-
ICC yasikiliza kesi dhidi ya kamanda wa zamani wa Gereza la Mitiga huko Libya kuhusu unyanyasaji
May 19, 2026 11:12Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imefungua kesi dhidi ya kamanda wa zamani wa gereza la Libya, Mohammed Ali El Hishri, anayetuhumiwa kusimamia uhalifu dhidi ya ubinadamu katika kituo maarufu cha kizuizi cha Mitiga karibu na Tripoli.
-
Mgomo wa sekta ya uchukuzi Kenya waahirishwa kuruhusu mazungumzo baina ya serikali na sekta hiyo
May 19, 2026 11:02Mgomo wa sekta ya uchukuzi uliokuwa umeingia siku ya pili nchini Kenya umeahirishwa kwa muda wa siku saba ili kutoa nafasi kwa mazungumzo kati ya serikali na viongozi wa sekta hiyo.
-
Watu wanne wauawa katika maandamano ya bei ya mafuta Kenya
May 19, 2026 05:48Takribani watu wanne wameuawa na wengine 30 kujeruhiwa nchini Kenya wakati maandamano ya kitaifa yakizuka kupinga kupanda kwa kasi kwa bei ya mafuta.
-
Uganda yapitisha sheria ya kudhibiti ushawishi wa kigeni
May 18, 2026 12:03Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ametia saini sheria mpya inayolenga kudhibiti ushawishi wa kigeni nchini humo.
-
Mgomo na maandamano Kenya kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta
May 18, 2026 11:51Maandamano dhidi ya kupanda kwa bei ya mafuta yamezuka katika miji kadhaa nchini Kenya siku ya Jumatatu huku athari mbaya za vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran zikiendelea kuhisika duniani kote.
-
Waziri: Marekani haiwezi kuizuia Afrika Kusini kushiriki kwenye kikao cha G20
May 18, 2026 04:30Waziri wa Afrika Kusini wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ronald Lamola, amesema Marekani haiwezi kuizuia nchi yake kushiriki kwenye Mkutano wa kilele wa nchi za G20 mwezi Desemba, akisisitiza kuwa nchi hiyo ni mwanachama mwanzilishi.
-
Felicien Kabuga aliyekuwa ameshtakiwa kwa mauaji ya kimbari ya Rwanda afariki dunia nchini Uholanzi
May 17, 2026 09:40Felicien Kabuga, aliyekuwa ameshtakiwa kwa kufadhili mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda, jana Jumamosi alifariki dunia katika hospitali huko The Hague, nchini Uholanzi akiwa na umri wa miaka 91.
-
WHO yaainisha mlipuko wa Ebola Congo DR na Uganda kama dharura ya afya ya umma
May 17, 2026 08:45Shirika la Afya Duniani (WHO) limeainisha mlipuko wa virusi vya Ebola vya Bundibugyo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda kama dharura ya afya ya umma inayotia wasiwasi kimataifa.
-
Watu wenye silaha wawateka nyara makumi ya wanafunzi katika Jimbo la Borno nchini Nigeria
May 17, 2026 02:34Watu waliokuwa na silaha wameteka nyara makumi ya wanafunzi wa shule katika jimbo lililokumbwa na machafuko la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Uchunguzi wa awali wabaini utambulisho wa miili 12 iliyopatikana pwani ya Matrouh, Misri
May 16, 2026 12:06Vyanzo rasmi vya Misri vimefichua kwamba miili 12 iliyopatikana kwenye boti ya mpira siku ya Alkhamisi nje ya pwani ya kijiji cha Abu Ghleila katika mji wa Sidi Barrani ni ya vijana wa Misri kutoka majimbo 5 nchini humo.