-
Ebola yaibuka tena nchini DRC, WHO yaimarisha hatua za kukabiliana na mlipuko
May 16, 2026 02:55Shirika la Afya Duniani, WHO, limetangaza kuisaidia kikamilifu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC baada ya kuthibitishwa kwa mlipuko mpya wa ugonjwa hatari wa Ebola katika jimbo la Ituri, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
YouTube yaifuta akaunti ya ‘Sovereign Media’ ya kupinga ubeberu nchini Kenya
May 15, 2026 09:42Kwa hatua iliyowashangaza wengi, YouTube imeiondoa bila taarifa ya awali akaunti ya Sovereign Media, chombo huru cha habari chenye makao yake Nairobi kinachojulikana kwa msimamo wake wa kupinga ubeberu.
-
UN yaonya kuwa mamilioni wanakabiliwa na njaa DRC kutokana na vita
May 15, 2026 09:40Onyo kali limetolewa na Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa kuhusu mgogoro wa njaa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unaoendelea kuwa mbaya zaidi, huku zaidi ya watu milioni 26.5 wakihangaika kupata mahitaji yao ya msingi ya chakula kila siku.
-
HRW yawatuhumu waasi M23 na wanajeshi wa Rwanda kwa mauaji, ubakaji katika mji wa Uvira, Kongo
May 15, 2026 06:01Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeeleza katika ripoti yake kuwa waasi wa kundi la M23 na wanajeshi wa Rwanda waliukalia kwa mabavu na kwa ukatili mji wa Uvira kwa muda wa mwezi mmoja unaopatikana mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo; hatua iliyoambatana na mauaji ya kiholela, ubakaji na kuwateka nyara raia.
-
Rais Macron akabiliwa na upinzani baada ya matamshi yake makali kwenye mkutano wa Nairobi
May 13, 2026 12:14Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anakabiliwa na upinzani mkali baada ya kukatiza kikao cha mjadala katika kongamano la Africa Forward Summit nchini Kenya akiwataka hadhirina wanyamaze kimya.
-
Ghana kuwarejesha nyumbani mamia ya raia walioko Afrika Kusini
May 13, 2026 12:05Ghana imetangaza kwamba imeanzisha mchakato wa kuwahamisha takriban raia wake 300 kutoka Afrika Kusini kufuatia wimbi la maandamano dhidi ya wageni.
-
Kenya yataka Afrika ipewe kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la UN
May 12, 2026 14:25Rais wa Kenya, William Ruto, ametoa wito kwa Afrika kupewa uanachama wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, takwa ambalo limeungwa mkono na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.
-
UN kujenga ofisi mpya yenye thamani ya dola milioni 340 Nairobi
May 12, 2026 09:01Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amshuhudia uwekezaji mkubwa wa Umoja wa Mataifa wenye thamani ya karibu dola milioni 340 katika ofisi yake katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
-
Macron asema Ufaransa “haikuwahi kufikiria” kupeleka jeshi Hormuz bila uratibu na Iran
May 12, 2026 04:28Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema Paris haijawahi kufikiria kupeleka vikosi vya kijeshi vya Ufaransa katika Mlango-Bahari wa Hormuz bila uratibu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wakati mvutano unaochochewa na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran ukiendelea.
-
Ramaphosa: Hujuma dhidi ya wageni haziakisi maoni ya Afrika Kusini
May 12, 2026 04:04Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesema kuwa "wahalifu walipanga mashambulizi dhidi ya wageni na kuzitoa hofu nchi nyingine za Afrika, ambazo zimeelezea wasiwasi wao kuhusu raia wake waliopo Afrika Kusini.