-
Iran: Itibari ya Troika ya Ulaya imeporomoka kwa kuunga mkono uvamizi wa Israel
Jul 14, 2025 10:42Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya sheria na kimataifa amesema kuwa Troika ya Ulaya, yaani Ufaransa, Ujerumani na Uingereza zilisambaratisha itibari na uaminifu wao wenyewe kwa kuunga mkono vitendo vya uchokozi vya utawala wa Israel dhidi ya Iran.
-
Jenerali Mousavi: Makombora ya Iran yalikata mikono ya maadui
Jul 14, 2025 09:13Kamanda mkuu wa Jeshi la Iran amevipongeza vikosi vya anga vya nchi hii kwa mashambulio madhubuti ya makombora waliyoyafanya dhidi ya maadui wa taifa hili mwezi uliopita na kuonya kwamba, kosa lolote litakalorudiwa litakabiliwa kwa jibu kali zaidi.
-
Araghchi: Netanyahu 'anaiamuru waziwazi' Marekani cha kufanya katika mazungumzo na Iran
Jul 14, 2025 00:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel ameshindwa kufikia lolote kati ya malengo ya vita vya karibuni vya utawala huo ghasibu dhidi ya Iran.
-
Mabalozi wa nchi 28 wakagua jengo la IRIB lililoshambuliwa na jeshi la kizayuni
Jul 13, 2025 12:10Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB), Peyman Jebelli, amewapokea mabalozi wanaowakilisha nchi 28 hapa mjini Tehran waliofanya ziara ya kukagua moja ya majengo ya IRIB lililolengwa na shambulio la kigaidi la jeshi la utawala wa kizayuni Israel mwezi uliopita.
-
Wabunge wa Iran waandaa muswada wa kuimarisha vikosi vya ulinzi kwa vita kamili na Israel
Jul 13, 2025 10:46Wabunge wa Iran wamo mbioni kuandaa mswada wa kuongeza bajeti ya matumizi ya kijeshi kwa lengo la kuviimarisha Vikosi vya Ulinzi kwa ajili ya makabiliano ya kijeshi ya pande zote na utawala haramu wa kizayuni wa Israel.
-
UNESCO yaongeza Bonde la Khorramabad la Iran kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia
Jul 13, 2025 10:46Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeongeza rasmi maeneo ya kale ya enzi ya mawe katika Bonde la Khorramabad, lililoko katika jimbo la Lorestan, magharibi mwa Iran, kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia.
-
Nini madhumuni ya barua mpya ya Iran kwa Baraza la Usalama kuhusiana na uvamizi wa kijeshi wa Israel dhidi ya Iran?
Jul 12, 2025 23:05Amir Saeid Iravani Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amemuandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama la umoja huo, na kuwasilisha ripoti iliyosasishwa kuhusu uharibifu uliosababishwa na uvamizi mkubwa wa kijeshi na wa bila ya sababu wa utawala wa Israel dhidi ya Iran.
-
Iran: Imani yetu kwa Marekani imeporomoka mno
Jul 12, 2025 12:30Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema Marekani imedhoofisha diplomasia na kukiuka sheria za kimataifa kwa mashambulizi yake ya kichokozi dhidi ya taifa hili, wakati mazungumzo ya nyuklia yalipokuwa yakiendelea, na hivyo kupunguza imani ya Iran kwa Marekani chini ya sifuri.
-
Araghchi: Iran haijasitisha ushirikiano wake na IAEA
Jul 12, 2025 10:59Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, ushirikiano wa Iran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki haujasimamishwa na kusisitiza kuwa, sisitizo la Ulaya kuhusu kuhuisha mchakato wa kurejeshwa vikwazo vya nyuklia dhidi ya Tehran litahitimisha jukumu lao katika faili la atomiki la Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kamanda Mkuu: Jeshi la Iran liko katika hali ya juu ya utayarifu wa kivita
Jul 12, 2025 03:55Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Iran amethibitisha kwamba Jeshi la Nchi hii linaendelea kudumisha kiwango cha uwezo wake “kamili.” Ametoa kauli hii chini ya mwezi mmoja tangu Majeshi ya Iran yalipojibu haraka na kwa ufanisi mashambulizi ya Israel, yaliyomlazimu adui Muisraeli kuomba kusitisha mapigano.