-
Israel yafuta mpango wa kushambulia Beirut baada ya onyo kali la Iran
Jun 02, 2026 09:12Utawala wa Israel umeachana na mpango wake wa kufanya mashambulizi makali ya ya kijeshi dhidi ya mji mkuu wa Lebanon, Beirut. Haya yameelezwa siku ya Jumatatu na Rais wa Marekani, Donald Trump, kufuatia onyo kali kutoka kwa Iran kwamba haitavumilia wimbi jipya la uvamizi dhidi ya Beirut, hatua ambayo ingekiuka makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na Marekani.
-
Qalibaf: Marekani ni lazima ilipe gharama za jinai za Israel Lebanon
Jun 02, 2026 03:01Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) Mohammad Baqir Qalibaf ameilaani Marekani kwa kuhusika katika mashambulizi ya utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Lebanon na kueleza kuwa Washington lazima ilipe gharama ya jinai za kivita zinazofanywa na utawala huo ghasibu dhidi ya Lebanon.
-
IRGC yapiga kambi ya anga ya Marekani iliyohusishwa na shambulio dhidi ya mnara wa mawasiliano kusini mwa Iran
Jun 02, 2026 02:59Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema limefanya shambulio la kulipiza kisasi dhidi ya kambi ya anga iliyotumiwa na Marekani kuanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya mnara wa mawasiliano katika kusini mwa Iran.
-
Kauli ya Umoja wa Ulaya inayolaani kujilinda halali kwa Iran ni ya kinafiki
Jun 01, 2026 11:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza kuwa Umoja wa Ulaya unapasa kuzingatia kanuni ya utawala wa sheria na Hati ya Umoja wa Mataifa ambazo unadai kufungamana nazo.
-
Iran yalaani vikali shambulio la polisi wa Uholanzi dhidi ya mke mjamzito wa Mpalestina
Jun 01, 2026 09:13Iran imelaani vikali shambulio la kikatili lililofanywa na polisi wa Uholanzi dhidi ya mke mjamzito wa mwanamume Mpalestina, ikitoa wito kwa serikali ya Uholanzi kuchunguza tukio hilo na kuwawajibisha waliohusika.
-
Spika Qalibaf: Iran inamrudisha nyuma adui kupitia umoja wa kitaifa
Jun 01, 2026 03:24Mohammad Baqir Qalibaf Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa Iran, kupitia umoja wa kitaifa, inamrudisha nyuma adui katika vita vinavyoacha historia.
-
Kwa nini Trump anatapatapa kati ya vitisho na makubaliano?
May 31, 2026 13:18CNN imesema katika ripoti kwamba: "Serikali ya Marekani huchanganyikiwa linapokuja suala la nyuklia la Iran." Katika kipindi cha wiki kadhaa zilizopita, Rais Donald Trump wa Marekani amebadilisha misimamo yake mara kadhaa kuhusu hatima ya hifadhi ya urani iliyorutubishwa ya Iran.
-
Trump anakabiliwa na chaguzi 'mbaya' au 'mbaya zaidi' kuhusu Iran: Jenerali wa IRGC
May 31, 2026 12:56Kamanda wa cheo cha juu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) anasema Rais wa Marekani, Donald Trump, hana chaguo zuri kuhusu Iran na anapaswa kuchagua kati ya njia "mbaya" au "mbaya zaidi".
-
Bunge la Iran kupigia kura mpango wa usimamizi wa Lango Bahari la Hormuz 'hivi karibuni'
May 31, 2026 04:25Bunge la Iran linatarajiwa kupitia na kuidhinisha sheria inayorasimisha usimamizi na mamlaka ya Jamhuri ya Kiislamu juu ya Mlango-Bahari wa Hormuz.
-
Waasi wa RSF wanaoungwa mkono na UAE wauwa raia 27 siku ya Eid nchini Sudan
May 30, 2026 11:49Waasi wa RSF wamewaua angalau raia 27, wakiwemo wazee, katika shambulio dhidi ya vijiji vilivyoko magharibi mwa Bara katika jimbo la North Kordofan nchini Sudan.