-
Majibu ya Tehran kwa Shutuma za Uongo za Ufaransa Kuhusu Mpango wa Nyuklia wa Amani wa Iran
Apr 30, 2025 22:48Mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeed Iravani, amewatumia barua Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akielezea kuwa madai ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa kwamba Iran iko "katika hatua ya mwisho" ya kuzalisha silaha za nyuklia ni yasiyo na msingi na kisiasa ni hatua isiyo ya uwajibikaji. Iran haijawahi kuwa na nia ya kutafuta silaha za nyuklia na haijabadilisha sera yake ya ulinzi.
-
Jasusi wa MOSSAD nchini Iran anyongwa, mtandao wake wasambaratishwa
Apr 30, 2025 08:28Katika pigo kubwa la kiusalama kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na vibaraka wake, Mahakama ya Iran imetangaza mapema leo Jumatano kwamba imetekeleza hukumu ya kunyongwa mmoja wa majasusi wakubwa wa shirika la ujasusi la Israel, MOSSAD.
-
Waitifaki wa Trump: Maajenti wa Mossad wanajaribu kuvuruga mazungumzo ya Iran na Marekani
Apr 30, 2025 08:25Vyombo vya habari na wafuasi wa karibu na Rais Donald Trump wa Marekani wamesema kuwa mawakala wa Mossad na wapenda vita wanaisukuma Marekani katika mzozo na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran; mshirika wa Sudan katika kujenga upya miundombinu ya viwanda
Apr 30, 2025 07:58Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza udharura wa kustawisha na kuimarisha uhusiano na Sudan na kusema: Iran iko tayari kushiriki katika kujenga upya viwanda vya nchi rafiki na ndugu ya Sudan.
-
Araqchi asisitiza kuimarishwa ushirikiano kati ya Iran na Algeria katika majukwaa ya kimataifa
Apr 30, 2025 07:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi amesisitiza umuhimu wa kuimarishwa ushirikiano kati ya Iran na Algeria katika vikao vya kimataifa na katika ngazi ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu ili kuunga mkono haki za wananchi wa Palestina.
-
Iran yatangaza utayarifu wa kupanua ushirikiano na Afrika katika nyanja za afya na tiba
Apr 30, 2025 03:49Mshauri Mkuu wa Waziri wa Afya na Elimu ya Tiba wa Iran ametangaza utayarifu wa sekta ya afya ya Jamhuri ya Kiislamu wa Iran kupanua ushirikiano wa kiuchumi na nchi za Kiafrika.
-
Aref: Msingi wa kuimarika uhusiano wa Iran, Niger ni Mapinduzi ya Kiislamu
Apr 29, 2025 23:03Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad-Reza Aref amesema Jamhuri ya Kiislamu imekuwa ikitekeleza sera yake ya kukuza uhusiano na Niger na mataifa mengine ya bara la Afrika kwa kuzingatia thamani na maadili ya Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Safari ya siku moja ya Rais wa Iran nchini Azerbaijan
Apr 29, 2025 09:37Rais wa Iran Masoud Pezeshkian amerejea Tehran baada ya ziara rasmi ya siku moja mjini Baku ambako alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Azerbaijan Ilham Aliyev.
-
Qalibaf: Uhai wa utawala wa Kizayuni unategemea mauaji na jinai
Apr 29, 2025 08:52Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) ameyataja matamshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa ni hila isiyo na thamani inayolenga kuvuruga mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani na kusema: "Hata asilimia ndogo ya uchokozi dhidi ya Iran itatambuliwa kuwa ni sawa na kuwasha moto pipa la baruti ambalo litalipua katika eneo hili."
-
Baqaei: IAEA inatakiwa kufanyia kazi masuala ya kiufundi, na si ya kisiasa
Apr 28, 2025 23:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Iran inataraji kuwa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) utachukua hatua kwa mujibu wa majukumu yake ya kiufundi kuhusu miradi ya nyuklia ya Iran.