-
Libya yatoa leseni za kwanza za mafuta kwa makampuni ya nishati ya nje tangu kupinduliwa Gaddafi
Feb 12, 2026 07:51Libya imetoa leseni kwa ajili ya uchimbaji na uzalishaji mafuta kwa makampuni kadhaa za nishati za kigeni, ikiwa ni pamoja na makampuni makubwa ya Chevron na BP kwa mara ya kwanza tangu kupinduliwa mamlakani kiongozi wa muda mrefu wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.
-
Serikali ya Kenya yamuongezea mchungaji Mackenzie mashtaka kwa vifo vya watu wengine 52
Feb 12, 2026 03:00Paul Mackenzie, kiongozi wa tapo la kikristo nchini Kenya aliyewaamuru wafuasi wake wajiue kwa njaa wao na watoto wao ili waende mbinguni amesomewa shtaka jengine jipya yeye na wenzake saba la kusababisha vifo vingine 52, kupitia mahubiri yake.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia atahadharisha kuhusu unyonyaji wa madola ya kigeni, ahimiza umoja wa Afrika
Feb 11, 2026 23:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia ametoa wito wa kuwepo Afrika yenye nguvu na mshikamano zaidi ili kulilinda bara hilo dhidi ya 'hatua za unyanyasaji' na ukandamizaji za pande za kigeni.
-
Kimbunga Gezani chaikumba Madagascar, chaua 20 na kujeruhi 33
Feb 11, 2026 22:59Kimbunga cha Tropiki cha Gezani kimepiga mji wa bandari wa Toamasina ulioko kwenye pwani ya mashariki mwa Madagascar, na kuua watu wasiopungua 20 na kujeruhi wengine 33 katika jiji hilo la pili kwa ukubwa kwenye kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi, huku mvua kali na upepo vikisababisha uharibifu mkubwa. Hayo ni kwa mujibu wa mamlaka husika ya nchi hiyo.
-
Mkuu wa Jumuiya ya Madola ahimiza kasi kuelekea mazungumzo ya fidia ya utumwa
Feb 11, 2026 06:18Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth), kundi la mataifa 56 linaloongozwa na Mfalme Charles wa Uingereza, amesema anatarajia nchi wanachama wa jumuiya hiyo zitapiga hatua ya kuanza mazungumzo kuhusu fidia ya biashara ya utumwa iliyovuka Bahari ya Atlantiki.
-
Serikali ya Kenya kusaidia familia za Waislamu wenye njaa mwezi wa Ramadhani
Feb 11, 2026 03:35Serikali ya Kenya imeweka mpango wa kusaidia familia za Kiislamu zilizo katika mazingira magumu huku zikijiandaa kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhan wiki ijayo.
-
Mawaziri Zimbabwe wapitisha muswada kumuwezesha Rais Mnangagwa kutawala hadi 2030
Feb 11, 2026 03:33Baraza la Mawaziri la Zimbabwe limeunga mkono muswada unaokusudia kubadilisha katiba ili kumruhusu Rais Emmerson Mnangagwa kubakia madarakani hadi angalau mwaka 2030.
-
Reuters: Kuna kambi ya siri ya wapiganaji wa RSF nchini Ethiopia
Feb 11, 2026 03:28Ripoti ya shirika la habari la Reuters, iliyotokana na picha za satalaiti na ushuhuda rasmi, imefichua kuwepo "kambi ya siri" nchini Ethiopia kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa maelfu ya wapiganaji wa Rapid Support Forces (RSF), ambao wanapigana na jeshi nchini Sudan.
-
Milio mikali ya risasi yasikika karibu na gereza la Conakry, mji mkuu wa Guinea
Feb 10, 2026 11:38Duru za habari zimearifu kuwa ulinzi mkali umeimarishwa baada ya milio mikali ya risasi kusikika mapema leo karibu na gereza kuu katika mji mkuu wa Guinea, Conakry.
-
Kamanda wa ngazi ya juu wa al Shabaab auawa katika oparesheni ya usalama Somalia
Feb 10, 2026 11:32Idara ya Intelijinsia na Usalama wa Taifa ya Somalia (NISA) leo Jumanne imetangaza kuuawa kiongozi wa ngazi ya juu wa wanamgambo wa kundi la al- Shabaab katika oparesheni ya usalama.