-
Baqaei: Matakwa ya Wairani ya haki na uadilifu hayatafifia
Jun 29, 2025 04:35Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, matakwa ya Wairani ya ukweli na uadilifu hayatafifia, kwa sababu jinai za kivita na jinai dhidi ya ubinadamu hazitapitwa na wakati.
-
Maulamaa wa Ahlu Sunna: Muqawama dhidi ya Wazayuni ni wajibu wa kidini
Jun 29, 2025 04:31Zaidi ya wasomi, wanazuoni na wanafikra wa Kisunni wa Iran 1,300 wamesisitiza katika taarifa yao kwa viongozi na vijana wa nchi za Kiislamu kwamba: Kusimama kidete (muqawaama) na kuwapinga makafiri wanaoupiga vita Uislamu na kuunga mkono kambi ya Kiislamu kwa sasa ni wajibu wa kidini na "wajibu wa Kimwenyezi Mungu".
-
Je, Iran ilipata mafanikio gani ya kimkakati katika Vita vya Siku 12?
Jun 29, 2025 00:54Licha ya Vita vya siku 12 kati ya utawala wa Kizayuni na Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kusababisha hasara kubwa ya kimaada na isiyo ya kimaada, lakini pia vimekuwa na mafanikio ya kistratijia kwa Iran.
-
Araqchi: Kila tishio dhidi ya Iran linapelekea tu kudhihirika nguvu halisi ya taifa hili
Jun 28, 2025 23:16Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran ametoa radiamali kwa bwabwaja na uropokaji wa Rais wa Marekani na kusisitiza kuwa, kuheshimiana pande mbili ni sharti la mazungumzo na kwamba, vitisho au udhalilishaji wowote hauna natija yoyote ghairi ya kudhihirisha nguvu halisi ya Iran.
-
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran: Vidole vyetu viko kwenye kitufe cha bunduki
Jun 28, 2025 23:15Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran amekosoa vikali sera za Marekani na utawala haramu wa Israel pamoja na hatua zao za kuutoheshimu ahadi na makubaliano yoyote.
-
China kwa Marekani: Tutajidhaminia nishati kwa kuzingatia maslahi ya kitaifa
Jun 28, 2025 08:02Akijibu matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani kwamba Beijing inaweza kununua mafuta kutoka Tehran, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesisitiza kuwa nchi yake inajidhaminia nishati kwa kuzingatia maslahi yake ya kitaifa.
-
Barua ya malamiko ya Iran kwa Umoja wa Mataifa kuhusu matamshi yasiyo na haya ya Israel na Marekani dhidi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Jun 28, 2025 07:52Katika barua yake kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Baraza la Usalama na Mwenyekiti wa Baraza Kuu la umoja huo, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani vikali matamshi yasiyo na haya yanayotolewa na watawala wa Marekani na Wazayuni dhidi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
-
Russia: Teknolojia ya nyuklia ya Iran haiwezi kuharibiwa kwa mabomu
Jun 28, 2025 07:47Sergei Ryabkov, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia akizungumzia mashambulizi ya karibuni ya Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran vinavyoendesha shughuli zake kwa malengo ya amani amesisitiza kuwa, ujuzi, uzoefu, teknolojia na utashi wa kisiasa wa Iran hauwezi kuharibiwa kwa mabomu.
-
Baqaei: Iran inataka amani lakini haitasalimu amri mbele ya ukandamizaji
Jun 28, 2025 07:44Esmaile Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Iran imejidhatiti kwa ajili ya suala la amani, lakini kwamba haitasalimu amri abadan mbele ya maadui
-
Mazishi ya mashahidi 60 katika mji wa Tehran; dhihirisho la umoja na kupinga ubeberu
Jun 28, 2025 04:28Leo Jumamosi tarehe 28 mwezi Juni 2025 inayosadifiana na tarehe pili Muharram 1447 Hijria Tehran inashuhudia shughuli kubwa na ya kihistoria ambapo zaidi ya mashahidi 60 wa muqawama kuanzia makamanda wa jeshi hadi raia wa kawaida wa wanawake na watoto, wameagwa na umati mkubwa wa wananchi wanamapinduzi wa Iran.