-
Iran yapokea ‘vipengele vya’ mapendekezo ya Marekani kupitia Oman
Jun 01, 2025 01:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amethibitisha kuwa nchi yake imepokea baadhi ya vipengele vya mapendekezo kutoka kwa Marekani, yaliyowasilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, ambaye nchi yake inatekeleza jukumu la upatanishi katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Tehran na Washington.
-
Iran: Hatutakubali utwishaji wa Magharibi; tutaendelea kurutubisha urani
May 31, 2025 08:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amepinga vikali mashinikizo ya nchi za Magharibi ya kuitaka Jamhuri ya Kiislamu iache kurutubisha madini ya urani, akiyataja mashinikizo hayo kuwa ni juhudi za kulitwisha taifa la Iran matakwa yao.
-
Iran yalalamika kufuatia matamshi ya kichochezi ya Austria kuhusu mpango wa nyuklia
May 31, 2025 04:30Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imemwita Naibu Balozi wa Austria mjini Tehran kulalamikia kile ilichokitaja kuwa ni madai ya “kutowajibika na ya kichochezi” yaliyotolewa na idara ya ujasusi ya ndani ya Austria kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran ambao ni wa amani.
-
Ayatullah Khatami: Iran katu haitalegeza msimamo kwa haki yake ya matumizi ya nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani
May 30, 2025 08:05Imamu wa muda wa Swala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa, Iran katu haitalegeza msimamo kwa haki yake ya matumizi ya nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani.
-
Rais Pezeshkian: Silaha za nyuklia hazina nafasi katika doktrini ya Jamhuri ya Kiislamu
May 30, 2025 07:43Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesisitiza kuwa, Iran kamwe haitaacha haki yake ya kisheria ya kurutubisha madini ya urani.
-
Iran yakanusha taarifa za kukaribia makubaliano na Marekani
May 30, 2025 04:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesisitiza dhamira ya Tehran ya kuendelea kushiriki katika mchakato wa kidiplomasia, huku akilaani kile alichokieleza kuwa ni upotoshaji wa vyombo vya habari unaolenga kuvuruga mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yanayoendelea kati ya Iran na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais Pezeshkian: Iran iko tayari kushirikiana kuthibitisha malengo ya amani ya nyuklia
May 29, 2025 07:15Rais Masoud Pezeshkian wa Iran, amesema kuwa nchi yake iko tayari kushirikiana kikamilifu kwa njia yoyote ile ili kudhihirisha kuwa shughuli zake za nyuklia ni za amani, lakini haitakubali kwa vyovyote vile kuacha haki yake ya kimsingi ya kurutubisha madini ya urani.
-
Araghchi: Iran haitaruhusu kuvurugwa kwa uhusiano na Saudi Arabia
May 29, 2025 07:09Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, amesisitiza dhamira ya Iran ya kudumisha uhusiano wa "kidugu" na Saudi Arabia, akisema kuwa Tehran haitakubali yeyote kuvuruga mahusiano hayo muhimu kwa ulimwengu wa Kiislamu.
-
Iran yazindua mpango wa kuzalisha megawati 20,000 za umeme wa nyuklia
May 29, 2025 01:05Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema Jamhuri ya Kiislamu imezindua mpango unaolenga kuzalisha hadi megawati 20,000 za umeme kutokana na shughuli zake za amani za nishati ya nyuklia.
-
Kamanda wa IRGc asema Iran imejiandaa kwa kila hali, aionya Marekani
May 29, 2025 01:01Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Meja Jenerali Hossein Salami, amepuuza vikali vitisho vya kijeshi kutoka Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akisisitiza kuwa taifa hili limejiandaa kikamilifu kukabiliana na hatari yoyote, na lina uwezo wa kujilinda dhidi ya aina zote za vitisho.