-
Semina ya kumuenzi Imam Shahidi Khamenei yafanyika nchini Tanzania
Jul 07, 2026 08:38"Wakati wananchi nchini Iran wakifanya marasimu ya kuaga na mazishi ya mwili wa ‘Shahidi wa Iran’ Imam Khamenei, wapenzi wake nchini Tanzania pia waliandaa matukio mbalimbali ya maombolezo kwa ajili ya kuomboleza kifo cha shahidi cha Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu."
-
HRW yaishutumu mamlaka ya Tigray kwa kuajiri watu kwa nguvu jeshini
Jul 07, 2026 03:27Shirika la kutetea hazi za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limetangaza kuwa, mamlaka za kikanda katika eneo la kaskazini mwa Tigray nchini Ethiopia zimekuwa zikiwateka nyara na kuwaajiri raia kinyume cha sheria hasa watoto wenye umri wa miaka 15, tangu Aprili 2026.
-
Idadi ya vifo kutokana na maradhi ya Ebola DRC vyafikia 506
Jul 07, 2026 03:21Idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeongezeka na kufikia 506.
-
UNICEF: Zaidi ya watoto 300 wapoteza maisha au kujeruhiwa katika vita vya Sudan kwa kipindi cha miezi sita
Jul 06, 2026 10:31Zaidi ya watoto 300 wameuawa au kujeruhiwa nchini Sudan katika kipindi cha miezi sita iliyopita, huku mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (drones) yakiwa chanzo kikuu cha vifo na majeraha hayo. Hayo yamefichuliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kusaidia watoto (UNICEF) wakati mapigano yakizidi kuenea katika sehemu mbalimbali za nchi hiyo ya Afrika.
-
Nigeria yataka haki baada ya raia wake wawili kuuawa katika machafuko Afrika Kusini
Jul 06, 2026 10:29Nigeria imetangaza kwamba raia wake wawili waliuawa mwezi uliopita nchini Afrika Kusini, kufuatia wimbi la maandamano ya chuki dhidi ya wahamiaji yaliyokuwa yakilenga wafanyakazi kutoka mataifa mengine ya Afrika nchini humo.
-
El Niño kuibua hatari ya maafa barani Afrika
Jul 06, 2026 03:29Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa (WMO) limetangaza kuwa hali ya mkondo joto baharini au El Nino imeanza katika ukanda wa kitropiki wa bahari ya Pasifiki na inatarajiwa kuimarika kwa kasi kati ya mwezi huu wa Julai na Septemba 2026.
-
Kesi za Ebola DRC zapanda na kuvuka 1,500, vifo vyafikia 473
Jul 06, 2026 03:20Idadi ya kesi zilizothibitishwa za ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imevuka 1,500 siku ya Ijumaa, baada ya maambukizi mapya zaidi ya 40 kuripotiwa, kulingana na takwimu rasmi, huku juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo na ufuatiliaji zikiendelea.
-
IOM : Mashambulizi ya RSF yanaweza kuifanya El Obeid nchini Sudan kuwa 'El Fasher nyingine'
Jul 06, 2026 02:48Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetahdharisha kuwa mji wa El-Obeid nchini Sudan, ambao ni makao makuu ya Jimbo la Kordofan Kaskazini, unaweza kukumbwa na hatima sawa na ile iliyoupata mji wa El Fasher katika jimbo jirani la Darfur Kaskazini iwapo mashambulizi yanayofanywa na wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka, Rapid Support Forces (RSF) yataendelea.
-
Zaidi ya Wasudan 1,000 warejea nyumbani kwa hiari kutoka Misri
Jul 05, 2026 03:42Jumla ya raia 1,174 wa Sudan wamerejea nchini kwa hiari wakitokea Misri, ikiwa ni sehemu ya juhudi zinazoendelea kufanywa na Sudan za kuwarejesha nyumbani raia wake wanaotaka kurejea kutoka nje ya nchi.
-
Rais wa Burundi awaalika viongozi wa upinzani kwa mashauriano ya mgogoro wa DRC
Jul 04, 2026 10:49Rais wa Burundi Évariste Ndayishimiye ambaye ni Mwenyekiti wa Kiduru wa Umoja wa Afrika amewaalika wapinzani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mazungumzo yanayolenga kujadili mgogoro wa DRC.