-
Rais wa Iran: Hatuna nia ya kuwa na migongano na nchi za Kiislamu
Mar 21, 2026 06:22Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ametoa ujumbe maalumu kwa mnasaba wa mwaka mpya wa Kiirani wa Hijria Shamsia, 1405 na kusema: “Mwaka huu, kuliko wakati mwingine wowote, tunaihitaji Nowruz; Nowruz inayonyesha umoja kwa dunia.”
-
Jenerali Qaani: Iran itawashangaza wengi katika medani ya vita
Mar 21, 2026 06:22Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema: Mrengo wa Haki utaendelea kuwa na uwezo na nguvu zaidi kila siku, na kwamba Iran itawashangaza wengi katika uwanja wa vita na utawala wa Kizayuni pamoja na Marekani.
-
Mkurugenzi wa zamani wa Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi cha Marekani: Mashambulizi ya Washington yamewafanya Wairani Kuungana Zaidi
Mar 21, 2026 06:18Mkurugenzi wa zamani wa Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi cha Marekani amekiri kwamba viongozi wakuu wa utawala wa Kizayuni na washirika wake wanaochochea vita wa Marekani ndio walimshinikiza rais wa nchi hiyo kuishambulia Iran.
-
Araqchi: Kushiriki Uingereza katika mashambulizi dhidi ya Iran kutasajiliwa katika historia ya uhusiano wa nchi mbili
Mar 20, 2026 08:10Sayyid Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezungumza kwa simu na mwenzake wa Uingereza, Yvette Cooper, kuhusu taathira za vita vya kulazimishwa vya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran na hali ya mambo ya sasa katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Msemaji wa IRGC: Uzalishaji wa makombora unaendelea hata wakati wa vita
Mar 20, 2026 04:52Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran amesema: "Hakuna wasiwasi katika uwanja wa makombora kwa sababu tunazalisha makombora hata wakati wa vita, jambo ambalo linashangaza, na hakuna tatizo maalumu katika suala la hifadhi ya makombora yetu."
-
Iran yamjibu waziri wa mambo ya nje wa Saudia
Mar 19, 2026 23:28Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza umuhimu wa hatua za haraka kutoka kwa nchi za eneo la Asia Magharibi ili kuzuia kuendelea kwa matumizi ya ardhi na miundombinu yao na Marekani pamoja na utawala wa Kizayuni katika mashambulizi dhidi ya Iran.
-
Onyo la Pezeshkian kuhusu uhalifu wa Marekani na utawala wa Kizayuni: Moto wa mgogoro huu utaathiri wengi
Mar 19, 2026 23:27Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, ametoa onyo kuhusu uhalifu wa Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran, akisisitiza kuwa moto wa mgogoro huu unaweza kuenea na kuwaathiri wengi.
-
Jeshi la Iran lalenga ndege ya kivita ya Marekani aina ya F‑35
Mar 19, 2026 23:13Ndege ya kivita ya kimkakati aina ya F‑35 ya Jeshi la Marekani imelengwa kwa kombora na kuharibiwa vibaya ikiwa inaruka katika anga ya kati mwa Iran kwa lengo la kutekeleza mashambulizi.
-
Baqaei: Raia wote wa US wanapaswa kutangaza kuchukizwa na vita haramu vya Trump
Mar 19, 2026 07:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa vita vya sasa si vita vya wananchi wa Marekani. Ismail Baqaei ameeleza haya katika ujumbe aliotuma katika mtandao wa kijamii wa X baada ya kujiuzulu Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kupambana na Ugaidi wa Marekani, Joseph Kent.
-
Pezeshkian: Taathira za mashambulizi dhidi ya miundo mbinu ya nishati ya Iran zitaitatiza dunia nzima
Mar 19, 2026 07:20Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ametuma ujumbe na kuandika kuwa: Mashambulizi dhidi ya miundo msingi ya nishati ya Iran yana taathira ambazo ukubwa wake utaitatiza dunia nzima.