-
Kanaani: Hasira za Netanyahu na Sunak kuhusu mabadiliko ya Asia Magharibi sio jambo ajabu
Mar 25, 2023 13:17Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuuri ya Kiislamu ya Iran, amejibu matamshi yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu na mwenzake wa Uingereza, Rishi Sunak dhidi ya Iran ya Kiislamu katika mkutano wao hapo jana na kueleza kwamba, si jambo la kushangazwa kutolewa matamshi kama hayo na mawaziri hao.
-
Iran na Oman zajadili kuondolewa vikwazo Tehran
Mar 25, 2023 07:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian amezungumza na mwenzake wa Oman, Badr Albusaidi kwa njia ya simu, na wawili hao wamejadili kuhusu hali ya sasa ya mazungumzo ya kuiondolea Jamhuri ya Kiislamu vikwazo vya kidhalimu.
-
Kan'ani aishauri Ufaransa: Badala ya kuibua machafuko katika nchi nyingine, sikilizeni sauti za watu wenu
Mar 25, 2023 02:21Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amezungumzia habari iliyochapishwa kwenye vyombo vya habari kuhusu kuchomwa moto manispaa ya mji wa "Bordeaux", nchini Ufaransa na kusisitiza kwamba, badala ya kuibua machafuko katika nchi nyingine, Ufaransa inapaswa sikiliza sauti za watu wake na kujiepuke kutenda ukatili dhidi yao.
-
Hatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Marekani inataka kuangamzia Uislamu
Mar 24, 2023 13:44Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amezungumzia njama zinazofanywa na Marekani kwa shabaha ya kuuangamiza Uislamu na Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na kusema kuwa, Marekani daima inafanya mikakati ya kujaribu kupenya kwenye imani na fikra za watu kupitia njia za kipropaganda.
-
Iran: Mashambulizi ya Israel dhidi ya Aleppo yanakiuka sheria za kimataifa
Mar 24, 2023 02:48Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani mashambulizi ya anga ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Aleppo (Halab) huko kaskazini mwa Syria na kusisitiza kuwa, uvamizi huo unakanyaga sheria za kimataifa, Hati ya Umoja wa Mataifa mbali na kuwa tishio kubwa kwa amani na uthabiti wa eneo la Asia Magharibi.
-
Kiongozi Muadhamu: Idadi ya wasomaji mahiri wa Qur'ani Tukufu imeongezeka sana nchini Iran
Mar 23, 2023 15:10Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, hii leo idadi ya wasomaji mahiri wa Qur'ani tukufu imeongezeka sana katika Jamhhuri ya Kiislamu ya Iran ikilinganishwa na kabla ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Raisi awapongeza viongozi wa nchi za Kiislamu kwa kuanza Ramadhani
Mar 23, 2023 11:18Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia salamu za pongezi viongozi wa nchi za Kiislamu kwa kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Amir Abdollahian aishukuru Austria kwa kuwa mwenyeji wa mazungumzo ya kuondoa vikwazo
Mar 23, 2023 07:36Hussein Amir- Abdollahian Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezungumza kwa simu na Alexander Schallenberg Waziri wa Mambo ya Nje wa Austria na kupongeza kitendo cha Vienna cha kuwa mwenyeji wa mazungumzo ya kuondoa vikwazo.
-
Nasser Kanaani: Marekani haina ustahiki wa kuzungumzia haki za binadamu
Mar 22, 2023 12:57Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamuu ya Iran amesema kuwa, Marekani haina ustahiki wowote wa kuzungumzia haki za binadamu kutokana na historia yake chafu ya ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Imarati: Mabadiliko katika uhusiano wa Saudi Arabia na Iran ni kwa maslahi ya Asia Magharibi
Mar 22, 2023 12:35Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) amesema kuwa, mabadiliko yaliyotokea katika uhusiano wa Saudi Arabia na Iran ni chanya na kwamba, hilo ni kwa maslahi ya eneo hili la Asia Magharibi.