-
Nchi za Magharibi zinaonyesha sura hasi kuhusu Iran ili kushughulisha maoni ya umma kutokana na mizozo ya ndani
Aug 02, 2025 10:34Televisheni ya Al Jazeera ya Qatar iliripoti mnamo Julai 31, 2025 kwamba Uingereza na nchi zingine 13 ziliituhumu Iran kuwa inapanga kufanya mauaji na utekaji nyara katika nchi za Magharibi, madai ambayo yamekanushwa vikali na Tehran.
-
Rais Pezeshkian amewasili Lahore katika ziara ya siku mbili ya kuitembelea Pakistan
Aug 02, 2025 10:11Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili Lahore, mji mkuu wa kihistoria wa Mkoa wa Punjab, katika kituo cha kwanza cha ziara rasmi ya siku mbili nchini Pakistan.
-
Iran: Mauaji ya Shahidi Haniya ilikuwa ni jinai kubwa na ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa
Aug 02, 2025 09:10Wizara ya mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ikieleza kwamba mauaji ya Shahidi Ismail Haniya yaliyofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel mjini Tehran ni jinai kubwa na ukiukaji mkubwa wa misingi na taratibu za sheria za kimataifa, mamlaka ya kujitawala kitaifa na umoja wa ardhi yote ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Khatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Tutaigeuza Tel Aviv kuwa mji wa mizimu kama itakariri upumbavu wake
Aug 01, 2025 10:08Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran, Ayatullah Ahmad Khatami, amewaonya viongozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu athari mbaya za uvunjaji wowote wa usitishaji vita na kusisitiza kuwa, "kama Israel itakariri upumbavu wa aina yoyote, Iran itafanya operesheni kali itakayoigeuza Tel Aviv kuwa mji wa mizimu."
-
Qalibaf amwambia Spika wa Knesset: Nyinyi ni aibu kwa ubinadamu
Aug 01, 2025 10:08Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameandika katika ujumbe wake kwa Spika wa Knesset (Bunge la Israel) kwamba: "Ulimwengu unashuhudia mauaji makubwa zaidi ya kimbari yanayofanywa na Israel. Nyinyi ni aibu kwa ubinadamu."
-
Iran yakadhibisha madai hewa ya US na nchi zingine chache za Magharibi dhidi yake
Aug 01, 2025 04:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani hatua ya Marekani, Ufaransa na nchi nyingine kadhaa za Magharibi ya kukariri tuhuma zisizo na msingi na za kuchekesha dhidi ya Iran na kuzielezea kuwa ni jaribio la waziwazi la kutaka kubebesha lawama wasiohusika na hila ya kuzibabaisha fikra za umma duniani ziachane na suala muhimu zaidi la wakati huu, yaani mauaji ya kimbari katika Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Spika wa Iran: Walimwengu wote wajifunze kutokana na hadaa na utovu wa uaminifu wa Marekani
Jul 31, 2025 23:47Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema, walimwengu wote inawapasa wajifunze kutokana na hadaa ya Wamarekani na akasisitiza kuwa, viongozi na wasomi wenye vipawa wa nchi za Kiislamu wasighafilike na hadaa na utovu wa uaminifu wa Marekani.
-
Maspika wa Mabunge ya Iran na Tanzania wataka kuimarisha ushirikiano wa Kibunge
Jul 31, 2025 09:43Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge ya Dunia (IPU).
-
Rais Pezeshkian: Hakuna nchi inayoweza kuipigisha magoti Iran yenye umoja
Jul 31, 2025 09:06Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa hakuna nchi inayoweza kuwapigisha magoti wananchi wa Iran na hakuna kizuizi chochote kinachoweza kukwamisha ustawi wao madhali wanadumisha umoja na mshikamano wao.
-
Araqchi: Marekani imependekeza kuanza tena mazungumzo na Iran
Jul 31, 2025 09:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi ametaka kufidiwa hasara za vita vya mwezi uliopita na kusisitiza kuwa Marekani inapasa kufidia hasara zilizosababishwa kwa Iran katika vita vya karibuni vya siku 12.