-
Spika wa Bunge: Israel imeshindwa ‘kwa fedheha zaidi’ katika ghasia za Iran kuliko vita vya siku 12
Jan 25, 2026 04:12Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa utawala wa Israel umeshindwa kwa fedheha kubwa zaidi katika ghasia za kigaidi zilizotokea hivi karibuni nchini Iran ikilinganishwa na vita vya siku 12 vya kulazimishwa vya mwezi Juni mwaka jana.
-
Waziri Mkuu wa Malaysia: Tutaendeleza uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na Iran
Jan 25, 2026 04:10Waziri Mkuu wa Malaysia amesisitiza kuwa, nchi yake itataendeleza uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
-
Maafisa na wachambuzi wa Israel: Tusizidishe chumvi; uwezo wa makombora wa Iran si mzaha
Jan 24, 2026 13:13Maafisa na wachambuzi wa Israel, wameonya kuhusu matokeo mabaya ya mzozo wowote na Iran, wakisisitiza kwamba nguvu ya makombora na uwezo wa kijeshi wa Jamhuri ya Kiislamu ni changamoto kubwa kwa Tel Aviv na kwamba Israel haipaswi kupuuzwa ukweli huo.
-
Vinara zaidi ya 140 wa ghasia za karibuni watiwa nguvuni katika mji wa Hamedan
Jan 24, 2026 13:11Askari usalama wa Iran wamefanikiwa kuwatambua na kuwakamata vinara 140 waliohusika katika machafuko ya karibuni hapa nchini kwa ufadhili na kuungaji mkono na nchi za nje. Vinara hao wa ghasia za karibuni wametiwa nguvuni katika mji wa Hamedan, magharibi mwa Iran.
-
Kamanda: Iran itatoa majibu makali kwa vitisho vya Trump
Jan 24, 2026 07:57Kamanda mwandamizi wa jeshi la Iran amesema kwamba Jamhuri ya Kiislamu iko tayari na ina hakika itajibu kwa nguvu vitisho na kauli za Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Iran yamjibu Zelensky; yamwambia dunia imechoka na 'vikaragosi vilivyochanganyikiwa'
Jan 24, 2026 03:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amemkosoa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky kwa kuingilia masuala ya ndani ya Jamhuri ya Kiislamu, na kumwambia bayana kwamba dunia imechoka na "Wanaserere Waliochanganyikiwa."
-
Imamu wa Swala ya Ijumaa Tehran: IRGC ndiyo nguzo kuu ya kuwalinda wananchi na Mapinduzi ya Kiislamu
Jan 23, 2026 14:49Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran, Hujjatul Islam Walmuslimin Haj Ali Akbari, amezungumzia matukio ya hivi karibuni na mashambulizi ya maadui kwenye maeneo mbalimbali yakiwemo ya ya kidini na kusisitiza kuwa: Maadui walidhani kwamba wangeweza kulilazimisha taifa la Iran kurudi nyuma na kudhibiti mitaa na viwanja kupitia vitisho na kuzusha hofu, lakini wananchi ambao ndio wamiliki halisi wa nchi hii, walijitokeza kwenye medani na kukabiliiana ipasavyo na fitina hiyo.
-
IRGC: Mashirika 10 ya ujasusi yaliilenga Iran baada ya Vita vya Siku 12
Jan 23, 2026 14:13Shirika la Ujasusi la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetoa taarifa likisema, machafuko ambayo yamekuwa yakifanyika nchini tangu mwishoni mwa Desemba yalikuwa sehemu ya "fitina iliyopangwa" na mashirika ya ujasusi ya nchi 10 maadui, kwa shabaha ya kuivuruga nchi kupitia vitendo vya vurugu, hujuma na kampeni za upotoshaji zilizoratibiwa kwa vyombo vya habari.
-
Rais Pezeshkian: Mpango wa maadui wa Umma wa Kiislamu ni kueneza ugaidi na machafuko
Jan 23, 2026 07:37Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mpango wa maadui wa Umma wa Kiislamu ni kueneza na kuendeleza ugaidi na ukosefu wa usalama katika eneo kwa kuzusha migogoro ya ndani katika mataifa ya Kiislamu.
-
Russia: Wananchi wa Iran wamesambaratisha njama za maadui
Jan 23, 2026 07:37Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Russia amesema kuwa, machafuko ya hivi karibuni nchini Iran yalifadhiliwa waziwazi kutoka nje ya nchi.