-
Iran: Mashambulizi yataendelea hadi adui atakapojisalimisha kikamilifu
Jul 26, 2026 03:09Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Baqer Zolghadr amesema mashambulizi ya vikosi vya jeshi la Iran yataendelea hadi adui atakapojisalimisha kikamilifu na hadi kulipiza kisasi kwa damu ya mashahidi.
-
Mawaziri wa Mambo ya nje wa Iran na Russia wajadili uchokozi wa Marekani
Jul 25, 2026 11:12Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kujitolea kikamilifu katika kulinda maslahi yake ya kitaifa na usalama wake, akisisitiza kuwa ukosefu wa utulivu wa sasa katika Lango Bahari la Hormuz ni matokeo ya moja kwa moja ya ukiukaji wa ahadi na jinai zilizofanywa na Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran yalaani kimya cha EU kuhusu jinai za kivita za Marekani na Israel
Jul 25, 2026 10:59Iran imekosoa vikali kauli za mkuu wa diplomasia wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Iran, huku ikibaki kimya kuhusu jinai za vita zinazofanywa na Marekani na Israel dhidi ya nchi hii, na kuzitaja kuwa ni “aina safi kabisa ya unafiki.”
-
Namna Trump Anavyodhihirisha Hasara ya Vita na Iran kama Mafanikio
Jul 25, 2026 09:17Kwa kuchapisha orodha ya wahanga wa vita tofauti vya Marekani, Rais Donald Trump amejaribu kudhihirisha mzozo na Iran kama "vita vyenye gharama ya chini, na vilivyofanikiwa" ambapo sasa anajivunia vifo vya wanajeshi 18 wa Marekani walioangamia katika vita vya karibuni.
-
IRGC yashambulia kambi za Marekani Kuwait na Bahrain, yaonya raia wakae mbali na maeneo walipo Wamarekani
Jul 25, 2026 03:11Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa kutekeleza mashambulizi mapya dhidi ya ngome za kijeshi za Marekani nchini Kuwait na Bahrain, huku likitoa onyo kwa raia katika nchi zinazowapa hifadhi wanajeshi wa Marekani kuondoka mara moja na kuwa mbali kwa angalau mita 500 kutoka maeneo yanayotumiwa na wanajeshi hao.
-
Mkuu wa Idara ya Mahakama: Iran Haina Uadui na nchi jirani
Jul 25, 2026 03:08Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Gholam-Hossein Mohseni Eje’i, amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haina uadui wowote dhidi ya nchi jirani, akibainisha kuwa mashambulizi ya kulipiza kisasi hulenga vituo vilivyotumika kutekeleza mashambulizi ya Marekani katika eneo hili.
-
Ayatullah Khatami: Watu wa Iran wamesimama imara mitaani hadi ushindi wa mwisho
Jul 24, 2026 10:02Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, watu wa Iran wamesimama imara mitaani hadi ushindi wa mwisho.
-
Araghchi: Kimya na misimamo ya kinafiki kwa mashambulizi dhidi ya Iran kunawapa kiburi wavamizi kuendeleza uhalifu
Jul 24, 2026 08:46Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, ukimya na misimamo ya kindumakuwili kuhusu mashambulizi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kunawapa nguvu na kuwahamasisha wavamizi kuendelea kutekeleza vitendo vyao.
-
Jeshi la SEPAH laionya Uingereza na kuitaka isizidi kulichafua faili lake
Jul 24, 2026 08:44Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) limetoa onyo kali kwa serikali ya kifalme ya Uingereza, likiitaja kuwa miongoni mwa nchi zilizokuwa na mchango mkubwa katika mashambulizi ya hivi karibuni yaliyofanywa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Baqaei aionya GCC na Jordan: Kushiriki uchokozi dhidi ya Iran ni kielelezo cha uvamizi
Jul 24, 2026 08:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei, amelionya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC) pamoja na Jordan kwamba, ushiriki wowote katika mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran utachukuliwa kuwa ni kitendo cha uchokozi wa kijeshi.