-
Makubaliano ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China ya kutekeleza mpango wa kistratejia wa nchi mbili
Dec 29, 2024 08:38Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China wametathimini kuwa chanya mchakato unaopiga hatua wa kutekeleza vipengee vya ushirikiano wa kistratejia katika miaka ya karibuni.
-
Araghchi: Mkataba wa ushirikiano wa miaka 25 ni msingi thabiti wa kuendeleza uhusiano Iran na China
Dec 29, 2024 04:14Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhurii ya Kiislamu ya Iran ameashiria historia ndefu na imara ya uhusiano kati ya mataifa mawili ya Iran na China, na kueleza kuwa, Tehran haitaacha juhudi zozote za kutumia fursa nyingi na Beijing, na kwamba, mpango wa miaka 25 ni msingi thabiti wa kupanua ushirikiano katika nyanja mbalimbali.
-
Iran: Marekani inalenga kuwapora Waislamu, haitafanikiwa chochote nchini Syria
Dec 28, 2024 23:23Jeshi la Iran linasema kutimuliwa kwa Rais Bashar al-Assad wa Syria na wanamgambo wanaoungwa mkono na mataifa ya kigeni ni njama ya Wamarekani na Wazayuni, lakini Marekani haitafanikiwa lolote katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Iran: Shambulio la Israeli katika Hospitali ya Kamal Adwan ni 'uhalifu mbaya wa kivita'
Dec 28, 2024 23:23Iran imekemea shambulio la kikatili la utawala wa Israel kwenye Hospitali ya Kamal Adwan katika eneo la kaskazini mwa Gaza kama “uhalifu mbaya wa kivita” na sehemu ya mauaji ya kimbari yanayoendelea kwenye ardhi za Palestina zilizokaliwa kwa mabavu na kusema kimya cha taasisi muhimu za kimataifa kuhusu suala hilo kama “hakikubaliki.”
-
Mkuu wa IRGC: Wayemeni hatimaye wataibuka washindi
Dec 28, 2024 10:08Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amelipongeza taifa la Yemen kwa kulitetea kwa ushujaa taifa la Palestina wakati huu wa hujuma ya umwagaji damu ya Israel dhidi ya Wapalestina wa Gaza na kueleza kuwa Wayemen hatimaye wataibuka washindi.
-
Ushauri muhimu wa Araghchi kwa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu
Dec 28, 2024 04:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesisitiza katika ushauri wake kwa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuhusu matukio ya Syria kuwa: ili kuondokana na kipindi hiki hahtari sana katika eneo hili, nchi zote zinapaswa kutumia busara, ushirikiano, kushirikishwa makundi yote, kuepuka migawanyiko na kutojali maslahi binafsi.
-
Araqchi: Kuvuka kipindi cha sasa kunahitaji kujiepusha na mifarakano
Dec 28, 2024 03:59Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amewaambia maafisa wakuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kwamba: Kuvuka kipindi hiki chenye taharuki nyingi katika eneo la Magharibi mwa Asia kunahitaji busara, ushirikishwaji, ushirikiano na kuepusha mizozo na kujitakia maslahi ya muda mfupi.
-
Rais wa Iran kutembelea Russia mwezi ujao kutia saini mkataba muhimu wa ushirikiano
Dec 27, 2024 23:39Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran atafanya ziara nchini Russia mwezi ujao ili kutia saini makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati wa kina kati ya nchi hizo mbili.
-
Iran na Saudi Arabia kuimarisha uhusiano katika sekta ya teknolojia
Dec 27, 2024 23:14Rais wa Shirika la Teknolojia ya Habari na Mawasiliano la Iran na Rais wa Kamati ya Mawasiliano, Anga za Mbali na Teknolojia (CST) ya Saudi Arabia katika mkutano wa pamoja huko Riyadh wamesisitiza kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu katika nyanja mbalimbali za teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA)
-
Ayatullah Siddiqi: Marekani ni mpangaji na mbunifu nambari moja katika uporaji na vita vyote
Dec 27, 2024 08:24Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo hapa mjini Tehran ameeleza kuwa, Marekani ndiye mpangaji mkuu katika mapinduzi yote, uporaji na vita na akasema: Jambo la lisilo na shaka ni kwamba suala la Syria kidhahiri lilionekana kuwa ni tukio lakini kwa ndani ilikuwa ni njama.