-
Hatua mpya katika uhusiano wa Iran na Kenya; kianzio katika diplomasia ya Kiafrika ya Tehran?
Dec 09, 2025 09:12Balozi wa Iran nchini Kenya amesema kuwa uhusiano kati ya Tehran na Nairobi umeingia katika hatua mpya.
-
Iran yalalamikia FIFA kuhusu nara ya mechi yake na Misri katika Kombe la Dunia
Dec 09, 2025 03:59Shirikisho la Soka la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limewasilisha malalamiko rasmi kwa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, dhidi ya hatua isiyo ya kimichezo ya kamati ya maandalizi ya Kombe la Dunia mjini Seattle, Marekani.
-
Mwanadiplomasia: Iran iliitia Israel hasara 'kubwa na iliyoenea' wakati wa Vita vya Siku 12
Dec 09, 2025 00:02Mwanadiplomasia mwandamizi wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu iliusababishia utawala wa kizayuni wa Israel uharibifu 'mkubwa na ulioenea' wakati wa uvamizi wake uliofanya mwezi Juni dhidi ya Iran kwa uungaji mkono wa Marekani.
-
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Azerbaijan zaazimia kuimarisha zaidi ushirikiano
Dec 08, 2025 07:48Seyyed Abbas Araghchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye alielekea Baku kushauriana na maafisa wakuu wa Jamhuri ya Azerbaijan leo asubuhi amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa nchi hiyo Ilham Aliyev.
-
Tarehe 16 Azar; Nembo ya utamaduni wa muqawama na harakati ya uhuru
Dec 08, 2025 07:31Tarehe 16 mwezi Azar inayosadifiana na Disemba 7 imesajiliwa katika kalenda rasmi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni "Siku ya Mwanachuo", siku ambayo ni nembo ya mapambano, kupigania haki na kusimama kidete tabaka la wasomi dhidi ya dhulma na ubeberu wa madola ya kigeni.
-
Araghchi: Marekani haiko tayari kwa mazungumzo ya manufaa kwa pande mbili, ya usawa na ya kuheshimiana
Dec 08, 2025 03:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema, Tehran imefikia hitimisho kwamba Marekani haiko tayari kwa mazungumzo ya manufaa kwa pande mbili, ya usawa na yanayofanyika kwa msingi wa kuheshimiana.
-
Iran: Mkakati mpya wa Usalama wa Taifa wa Marekani unaandikwa hasa kwa ajili ya Israel
Dec 07, 2025 23:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Mkakati mpya wa Usalama wa Taifa wa Marekani (NSS) unaobainisha misingi na vipaumbele vya Washington katika sera za nje kimsingi ni hati ya usalama kwa ajili ya utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Qalibaf azionya nchi jirani kutoijaribu Iran kuhusu visiwa vitatu vya Ghuba ya Uajemi
Dec 07, 2025 07:39Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge la Iran) Mohammad Baqer Qalibaf amepuuzilia mbali madai ya kukaririwa kuhusu visiwa vitatu vya Iran katika taarifa ya mwisho ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC), akiyaonya mataifa jirani kutoijaribu azma ya Jamhuri ya Kiislamu ya kulinda mamlaka yake ya kujitawala na umoja wa ardhi nzima ya nchi hii.
-
Spika Qalibaf: Marekani ina chuki ya kihistoria na mwanachuo wa Kiirani
Dec 07, 2025 03:22Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa: Mfumo wa kibeberu kinara wake akiwa Marekani una chuki na uadui wa kihistoria dhidi ya mwanachuo wa Kiirani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Hivi sasa mpira uko upande wa Marekani
Dec 07, 2025 03:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Ira amesema iwapo Marekani itabadili mkondo wake, Iran nayo itakuwa tayari kupata matokeo ya haki na usawa.