Apr 01, 2024 11:22
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kwamba, kilichofichuliwa na vyombo vya habari vya Israel kuhusu hatua ya jeshi la utawala huo ya kuanzishwa "maeneo ya kunyonga watu" katika Ukanda wa Gaza, ambapo mtu yeyote anayetembea katika maeneo hayo anauawa, ni jinai ya kikatili ya kivita.