Waziri Mkuu wa Malaysia: Tutaendeleza uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na Iran
-
Waziri Mkuu wa Malaysia Anwar Ibrahim
Waziri Mkuu wa Malaysia amesisitiza kuwa, nchi yake itataendeleza uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Akibainisha kuwa uhusiano wa Kuala Lumpur na Tehran kwamba, bado haujabadilika, Waziri Mkuu wa Malaysia Anwar Ibrahim alisema: "Mimi binafsi nimeshirikiana na Iran mara mbili na mawaziri kadhaa wametumwa huko. Katika masuala yote yanayohusiana na uhusiano wa kimataifa, ni lazima tuchukue hatua kwa busara."
Waziri Mkuu wa Malaysia Anwar Ibrahim, akijibu swali kutoka kwa mbunge wa bunge la nchi hiyo kuhusu iwapo msimamo wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kutoza ushuru wa 25% kwa bidhaa kutoka nchi yoyote inayofanya biashara na Iran utaathiri uhusiano au biashara ya Malaysia na Iran, alisema: "Malaysia itaendelea na uhusiano wake wa kibiashara na kidiplomasia na Iran."
Kuhusu biashara na Iran, alisema: "Uhusiano wetu na nchi hii unabakia kuwa imara. Mimi binafsi nimeamiliana na Iran mara mbili na mawaziri kadhaa wametumwa huko. Katika masuala yote yanayohusiana na uhusiano wa kimataifa, ni lazima tutende kwa busara."
Afisa huyo mkuu wa Malaysia aliendelea kusisitiza kwamba, nchi yake inaendelea kujitolea kutetea haki na uhuru wa Iran kama msingi wa sera na kwamba kuhusu uhusiano na Iran, uhusiano huu unabakia imara. Alisema: "Tunaendelea kuunga mkono na kutetea haki na uhuru wa Iran. Hii ndiyo kanuni na msingi tunaoufuata."