-
Nasser Kanani: Hatua ya Baraza la Usalama la UN kuhusu kusimamisha vita Gaza haitoshi
Mar 26, 2024 04:23Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema hatua ya Baraza la Usalama kuhusu kusitisha vita katika Ukanda wa Gaza haitoshi. Amesema, hatua muhimu, zaidi ya kupasisha azimio hilo ni kuchukuliwa hatua athirifu ili kufanikisha utekelezaji wa azimio hilo na kusitisha kikamilifu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuondoa kikamilifu mzingiro wa kidhulma dhidi ya Gaza.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akosoa undumakuwili wa Magharibi
Mar 26, 2024 04:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumza kwa simu na mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya katika Masuala ya Nje na Sera ya Usalama na kukosoa vikali vigezo vya undumakuwili na vinavyokinzana vya nchi za Magharibi mkabala wa Palestina na Gaza.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aonana na watungaji tungo za kishairi
Mar 25, 2024 23:26Jioni ya jana Jumatatu ambayo ilisadifiana na usiku wa mwezi 15 Ramadhani, siku ya kukumbuka alipozaliwa Imam Hassan al Mujtaba AS, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alionana na jamii ya washairi na watu wa sanaa na utamaduni na kuzungumza nao kwa karibu na kwa mapenzi makubwa.
-
Shirikisho la Soka la Iran likaribisha pendekezo la Wapalestina la kuwekewa vikwazo Shirikisho la soka la Israel
Mar 25, 2024 08:14Mkuu wa Shirikisho la Soka la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtumia barua Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), akikaribisha mpango uliopendekezwa wa Shirikisho la Soka la Palestina kuhusu kuwekewa vikwazo Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Iran na Oman zasisitizia udharura wa kukomeshwa mara moja jinai za Israel Ghaza
Mar 25, 2024 02:43Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Oman wamefanya mazungumzo ya simu na kutilia mkazo wajibu wa kuchukuliwa hatua za haraka na jamii ya kimataifa za kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi madhlumu na wasio na ulinzi wa Palestina hasa wa Ukanda wa Ghaza.
-
Wairani waandamana kulaani jinai za Israel katika Ukanda wa Gaza
Mar 24, 2024 23:21Wananchi wa Iran wamefanya maandamano makubwa katika sehemu mbalimbali za nchi ukiwemo mji mkuu Tehran, kutangaza mshikamano na wananchi madhulumu wa Palestina wanaoendelea kuuawa, sambamba na kulaani jinai za kutisha zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Ndege ya kivita isiyo na rubani ya Iran ijulikanayo kama 'Gaza' yavuma kimataifa
Mar 24, 2024 08:00Iran imeanza kusambaza bidhaa zake za kijeshi na ulinzi kimataifa, huku gazeti moja la Marekani likisema kuwa sekta ya ulinzi ya Iran imeingia rasmi katika soko la kimataifa kwa kushiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Silaha ya Doha nchini Qatar ambapo imeonyesha ndege ya kisasa ya kivita isiyo na rubani iliyopewa jina la 'Gaza'.
-
Iran: Tuko pamoja na Russia baada ya shambulio la kigaidi la Moscow
Mar 23, 2024 23:22Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mwito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua kali za kuwaadhibu magaidi waliohusika na shambulio la kigaidi kwenye jumba moja la starehe katika viunga vya Moscow, mji mkuu wa Russia.
-
"Mauaji ya kimbara Gaza yamefichua dhati na unafiki wa Wamagharibi"
Mar 23, 2024 04:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mauaji ya kimbari yanayoshuhudiwa katika Ukanda wa Gaza yameweka bayana kuwa nchi za Magharibi zinatumia suala la 'haki za binadamu' kama wenzo wa kisiasa tu.
-
Msemaji wa AEOI: Iran inahitaji vituo 20 vya nyuklia
Mar 23, 2024 04:15Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema Jamhuri ya Kiislamu inapasa kuwa na vituo kati ya 15 na 20 vya nyuklia ili kujidhaminia mahitaji yake ya nishati.