-
Araghchi: Iran imejiandaa zaidi kukabiliana na uhasama wa Israel
Nov 21, 2025 08:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu sasa imejiandaa kuliko wakati wowote kukabiliana na uhasama wowote kutoka Israel.
-
Azimio jipya la Bodi ya Magavana ya IAEA lina lengo la kufidia kushindwa Marekani na Troika ya Ulaya
Nov 21, 2025 03:03Mwakilishi wa kudumu na balozi wa Iran katika taasisi za kimataifa zenye makao yake mjini Vienna Austria amesema kupitishwa azimio la kisiasa dhidi ya nishati ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani ni jaribio la Marekani na Umoja wa Ulaya ili kufidia kushindwa kwao katika utaratibu wa Snapback huko New York.
-
Kharrazi amwambia Trump: Huwezi kuilazimisha Iran kufumbia macho haki zake
Nov 20, 2025 10:17Kamal Kharrazi, mshauri wa ngazi za juu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametoa ujumbe wa wazi kwa Marekani na kusema kuwa, siasa za Donald Trump za kutumia mabavu haziwezi kuifanya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kubadilisha njia yake.
-
Iran yalaani shambulio la kigaidi la Israel na Marekani dhidi ya wakimbizi ya Palestina Lebanon
Nov 20, 2025 10:16Iran imelaani vikali shambulio la hivi karibuni la kigaidi lililofanywa na Israel kwa msaada kamili wa Marekani dhidi ya kambi kubwa zaidi ya wakimbizi ya Palestina kusini mwa Lebanon ikisema kwamba Marekani inahusika moja kwa moja na jinai hiyo.
-
Araghchi: Hatutakubali kwa namna yoyote ile kushusha urutubishaji urani hadi kiwango cha sifuri
Nov 20, 2025 06:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesema: "hatutakubali kwa namna yoyote ile kushusha urutubishaji wa urani hadi kiwango cha sifuri kwa sababu hili limekuwa ni jambo la fakhari na heshima kwa taifa, tumetumia gharama nyingi sana za kimaada na kimaanawi kwa ajili yake, na tumepoteza wanasayansi kadhaa waliouawa shahidi kwa ajili ya kulidumisha".
-
Iran: Azimio la Marekani lililopasishwa na UN kuhusu Gaza linahalalisha ukaliaji mabavu
Nov 19, 2025 12:46Iran imekosoa azimio lililoandaliwa na Marekani na kupasishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linaloweka utaratibu wa kutumwa Gaza usimamizi wa nchi ajinabi na kutahadharisha kuwa azimio hilo linadhoofisha haki za msingi za watu wa Palestina.
-
Grossi: Wakaguzi wa wakala wa IAEA wamerejea Iran
Nov 19, 2025 12:05Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema katika kikao cha robo mwaka cha Bodi ya Magavana ya wakala huo kwamba: "Wakaguzi wa IAEA wamerejea Iran na wamefanya ukaguzi katika vituo ambavyo havikuathiriwa na mashambulizi ya Juni, lakini ushirikishwaji zaidi unahitajika ili kurejesha ukaguzi kamili."
-
Rais Pezeshkian: Iran inalenga kuimarisha uhusiano na Oman
Nov 19, 2025 06:59Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesifu uhusiano imara kati ya Iran na Oman, na kueleza kuwa Tehran ina imani kwamba uhusiano wa pande mbili utaendelea kukua kwa "nguvu na uthabiti.
-
Bin Salman: Tunajaribu kupatanisha baina ya Iran na Marekani
Nov 19, 2025 02:49Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia ambaye kimsingi ndiye kiongozi nambari moja wa nchi hiyo amesema: "Tutafanya kila tunavyoweza kuhakikisha kunafikiwa makubaliano kati ya Iran na Marekani; (ninaamini kwamba) Tehran pia iko tayari kusaini makubaliano hayo."
-
Iran yapendekeza mfumo wa malipo wa kidijitali katika Jumuiya ya Shanghai
Nov 19, 2025 02:24Mohammad Reza Aref Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran amependekeza kuanzisha mfumo wa pamoja wa malipo ya kidijitali ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi 10 wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO).