-
Msemaji wa IRGC: Tunavisubiri kwa hamu kubwa vikosi vya US kwenye Lango-Bahari la Hormuz
Mar 07, 2026 14:18Msemaji wa Kamandi ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC ya Khaatamul-Anbiyaa amesema: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inakaribisha na kusubiri kwa hamu kubwa kuthibiti kwa madai ya vikosi vya jeshi la Marekani vya kusindikiza meli za mafuta na kujikita kwenye Lango-Bahari la Hormuz.
-
Iran: UN inabeba dhima ya kisheria na kimaadili ya vita haramu vya US, Israel
Mar 07, 2026 10:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei amejibu taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ambaye bila kulaani uvamizi na mashambulizi ya kichokozi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, ameeleza wasiwasi wake juu ya vita hivyo kwa uchumi wa dunia.
-
Maulamaa wa Kishia na Kisunni, wa ndani na nje ya Iran watoa fatua ya Jihadi dhidi ya Marekani na utawala wa kizayuni
Mar 07, 2026 08:37Maraajii Taqlidi wa madhehebu ya Shia, ndani na nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, pamoja na Maulamaa wakubwa wa Kisunni wa hapa nchini na katika mataifa mengine ya Ulimwengu wa Kiislamu wametoa fatua ya Jihadi dhidi ya Marekani na utawala wa kizayuni wa Israel kufuatia uchokozi wa kidhalimu walioanzisha dhidi ya ardhi ya Iran.
-
Mazungumzo ya simu kati ya Vladimir Putin na Masoud Pezeshkian
Mar 07, 2026 04:07Rais wa Russia, Vladimir Putin, amefanya mazungumzo ya simu na Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian kuhusu matukio ya hivi karibuni katika eneo, ambapo Rais wa Iran amesisitiza kuwa: “ Njia yetu ni kujihami kwa nguvu ili kulinda mipaka yetu na kuleta amani endelevu.
-
Siku ya 7 ya Vita; Vikosi vya Iran Vyalenga Kitovu cha Tel Aviv
Mar 06, 2026 12:29Katika siku ya saba ya vita vya kukabiliana na uchokozi wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza wimbi la ishirini na moja la Operesheni “Ahadi ya Kweli 4”, likihusisha mashambulizi ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni), pamoja na kurushwa kwa makombora ya Kheibar yenye vichwa vingi vya kivita dhidi ya malengo yaliyoko katikati ya Tel Aviv.
-
Pezeshkian: Iran imesimama kidete katika kujihami, kulinda heshima ya taifa
Mar 06, 2026 10:28Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haitasita kuendelea kujihami na kujilinda mkabala wa mashambulizi ya kichokozi ya maadui wa taifa hili.
-
Araqchi: Yoyote anayeendeleza vita atakwama kwenye kinamasi
Mar 06, 2026 09:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema katika mahojiano yake na mwandishi habari Tom Llamas wa televisheni ya NBC kwamba: Serikali ya Marekani inahusika kikamilifu na umwagaji damu unaoshuhudiwa hivi sasa.
-
Msemaji wa IRGC: Silaha mpya za Iran za kukabiliana na uchokozi wa adui Marekani na mzayuni ziko njiani
Mar 06, 2026 09:06Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, IRGC ametangaza kuwa mbinu mpya na silaha mpya ziko njiani kuzinduliwa kwa ajili ya kukabiliana na uchokozi wa kijeshi ulioanzishwa na Marekani na utawala wa kizayuni.
-
Mohsen Rezaei: Tutaifukuza Marekani kutoka Ghuba ya Uajemi
Mar 06, 2026 03:50Kamanda wa zamani wa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amezungumzia matukio ya hivi karibuni ya vita na kusema: “Wananchi wa Iran wanapaswa kufahamu kwamba wana wao walioko katika vikosi vya ulinzi wako tayari kuwafundisha wahalifu Donald Trump na Benjamin Netanyahu funzo kali kiasi kwamba hawatathubutu tena kufanya jeuri ya aina hii.”
-
Khorramshahr-4 yaingia uwanjani katika operesheni Ahadi ya Kweli 4, yatwanga ngome za Israel
Mar 05, 2026 15:02Idara ya Uhusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (Sepah) imetangaza kuwa makombora ya Khorramshahr 4, (Khaybar), ya kikosi cha Anga cha jeshi hilo yameanza kutumika kwa kushambulia katikati ya mji wa Tel Aviv, Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion na kambi ya jeshi la anga la Israel katika uwanja huo.