-
Jeshi la majini la Iran lasaini hati ya ushirikiano wa kimkakati na nchi za eneo la Kaspi zenye ukanda wa pwani
Oct 08, 2025 08:59Makamanda wa majeshi ya majini ya Iran, Russia, Kazakhstan na Azerbaijan wametia saini mkataba wa ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuimarisha usalama katika maji ya pamoja.
-
Qalibaf: Kimbunga cha al-Aqswa kimeipeleka dunia upande wa kuufuta "Umarekani" na kutetea wanaodhulumiwa
Oct 08, 2025 04:20Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, operesheni ya Kimbunga cha al-Aqswa iliyotokelezwa na wanamuqawama wa Palestina dhidi ya Israel iliipeleka dunia upande wa kuufuta "Umarekani" na kutetea wanaodhulumiwa.
-
Araghchi: Wamarekani wataabani kuingia vitani kupigana kwa ajili ya "vita visivyo na mwisho" vya Israel
Oct 07, 2025 23:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametoa mjibizo kwa kauli ya hivi karibuni ya Rais wa Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu na kueleza kwamba: Wamarekani wataabani kuingia vitani kupigana kwa ajili ya "vita visivyo na mwisho" vya Israel.
-
Ulaya haina haki ya kutoa maoni kuhusu uwezo wa kiulinzi wa Iran
Oct 07, 2025 07:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amepinga vikali madai ya uingiliaji kati na yasiyo na msingi ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi na Umoja wa Ulaya, alkiwaonya viongozi wa nchi za Ulaya na Magharibi kwamba hawana haki ya kusema chochote kuhusu uwezo wa kiulinzi wa Iran.
-
Araghchi: Israel inatumia mamilioni ya dola kulipa watu waongope mitandaoni
Oct 07, 2025 03:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi ameshutumu kampeni ya propaganda iliyofichuliwa hivi karibuni ya Israel, yenye lengo la kuhamasisha uungwaji mkono kwa utawala huo kwenye mitandao ya kijamii.
-
Iran yaibuka ya 3 katika Mashindano ya Riadha ya Walemavu India
Oct 07, 2025 02:38Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imemaliza katika nafasi ya tatu katika Duru ya 12 ya Mashindano ya Riadha ya Walemavu yaliyofanyika nchini India.
-
Kallas asisitiza tena kuendelezwa diplomasia ya nyuklia na Iran
Oct 06, 2025 08:57Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ambaye alielekea Kuwait kuhudhuria Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Usalama na Ushirikiano wa Kikanda kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa kutekelezwa utaratibu kwa jina la Snapback hakumaanishi kufikia kikomo diplomasia na Iran.
-
Iran: Marekani na Israel zinabeba dhima kwa mashambulizi haramu dhidi ya vituo vya nyuklia
Oct 06, 2025 08:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Marekani na utawala wa Israel zinabeba dhima kwa mashambulizi yaliyo kinyume cha sheria zilizoyafanya dhidi ya taasisi za nyuklia za Iran zinazoendesha shughuli zake kwa malengo ya amani na ya kiraia na pia mashambulizi ya pande mbili hizo dhidi ya umoja wa ardhi na mamlaka ya kujitawala nchi hii.
-
Kamanda wa IRGC: Iran itajibu kwa ukali na nguvu zaidi uchokozi wa maadui
Oct 06, 2025 03:58Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Meja Jenerali Mohammad Pakpour amesisitiza kuwa, Jeshi la Iran limejiandaa kikamilifu kutoa jibu thabiti na kali kwa chockochoko tarajiwa za maadui.
-
Iran yaunga mkono uamuzi wa Palestina juu ya usitishaji vita Gaza; lakini yaonya...
Oct 06, 2025 02:21Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema itaunga mkono uamuzi wowote wa watu wa Palestina na Muqawama kuhusu pendekezo la kusitisha mapigano Gaza linaloungwa mkono na Marekani, huku ikiionya jamii ya kimataifa kuhusu mwelekeo hatari wa mpango huo na historia ya kutokuwa na muamana Israel.