-
Rais Pezeshkian kukutana na Marais wa Russia, China na Afrika Kusini
Oct 23, 2024 04:33Rais wa Iran, Massoud Bishikian, leo Jumatano atakutana na marais wa Russia, China Afrika Kusini na viongozi baadhi ya nchi zinazoshiriki katika mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Kiuchumi ya BRICS ulianza jana katika mji wa Kazan nchini Russia.
-
IRGC: Hatua yoyote ya Israel dhidi ya Iran itakabaliwa na majibu makubwa zaidi
Oct 23, 2024 04:28Kamanda wa ngazi ya juu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameonya kwamba iwapo Wazayuni watachukua "hatua kubwa" dhidi ya Iran, bila shaka watakabiliwa na jibu kubwa "mara kadhaa zaidi".
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Visiwa vitatu vya Bu Musa na Tunb Kubwa na Ndogo ni mali ya Iran
Oct 23, 2024 00:15Makamu wa kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuhusu madai ya Imarati ya kumiliki visiwa vitatu vya Bu Musa na Tunb Kubwa na Ndogo kwamba, kila mtu anajua kwamba visiwa hivi ni vya Iran na Jamhuri ya Kiislamu katu haitalegeza kamba kwa vyovyote vile kuhusiana na visiwa hivyo.
-
Qalibaf atoa wito wa kuwekewa vikwazo vya kiuchumi, kukata mishipa ya uhai ya Israel
Oct 22, 2024 22:58Spika wa Bunge la Iran amezitaka nchi za Kiislamu kuchukua hatua kwa uratibu na kufanya kazi kwa ajili ya kuweka "vikwazo vya kiuchumi na kukata njia muhimu za uhai wa utawala dhalimu wa Israel."
-
Rais wa Iran: Marekani na nchi za Ulaya ni watetezi wa uhalifu dhidi ya binadamu
Oct 22, 2024 11:56Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Nchi za Ulaya na Marekani zimeupatia silaha kwa nguvu zote utawala wa Israel na zinatetea jinai dhidi ya binadamu bila haya wala kuona soni.
-
Araqchi aionya Israel: Iran ina mbinu za kulinda taasisi zake za nyuklia
Oct 22, 2024 11:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameuonya utawala wa Kizayuni Israel dhidi ya kufanya mahesabu mabaya na kusisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inategemea zana za kijeshi zilizotengenezwa hapa nchini na pia mbinu mbalimbali ili kulinda taasisi zake za nyuklia zenye malengo ya kiraia.
-
Safari ya Pezeshkian nchini Russia na mahudhurio ya kwanza rasmi ya Iran katika BRICS
Oct 22, 2024 05:42Mkutano wa 16 wa wakuu wa Jumuiya ya Kiuchumi ya BRICS umeanza leo katika mji wa Kazan nchini Russia. Rais Masoud Pezeshkian wa Iran anahudhuria mkutano huo unaotarajiwa kuendelea hadi 24 Oktoba.
-
Iran yaliandikia barua Baraza la Usalama ikilaani chokochoko za US
Oct 22, 2024 03:46Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amekosoa vikali matamshi ya hivi karibuni ya Rais Joe Biden wa Marekani kuhusiana na njama ovu ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Tehran na kusisitiza kuwa, matamshi hayo "yanatia wasiwasi sana na ni ya kichochezi."
-
Iran yataka majirani wa Ghuba ya Uajemi wasihadaiwe na vishawishi vya Wamagharibi
Oct 21, 2024 22:54Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran ameyataka mataifa jirani na Iran ya Ghuba ya Uajemi yasidanganyike na vishawishi vya nchi za Magharibi.
-
IRGC: Vikosi vya Ulinzi vya Iran viko tayari kujibu tishio lolote dhidi ya Iran
Oct 21, 2024 08:09Naibu Kamanda wa Uratibu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) amesisitiza kuwa vikosi vya ulinzi vya nchi hii vimejiandaa kikamilifu kujibu tishio lolote dhidi ya nchi hii kufuatia kupamba moto mivutano katika eneo.