-
"G20" latajwa kuwa neno maarufu zaidi kwa mwaka 2025 nchini Afrika Kusini
Dec 24, 2025 07:55Neno "G20" lilikuwa ndilo neno lililotumika mara nyingi zaidi nchini Afrika Kusini mwaka wa 2025. Hayo ni kwa mujibu wa Bodi ya Lugha ya Afrika Kusini (PanSALB).
-
Mkuu wa majeshi Libya na wenzake wafariki katika ajali ya ndege, serikali yatangaza mambolezo ya siku 3
Dec 24, 2025 02:49Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid Dbeibeh ametangaza kuwa Mkuu wa Majeshi Luteni Jenerali Mohammad Ali Ahmed al-Haddad na maafisa wengine wanne waandamizi wamefariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea wakati walipokuwa wakirejea Libya kutoka kwenye ziara rasmi nchini Uturuki.
-
Mali, Burkina Faso na Niger zaanzisha kituo cha Televisheni kukabiliana na taarifa za upotoshaji
Dec 24, 2025 02:47Viongozi wa Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES), kundi linalojumuisha Mali, Burkina Faso na Niger, umeanzisha shirika jipya la habari lenye makao yake makuu katika mji mkuu wa Mali, Bamako.
-
UN: Robo ya wananchi wa Somalia wameathiriwa na ukame
Dec 23, 2025 23:04Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema ukame umeathiri zaidi ya watu milioni 4.6 nchini Somalia, karibu robo ya idadi ya watu wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Kuzidi kuwa tata vita vya Sudan; indhari ya Umoja wa Mataifa kuhusu kupanuka wigo wake
Dec 23, 2025 08:24Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa sanjari na kusisitiza umuhimu wa kusitisha vita nchini Sudan, ameonya kuhusu utambulisho wake tata na athari zake zinazopanuka kwa nchi jirani na eneo kwa ujumla.
-
Pakistan kumuuzia silaha Haftar wa Libya za dola bilioni 4 zikiwemo ndege za kivita za China
Dec 23, 2025 08:09Shirika la habari la Reuters limeripoti kuwa, Pakistan imesaini makubaliano yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni 4 ya kuuza zana za kijeshi, ikiwa ni pamoja na ndege za kivita zilizoundwa na nchi hiyo kwa kushirikiana na China, kwa kundi liitwalo Jeshi la Taifa la Libya (LNA)LNA linaloongozwa na Jenerali Khalifa Haftar, mmoja wa wababe wakuu wa kivita nchini humo.
-
Sudan yapendekeza usitishaji mapigano kamili chini ya usimamizi wa kikanda na kimataifa
Dec 23, 2025 04:39Waziri Mkuu wa Sudan, Kamil Idris jana Jumatatu, alihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kuwasilisha mpango ambao unajumuisha usitishaji mapigano kamili chini ya usimamizi wa kikanda na kimataifa, akisisitiza kwamba Sudan imelipa gharama kubwa kutokana na mzozo unaoendelea nchini humo.
-
Ndege za kijasusi za Marekani zaruka katika maeneo mbalimbali ya Nigeria
Dec 23, 2025 04:23Ndege za Marekani zimekuwa zikipataa katika maeneo mengi ya Nigeria kwa lengo la kukusanya taarifa za kijasusi tangu mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu.
-
Mataifa ya Maziwa Makuu kutatua mgogoro wa DRC
Dec 22, 2025 23:45Wajumbe kutoka Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameafikiana kwamba nchi za Maziwa makuu zinapaswa kuhusishwa katika juhudi za kuutatua mgogoro huo ambao sasa unaihusisha Burundi moja kwa moja.
-
UNDP yapasisha mradi wa dola milioni 5.8 kulinda Maziwa ya Ubari nchini Libya
Dec 22, 2025 23:44Shirila la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Libya lilitangaza jana Jumatatu kuwa limeidhinisha mradi wa dola milioni 5.8 unaofadhiliwa na Kituo cha Mazingira Duniani (GEF) ili kushughulikia changamoto za mazingira na maendeleo katika bonde la Maziwa ya Ubari huko magharibi mwa Libya.