-
Guterres atoa wito wa uchaguzi wa amani na jumuishi CAR
Dec 25, 2025 08:17Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa raia wote wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR), kushiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao wa nchi hiyo, akisisitiza umuhimu wa utulivu, nidhamu na kuheshimu misingi ya kidemokrasia kabla ya uchaguzi huo uliopangwa kufanyika tarehe 28 Desemba.
-
40 wauawa, kujeruhiwa katika shambulio la bomu Msikitini Maiduguri, Nigeria
Dec 25, 2025 02:13Mripuko mkubwa wa bomu umeripotiwa kutikisa Msikiti mmoja wakati wa Swala ya Magharibi usiku wa kuamkia leo huko mjini Maiduguri, makao makuu ya jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Bunge la Algeria laidhinisha sheria inayojinaisha ukoloni wa Ufaransa
Dec 25, 2025 00:03Bunge la Algeria jana Jumatano lilipasisha kwa kauli moja sheria inayotambua ukoloni wa Ufaransa nchini humo kuwa ni jinai, ikiutaja kuwa ni "uhalifu wa serikali," na kuitaka Ufaransa iombe msamaha rasmi kwa jinai hiyo.
-
Wapiganaji wawateka wasafiri Waislamu nchini Nigeria
Dec 24, 2025 23:16Watu wenye silaha wamewateka nyara wasafiri 28 Waislamu katikati ya Nigeria, mamlaka zimeripoti, likiwa ni tukio jipya katika wimbi la utekaji nyara linalotikisa taifa hilo lenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika.
-
UN yaongeza muda wa kuhudumu askari AUSSOM nchini Somalia
Dec 24, 2025 23:08Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja azimio la kuongeza muda wa Ujumbe wa Umoja wa Afrika wa Msaada na Kurejesha utulivu nchini Somalia (AUSSOM) kwa mwaka mmoja zaidi, hadi tarehe 31 Desemba 2026.
-
Ujumbe wa Libya wawasili Ankara, Uturuki kufuatilia kifo cha Mkuu wa Jeshi
Dec 24, 2025 07:57Ujumbe wa Libya leo Jumatano umewasili Ankara, Uturuki kufanya uchunguzi kuhusu ajali ya ndege binafsi iliyowaua maafisa wakuu wa jeshi la Libya akiwemo Mkuu wa Jeshi wa nchi hiyo, Luteni Jenerali Mohammad Ali Ahmed al-Haddad.
-
"G20" latajwa kuwa neno maarufu zaidi kwa mwaka 2025 nchini Afrika Kusini
Dec 24, 2025 07:55Neno "G20" lilikuwa ndilo neno lililotumika mara nyingi zaidi nchini Afrika Kusini mwaka wa 2025. Hayo ni kwa mujibu wa Bodi ya Lugha ya Afrika Kusini (PanSALB).
-
Mkuu wa majeshi Libya na wenzake wafariki katika ajali ya ndege, serikali yatangaza mambolezo ya siku 3
Dec 24, 2025 02:49Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid Dbeibeh ametangaza kuwa Mkuu wa Majeshi Luteni Jenerali Mohammad Ali Ahmed al-Haddad na maafisa wengine wanne waandamizi wamefariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea wakati walipokuwa wakirejea Libya kutoka kwenye ziara rasmi nchini Uturuki.
-
Mali, Burkina Faso na Niger zaanzisha kituo cha Televisheni kukabiliana na taarifa za upotoshaji
Dec 24, 2025 02:47Viongozi wa Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES), kundi linalojumuisha Mali, Burkina Faso na Niger, umeanzisha shirika jipya la habari lenye makao yake makuu katika mji mkuu wa Mali, Bamako.
-
UN: Robo ya wananchi wa Somalia wameathiriwa na ukame
Dec 23, 2025 23:04Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema ukame umeathiri zaidi ya watu milioni 4.6 nchini Somalia, karibu robo ya idadi ya watu wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.