-
Baqaei: Rasimu ya azimio inasisitiza kuzuiwa mashambulizi dhidi ya taasisi za nyuklia za malengo ya kiraia
Sep 16, 2025 12:11Esmail Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ametoa taarifa kuhusu rasimu ya azimio la Iran katika Mkutano Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) unaoendelea Vienna, Austria ambayo inalenga kuzuia mashambulizi kwenye vituo vya nyuklia vinavyoendesha shughuli zake kwa malengo ya amani na ya kiraia.
-
Rais wa Iran azitahadharisha nchi za Kiislamu Doha: Hakuna nchi itakayokuwa salama na uchokozi wa Israel
Sep 16, 2025 07:42Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mashambulizi ya Israel ya Septemba 9 dhidi ya Qatar yameonyesha kuwa hakuna nchi ya Kiarabu au ya Kiislamu iliyo salama kutokana na vitendo vya uchokozi vya utawala huo.
-
Iran yatwaa taji la ubingwa wa dunia wa Miereka 2025, yaziacha nyuma Russia na Marekani
Sep 16, 2025 06:48Timu ya taifa ya mchezo wa miereka aina ya Freestyle ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Mashindano ya Dunia ya Miereka ya mwaka 2025 yanayofanyika mjini Zagreb, Croatia kwa kunyakua jumla ya medali tano na kulitwaa taji hilo kabla ya muda wa mashindano kumalizika.
-
Eslami: Shambulio dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran lilikuwa shambulio dhidi ya itibari ya IAEA
Sep 16, 2025 03:09Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amesisitiza katika Mkutano Mkuu wa 69 wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kwamba: Mashambulio ya Marekani na utawala wa Israel dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran si tu kuwa ni jinai na uoga, bali pia ni shambulio la moja kwa moja dhidi ya itibari ya Wakala huo na mfumo wake wa ulinzi.
-
Rais wa Iran afanya mazungumzo na Amir wa Qatar
Sep 15, 2025 11:20Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo amekutana na kufanya mazungumzo na Amir wa Qatar katika mji mkuu wa nchi hiyo Doha.
-
Araghchi: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko bega kwa bega na Qatar na Waislamu wote
Sep 15, 2025 06:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ambaye yuko mjini Doha, Qatar kushiriki katika mkutano wa dharura wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Kiislamu na Kiarabu, amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko bega kwa bega na ndugu zake Waislamu wote.
-
Iran yapinga madai ya G7, na kuyataja kuwa ya uongo
Sep 14, 2025 09:08Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imekanusha vikali tuhuma zilizotolewa katika taarifa ya pamoja ya G7 na washirika wake, ikizitaja kuwa ni za kupotosha, zisizo na msingi, na ni mbinu ya kisiasa ya kujiepusha na lawama.
-
Juhudi za mhimili wa Magharibi za kuchafua jina la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Sep 14, 2025 08:16Wanachama wa Mchakato wa Radiamali ya Haraka wa Kundi la G7 ambazo ni nchi za Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan, Uingereza, Marekani na Umoja wa Ulaya, pamoja na Australia na New Zealand, katika taarifa ya pamoja siku ya Ijumaa walidai kulaani hatua za Iran kuhusiana na eti kuongezeka kwa kampeni ya ukandamizaji unaotekelezwa nje ya mipaka yake.
-
Iran yazionya Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani kuhusu vikwazo
Sep 14, 2025 06:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ametoa onyo kali kwa Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani kwamba iwapo zitaendeleza juhudi zao za kuanzisha tena vikwazo vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran, basi zitakumbwa na madhara yasiyoweza kurekebishwa.
-
Mkuu wa zamani IRGC azitahadharisha Saudia, Uturuki na Iraq, asema; mabomu ya Israel yanawasubiri
Sep 14, 2025 03:26Kamanda Mkuu wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amezitahadharisha nchi za eneo zikiwemo Saudi Arabia, Uturuki na Iraq kwamba ziko katika hatari ya kukabiliwa na uvamizi wa Israel iwapo nchi za kanda hii zitashindwa kuunda "muungano wa kijeshi" dhidi ya utawala wa Kizayuni.