-
Tebboune: Tunao ushahidi unaothibitisha ukatili wa jinai za kikoloni za Ufaransa
Feb 16, 2026 02:29Rais wa Algeria, Abdelmadjid Tebboune, ametangaza kwamba nchi yake iko tayari kuwasilisha nyaraka, ushahidi na ushuhuda kwa vyombo vya kisheria vya Afrika ambavyo "vinathibitisha uhalifu mbaya" wa ukoloni wa Ufaransa nchini Algeria.
-
Watu 10 wauawa katika mashambulizi dhidi ya maeneo ya kijeshi nchini Burkina Faso
Feb 16, 2026 02:27Vyanzo vya usalama vimesema kwamba mashambulizi ya waasi wenye silaha yamewaua watu wasiopungua 10 kaskazini na mashariki mwa Burkina Faso.
-
Umoja wa Afrika wapitisha “Azimio la Algiers” kuhusu uhalifu wa kikoloni barani Afrika
Feb 15, 2026 23:28Kikao cha 39 cha kawaida cha Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kilichofanyika Jumapili jijini Addis Ababa kimepitisha “Azimio la Algiers” kuhusu uhalifu wa kikoloni barani Afrika, huku pia kikiidhinisha tarehe 30 Novemba kuwa Siku ya Afrika ya Mashahidi wa Bara Afrika
-
Waasi wenye silaha wauwa watu wasiopungua 32 kaskazini mwa Nigeria
Feb 15, 2026 04:28Watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki wamevamia vijiji vitatu kaskazini mwa Nigeria, na kuua takriban watu 32 na kuwateka nyara wengine kadhaa.
-
Madagascar yatangaza kimbunga Gezani janga la kitaifa
Feb 15, 2026 04:27Serikali ya Madagascar jana ilitangaza kuwa kimbunga cha Gezani kilichoiathiri nchi hiyo ni janga la kitaifa. Kimbunga hicho cha kitropiki kmesasabisha vifo vya watu 43, majeruhi kadhaa, uharibifu wa miundombinu na makazi na hasara kubwa katika baadhi ya maeneo.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia ahimiza kuwepo uhusiano wa heshima kati ya Afrika na Italia
Feb 15, 2026 04:26Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa Ethiopia amehimiza kuhusu ushirikiano mpya kati ya Afrika na Ulaya unaozingatia utu na ustawi wa pamoja. Waziri Mkuu wa Ethiopia ameeleza haya alipokuwa mwenyeji wa Mkutano wa Pili wa Italia na Afrika mjini Addis Ababa mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Umoja wa Afrika: Mateso dhidi ya Wapalestina lazima yakomeshwe
Feb 14, 2026 23:20Mahmoud Ali Youssouf Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) amesema kuwa, mauaji dhidi ya wananchi wa Palestina ni lazima yakomeshwe. Mahmoud Ali Youssouf alisema hayo jana (Jumamosi) wakati akiufungua mkutano wa kilele wa 39 wa umoja huo.
-
Katibu Mkuu wa UN: Lazima Afrika iwe na sauti na iweze kunufaika na rasilimali zake
Feb 14, 2026 06:26Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito mkali wa kuhakikisha haki na mageuzi yanatekelezwa na kuimarishwa ushirikiano wa kimataifa, huku akiutaja Umoja wa Afrika AU, kama “kinara wa ushirikiano wa kimataifa katika dunia iliyogawanyika”.
-
Rais Xi Jinping wa China: Tutaziondolea ushuru nchi za Afrika ifikapo mwezi Mei
Feb 14, 2026 06:25Rais Xi Jinping wa China ametangaza kuwa, nchi yake itaziondolea ushuru nchi zingine za Afrika ifikapo mwezi Mei mwaka huu.
-
Algeria yaanza operesheni ya kwanza ya kusafisha maeneo ya majaribio ya nyuklia ya Ufaransa
Feb 14, 2026 02:52Algeria jana Ijumaa ilianza kusafisha baadhi ya maeneo ya majaribio ya silaha za nyuklia yaliyofanywa na Ufaransa katika jangwa la nchi hiyo katika kipindi cha ukoloni, miaka ya 1960.