-
Iran: Baraza la Usalama la UN lilaani shambulio la Marekani lililoua raia kwenye sherehe ya harusi
Sep 03, 2026 03:19Iran imeliitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani shambulio la Marekani lililolenga nyumba ya makazi iliyokuwa ikiandaa sherehe ya harusi kusini mwa Jamhuri ya Kiislamu, ambalo limesababisha kuuawa shahidi wa raia watano, akiwemo mtoto wa miaka minne, na kuwajeruhi zaidi ya watu 70 wengine.
-
Waziri wa Fedha wa Ujerumani amwambia Trump: Komesha vita 'visivyo na uwajibikaji' dhidi ya Iran
Aug 29, 2026 10:14Waziri wa Fedha wa Ujerumani amemtaka Rais Donald Trump wa Marekani kukomesha vita "visivyo vya kuwajibika" dhidi ya Iran.
-
Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran: Iran kupanua kwa mafanikio mifumo ya ulinzi
Aug 27, 2026 04:24Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran amesema kuwa Iran inapiga hatua mbele kwa kutegemea kikamilifu uwezo wake wa ndani, ikipanua mifumo yake ya ulinzi wa anga na kuzalisha nakala za mifumo ile iliyofanya vyema wakati wa vita vya siku 40.
-
Malik Agar: Chaguo letu ni suluhisho la kijeshi hadi mazingira ya mazungumzo yatakapotimizwa
Aug 23, 2026 14:19Malik Agar, naibu mkuu wa Baraza Kuu la Utawala nchini Sudan, amesema kwamba chaguo la sasa ni suluhisho la kijeshi mpaka pale mazingira ya kufanyika mazungumzo yatakapotimizwa, akisisitiza kwamba Khartoum inalitaka kundi la Rapid Support Forces (RSF) kuondoka katika miji na maeneo ya makazi ya raia kabla ya mazungumzo yoyote kuanza.
-
Iran yamtahadharisha Trump kuhusu 'fikra potofu' ya kudai Mlango-Bahari wa Hormuz ni eneo la Marekani
Aug 19, 2026 04:16Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia Masuala ya Kisheria na Kimataifa Kazem Gharibabadi amemkosoa vikali Rais Donald Trump wa Marekani kwa madai yake kuhusu Lango la Bahari la Hormuz, akionya kuwa "fikra yake potofu" ya kuihesabu njia hiyo muhimu ya maji kama "eneo jipya la Marekani" inapasa kurekebishwa, la sivyo Tehran itamweka sawa.
-
Mtawala wa Dubai 'azongwa' kwenye mitaa ya London kwa kuhusika UAE katika vita vya Sudan
Aug 12, 2026 03:31Mtawala wa Dubai ambaye ni waziri mkuu wa Muungano wa Falme za Kiarabu, UAE amezongwa kwa maneno katika mitaa ya katikati mwa mji mkuu wa Uingereza, London kuhusiana na ushiriki wa nchi yake katika vita vya ndani nchini Sudan.
-
Yemen yavishambulia vituo vya nishati vya Saudi baada ya nchi hiyo kukiuka anga ya Sa’adah na Hajjah
Aug 09, 2026 11:00Yemen imeishambulia miundombinu ya nishati ya Saudi Arabia ikiwa ni jibu kwa ndege zisizo na rubani za adui zinazokiuka anga ya mikoa ya Sa’adah na Hajjah huko Yemen.
-
Waziri wa Afya wa Iran alaani shambulio la Marekani dhidi ya uwanja wa michezo wa Lamerd Februari mwaka huu
Aug 05, 2026 12:18Waziri wa Afya wa Iran kwa mara nyingine tena amelaani shambulio lililofanywa na jeshi la Marekani dhidi ya uwanja wa michezo katika mji wa Lamerd mwanzoni mwa mashambulizi ya nchii hiyo na utawala katili wa Israel mwezi Februari mwaka huu hapa nchini lililosababisha vifo kuwajeruhi raia kadhaa.
-
Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran yaharibu ndege tatu za F-35 katika kambi ya Marekani huko Jordan
Jul 30, 2026 14:59Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limefanya mashambulizi ya makombora ya balestiki kwenye Kituo cha Anga cha Muwaffaq Salti kinachoendeshwa na jeshi la Marekani huko Azraq, nchini Jordan, na kuharibu ndege tatu za kivita za Marekani aina ya F-35 na kusababisha madhara makubwa kwa ndege nyingine tatu, katika operesheni ya kulipiza kisasi kwa shambulio la anga la Marekani lililoua watu watatu wa familia moja kwenye Kisiwa cha Qeshm nchini Iran.
-
Pezeshkian: Uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na Marekani ufuatiliwe kisheria kimataifa
Jul 27, 2026 03:57Rais Masoud Pezeshkian amelaani mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani dhidi ya miundombinu ya usafiri ya Iran akiyataja kuwa ni "uhalifu wa kivita," na kutaka hatua za kisheria za kimataifa zichukuliwe dhidi ya uharibifu uliosababishwa na nchi hiyo kwenye vituo vya mpakani, vituo vya forodha na mitandao ya usafirishaji.