-
Baqaei: Hatua hatari za kukurupuka za Ukraine zitapewa majibu muwafaka
Jul 28, 2026 03:45Shambulio la Ukraine dhidi ya meli ya Iran lilikuwa kinyume cha sheria, limekiuka Mkataba wa Umoja wa Mataifa na ni kitendo hatari cha kichokozi.
-
Baghaei: Marekani imesaliti diplomasia kwa mara ya tatu
Jul 27, 2026 09:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, amesema kuwa Marekani imeisaliti diplomasia kwa mara ya tatu, akieleza kuwa hatua za Washington zimeendelea kudhoofisha juhudi za kutatua migogoro kupitia mazungumzo.
-
Je, Marekani imefikia mkwamo wa kimkakati katika mgogoro wake na Iran?
Jul 27, 2026 07:10Wachambuzi wengi mashuhuri wa Marekani wanaonya kwamba Washington inatembea kwenye njia ya mgogoro na Iran ambayo si lazima ifanikiwe kisiasa au kistratijia. Wanaamini kwamba changamoto kuu inayoikabili Marekani kwa sasa si kuanzisha vita, bali ni kutafuta njia ya kujiondoa kwenye mkwamo unaozidi kuongezeka siku hadi siku.
-
Kiongozi Muadhamu: Uimara wa Hizbullah ni ujumbe kwa mataifa huru
Jul 27, 2026 03:59Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ameisifu harakati ya Hizbullah kwa msimamo wake thabiti na usioyumba katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema, kuwa uimara wa harakati hiyo ya Lebanon ni ujumbe wenye nguvu wa ukombozi kwa mataifa yaliyodhulumiwa duniani kote.
-
Pezeshkian: Uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na Marekani ufuatiliwe kisheria kimataifa
Jul 27, 2026 03:57Rais Masoud Pezeshkian amelaani mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani dhidi ya miundombinu ya usafiri ya Iran akiyataja kuwa ni "uhalifu wa kivita," na kutaka hatua za kisheria za kimataifa zichukuliwe dhidi ya uharibifu uliosababishwa na nchi hiyo kwenye vituo vya mpakani, vituo vya forodha na mitandao ya usafirishaji.
-
IRGC yazionya Israel na Uingereza kuhusu kuisaidia Marekani katika vita dhidi ya Iran
Jul 26, 2026 13:20Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limezionya Uingereza na utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kuisaidia na kushirikiana na Marekani katika vita vyake vya jinai na uchokozi dhidi ya Iran.
-
Iran yasifu mazungumzo ‘yenye tija’ na Oman kuhusu usafirishaji katika Lango-Bahari la Hormuz
Jul 26, 2026 13:18Iran imesema kuwa mazungumzo kati yake na Oman kuhusu safari salama za meli katika Lango Bahari la Hormuz yamepiga hatua nzuri, lakini hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika katika suala la usafirishaji kupitia njia hiyo muhimu ya maji.
-
Jeshi la Iran: Karibu miundombinu yote ya Marekani huko Erbil imeharibiwa
Jul 26, 2026 13:16Msemaji wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza kuwa karibu miundombinu yote ya Marekani katika mji wa Erbil, kaskazini mwa Iraq imeharibiwa.
-
Trump Aidhinisha Saudi Arabia kuwa na Mpango wa Nyuklia: Mfano Mwingine wa Undumakuwili wa Marekani
Jul 26, 2026 09:40Rais Donald Trump wa Marekani hatimaye ametiliana saini na Saudi Arabia makubaliano ya ushirikiano wa nishati ya nyuklia kwa matumizi ya kiraia, ambayo yanafungua njia kwa ajili ya shughuli za kurutubisha urani ndani ya ufalme huo.
-
Araqchi alaani vikali shambulio la Ukraine dhidi ya meli ya biashara ya Iran Bahari ya Caspian
Jul 26, 2026 03:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amelaani vikali shambulio la kijeshi lililofanywa na utawala wa Ukraine dhidi ya meli ya biashara ya Iran katika Bahari ya Caspian.