-
DRC yaripoti mlipuko wa Ebola katika mikoa mitano; idadi ya maambukizi yavuka 1,900
Jul 14, 2026 04:39Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeripoti kuenea kwa ugonjwa wa Ebola katika mikoa mitano, huku idadi ya kitaifa ya maambukizi ikipanda na kufikia visa 1,926 vilivyothibitishwa, ikiwa ni pamoja na vifo 702. Haya ni kwa mujibu wa ripoti rasmi iliyotolewa Jumapili na mamlaka za afya nchini humo.
-
Viongozi wa kijeshi wa Libya kutoka Mashariki na Magharibi wakutana kujadili kuliunganisha jeshi
Jul 13, 2026 10:08Saddam Haftar Naibu Kamanda Jeshi la Mashariki mwa Libya amesema kuwa viongozi wakuu wa kijeshi kutoka mashariki na magharibi mwa Libya wamekutana katika mji wa Sirte katikati mwa nchi hiyo kujadili kuunganisha vikosi vya jeshi vilivyogawanyika nchini humo.
-
Shirika la haki za binadamu: RSF inawashikilia raia 6,000 katika magereza ya El Fasher
Jul 13, 2026 08:15Ripoti iliyoandaliwa na Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu nchini Sudan imeonyesha kuwa watu 6,000 wanashikiliwa na wapiganaji wa kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF) katika magereza huko El Fasher, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa nchi, na pia imerekodi ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na kundi hilo dhidi ya raia.
-
Raia wa Zimbabwe warejea nyumbani kutoka Afrika Kusini huku ghasia dhidi ya wahamiaji zikiendelea
Jul 13, 2026 03:03Raia wa Zimbabwe wanaokimbia vurugu na vitisho vya chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini wamewasili katika kituo cha mapokezi katika mji wa mpakani wa Beitbridge, Zimbabwe.
-
Serikali ya Sudan na UNICEF zaonya kuhusu kuzorota hali ya kiafya katika maeneo yenye migogoro
Jul 12, 2026 10:46Serikali ya Sudan na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) zimeonya kuhusu mgogoro mbaya wa utapiamlo miongoni mwa watoto nchini Sudan, huku vita na mapigano ya ndani yakiendelea kwa mwaka wa nne sasa.
-
Mwanamuziki wa Somaliland afungwa jela bila kesi kwa kutunga wimbo wa al-Quds
Jul 12, 2026 04:13Askari usalama katika eneo lililojitenga na Somalia la Somaliland wamemkamata mwanamuziki kijana, Khalid Mohamud Abdillahi, anayejulikana sana kama Khalid Kamil, baada ya kutunga wimbo kuhusu al-Quds iliyokaliwa kwa mabavu. Hayo yameripotiwa na Hiiraan Online, ikinukuu familia yake.
-
Maambukizi ya Ebola yapanda hadi zaidi ya 1,800 nchini DRC huku virusi vikisambaa hadi mkoa wa nne
Jul 11, 2026 11:28Idadi ya visa vilivyothibitishwa vya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imevuka 1,800, kwa mujibu wa takwimu rasmi zilizotolewa siku ya Jumamosi, huku virusi hivyo vikisambaa hadi mkoa wa nne katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Rais Ruto: Kiwanda kikubwa zaidi cha kusafisha mafuta Afrika Mashariki kujengwa Lamu, Kenya
Jul 11, 2026 04:38Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto, ametangaza hatua kuu ya maendeleo ya kiuchumi Ijumaa hii, akithibitisha kuwa mipango ya ujenzi wa kiwanda kikubwa zaidi cha kusafisha mafuta Afrika Mashariki imekamilika.
-
Wamalawi 38,000 waondoka Afrika Kusini kufuatia maandamano ya ghasia dhidi ya wahamiaji
Jul 11, 2026 03:29Wamalawi 38,000 waondoka Afrika Kusini kufuatia maandamano ghasia dhidi ya wahamiaji
-
Wapinzani Kongo wapinga jitihada za Rais Tshisekedi za kuwania muhula wa tatu wa urais
Jul 11, 2026 02:45Wapinzani Kongo wapinga jitihada za Rais Tshisekedi za kuwania muhula wa tatu wa urais