yaendeleza mashambulizi dhidi ya Kambi za Jeshi la Marekani kulipiza kisasi jinai
Jul 17, 2026 04:14Kufuatia hujuma za kikatili za jeshi la kigaidi la Marekani dhidi ya madaraja kadhaa katika maeneo ya kusini mwa Iran, operesheni kubwa na endelevu ya makombora na droni za Iran imetekelezwa usiku wa kuamkia leo dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Umoja wa Mataifa waonya dhidi ya kutumia vibaya rasilimali za Sudan kufadhili vita
Jul 16, 2026 03:04Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba makundi yanayopigana nchini Sudan yanafaidika kutokana na udhibiti wa rasilimali za nchi hiyo, wakati uchumi wa vita ukichangia katika kuendeleza mzozo huo.
-
Jeshi la Iran kwa Marekani: Lango la Hormuz halitafunguliwa kamwe kupitia vita na uchokozi
Jul 14, 2026 11:14Msemaji wa Jeshi la Iran ametoa onyo kali kwa Marekani kuwa hakuna kitendo chochote cha uchokozi kitakachoweza kulazimisha kufunguliwa kwa Lango la Bahari la Hormuz, kufuatia uamuzi wa Tehran wa kulifunga lango hilo la kimkakati baada ya Marekani kukiuka makubaliano.
-
Iran yawasilisha malalamiko rasmi UN kuhusu ukiukaji wa Marekani wa Mkataba wa Islamabad
Jul 14, 2026 11:12Iran imewasilisha rasmi malalamiko ya kina kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC), ikilaani vikali Marekani kwa kukiuka kwa mfumo Mkataba wa Maelewano (MoU) wa Islamabad uliotiwa saini mwezi uliopita.
-
Serikali ya Sudan na UNICEF zaonya kuhusu kuzorota hali ya kiafya katika maeneo yenye migogoro
Jul 12, 2026 10:46Serikali ya Sudan na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) zimeonya kuhusu mgogoro mbaya wa utapiamlo miongoni mwa watoto nchini Sudan, huku vita na mapigano ya ndani yakiendelea kwa mwaka wa nne sasa.
-
Iran yashambulia kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Oman, Qatar na Bahrain, yafunga Lango Bahari la Hormuz
Jul 12, 2026 04:20Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo asubuhi vimetekeleza operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Qatar, Oman na Bahrain, ikiwa ni hatua ya kujibu mashambulizi endelevu ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
‘Zungumza kwa heshima, Bw. Trump; la sivyo Wairani watajibu kwa lugha tofauti’: Mkuu wa usalama Iran amwambia Trump
Jul 07, 2026 03:30Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Kitaifa la Iran (SNSC), Mohammad Baqer Zolqadr, ametoa jibu madhubuti kwa vitisho vya hivi karibuni vya Rais wa Marekani, Donald Trump dhidi ya taifa la Iran, akisisitiza kwamba Tehran haitavumilia lugha isiyo na heshima na itajibu ipasavyo ikiwa italazimu.