-
Siku ya Jeshi: Kiongozi apongeza jeshi la Iran kwa ujasiri katika kulilinda taifa dhidi ya wavamizi
Apr 19, 2026 10:57Katika ujumbe alioutoa Jumapili kwa mnasaba wa Siku ya Jeshi, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Mojtaba Khamenei amelisifu Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kusimama kwa ujasiri kulilinda taifa katika vita vya hivi karibuni vya kulazimishwa, kama lilivyofanya katika vita vya kulazimishwa vya awamu zilizopita.
-
Iran kudhibiti trafiki ya Lango Bahari la Hormuz hadi makubaliano yafikiwe kumaliza vita
Apr 19, 2026 10:50Baraza la Juu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) limesema kwamba Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kusimamia na kudhibiti trafiki yote inayopita katika Lango Bahari la Hormuz, ambalo ni njia ya kimkakati, hadi kufikiwa mapatano kamili ya kumaliza vita vya kulazimishwa vya Marekani na Israel dhidi ya nchi hii.
-
Esmaeil Baqaei: Iran yasema haitakubali ubabe wa Marekani katika mazungumzo
Apr 16, 2026 06:05Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei, amesisitiza kuwa Iran ilikataa mapendekezo aliyoyaita “yasiyo na mantiki” yaliyowasilishwa na Marekani katika mazungumzo yaliyofanyika Islamabad, akionya kuwa Tehran haitawahi kukubali mazungumzo yanayoendeshwa kwa mfumo wa ubabe na kulazimisha masharti.
-
Iravani: Silaha zilizotumiwa katika uvamizi dhidi ya Iran zilitoka kwenye maghala ya baadhi ya nchi za Kiarabu
Apr 15, 2026 08:08Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amepinga madai ya Bahrain, akisema: Mabaki yaliyopatikana kutoka kwenye silaha zilizotumiwa katika mashambulizi ya miji ya Iran yanathibitisha kuwa silaha hizo zilitoka kwenye maghala ya baadhi ya nchi za kiarabu za Ghuba ya Uajemi.
-
Pezeshkian: Taifa la Iran limemfanya adui akate tamaa kwa mapambano yake ya siku 40
Apr 12, 2026 09:32Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametilia mkazo nafasi muhimu ya Muqawama na mapambano ya kitaifa katika kuvuka kipindi na hali ya vita na kusema: "Taifa la Iran, limemfanya adui akate tamaa na kukosa matumaini kwa Muqawama na mapambano yake ya siku 40."
-
Mwanazuoni wa Ahlu‑Sunnah wa Russia: Imam Khamenei hakukubali udhalili
Apr 12, 2026 08:50Mufti wa Volgograd, nchini Russia amesema: Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ni shahidi mkubwa wa Umma wa Kiislamu na mfuasi wa Suna ya Mtume Muhammad (S.A.W.), na jina lake litasalia katika historia kama kiongozi jasiri na mwanaume halisi.
-
Jeshi la IRGC lashambulia Kamandi ya Jeshi la Marekani na ngome za Israel katika Ghuba ya Uajemi
Apr 06, 2026 04:50Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetekeleza wimbi jipya la mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya shabaha mbalimbali zenye mfungamano na Marekani na Israel katika eneo la Ghuba ya Uajemi katika sehemu ya wimbi la 97 la Oparesheni Ahadi ya Kweli-4.
-
Qalibaf amwambia Trump: Kutii maagizo ya Netanyahu kutawasha moto kwenye kanda nzima
Apr 06, 2026 02:28Spika wa Bunge la Iran amejibu vitisho vya hivi karibuni vya Donald Trump, rais gaidi wa Marekani katika ujumbe wake kwenye mtandao wa kijamii wa X akisema tabia yake ya kutii na kufuata maagizo ya waziri mkuu katili wa Israel Benjamin Netanyahu kutawasha zaidi moto wa vita katika kanda nzima ya Magharibi mwa Asia.
-
Baghaei: Vita vilivyotwishwa Iran vimelenga utambulisho wa Iran
Apr 06, 2026 02:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: Vita vya kulazimishwa vya Wamarekani na Wazayuni dhidi ya Iran vimelenga uwepo na utambulisho wa Kiirani.
-
Aragchi: Tishio la Trump dhidi ya miundombinu ya nishati Iran ni kukiri uhalifu wa kivita
Apr 05, 2026 22:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa vitisho vya Marekani vya kushambulia miundombinu ya nishati ya Iran ni kukiri wazi nia ya kutenda uhalifu wa kivita.